To Chat with me click here

Thursday, June 28, 2012

JINSI HALI YA DR. ULIMBOKA ILIVYO KWA SASA

Dr. Steven Ulimboka kama aonekanavyo pichani, baada ya kukutwa akiwa hoi kwa kufanyiziwa na watu wasio julikani.

Dr. Ulimboka akiwa ndani ya gari akipelekwa hospitali kwa ajili ya matibabu, huku akiwa ameumia vibaya sana kutokana na kufanyiziwa huko.

Hapa akiwa anakunywa maji (Uhai) ili kupoza koo kidogo. Kwakweli hali hii inasikitisha sana.

Hapa Dr. Ulimboka akiwa hospitali ya Taifa, Muhimbili akipata matibabu kutokana na kufanyiwa na watu hao ambao mpaka sasa hawajajulikana.

CHADEMA yalaani Dk Ulimboka kushambuliwa

 Dr. Steven Ulimboka

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema), kimelaani kukamatwa na kushambuliwa kwa viongozi wa madaktari ikiwamo Dk Ulimboka Steven ikieleza kuwa hatua hiyo haiwezi kuwa suluhu bali itachochea zaidi mgogoro wa madaktari na Serikali.

Taarifa iliyotolewa jana na Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa Chadema, John Mnyika inaeleza pia kwamba udhaifu wa Serikali kuharakisha kwenda mahakamani kabla ya Bunge kupewa fursa ya kujadili madai ya madaktari na kuisimamia Serikali umelifikisha taifa katika hali iliyopo sasa.

"Nalaani uamuzi wa Serikali wa kutumia vyombo vya dola kukamata na kushambulia viongozi wa madaktari ikiwemo Dk Ulimboka Steven kwa hauwezi kuwa suluhu bali utachochea zaidi mgogoro kati ya madaktari na Serikali," ilisisitiza sehemu ya taarifa hiyo ya Mnyika na kuongeza:

“Nichukue fursa hii kuwaomba madaktari kufanya kila kinachowezekana kuokoa uhai wa wagonjwa katika kipindi hiki kigumu.” Mnyika alisema kuwa ameomba wabunge wapewe nakala ya Taarifa ya Kamati ya Huduma za Jamii kuhusu madai ya madaktari na hoja ya taarifa husika iwekwe katika orodha ya shughuli za Bunge katika mkutano wa Bunge unaoendelea ili ijadiliwe na kupitisha maazimio, kuwezesha hatua za muda mfupi, wa kati na muda mrefu kuupatia ufumbuzi mgogoro huo na kuboresha sekta ya afya nchini.

“Natarajia kwamba Spika atawezesha kamati kuwasilisha taarifa yake na Bunge kujadili baada ya Serikali kutoa kauli yake bungeni,”alisema. Mnyika alisema ikiwa wabunge wataelezwa ukweli na kupewa taarifa kamili wataweza kuisimamia Serikali na kuwaeleza ukweli madaktari kipi kinawezekana na kipi hakiwezekani.

Alisema kuwa ingawa Waziri Mkuu Mizengo Pinda ametoa maelezo bungeni kuwa Serikali itatoa kauli bungeni kuhusu mgomo huo, Bunge halitaruhusiwa kujadili kauli husika, hivyo kukoseshwa fursa ya kuisimamia Serikali kwa niaba ya wananchi.

Mchango wangu Bungeni-Hotuba ya Waziri Mkuu: Haki za Uraia, Mafuta/Gesi Asilia na Uwajibikaji


Unyanyasi wa Watu wa Kigoma
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kuchangia Hotuba hii ya Waziri Mkuu. Jana Mheshimiwa Waziri amekuja kuomba Bunge limuidhinishie jumla ya shilingi trilioni 3.8 kwa ajili ya Ofisi yake na taasisi zote zilizo chini ya Ofisi yake pamoja na takribani shilingi bilioni 113 kwa ajili ya Bunge. Fedha zote hizi takribani shillingi trilioni 3.2 zinakwenda Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla hatujaweza kumuidhinishia Mheshimiwa Waziri Mkuu fedha hizi na yeye kama Mkuu wa Shughuli za Serikali, msimamizi wa kazi za Serikali za kila siku na ambaye anaangalia utendaji wa takribani Mawaziri, wote ni vizuri aweze kutoa majibu kwa baadhi ya masuala ambayo mengine ameyaainisha kwenye hotuba yake, lakini mengine hakuyaainisha katika hotuba yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitaanza na Kigoma. Mheshimiwa Waziri Mkuu katika ukurasa wa 51 wa Hotuba yake amezungumzia masuala ya ulinzi na usalama lakini hakugusia kabisa operesheni ambazo zinaendelea hivi sasa katika Mkoa wa Kigoma nadhani na Mkoa wa Kagera kuhusiana na masuala ya wahamiaji haramu. Hivi tunavyozungumza ni kwamba mamia ya watu wa Kigoma wameonyeshwa kwamba siyo raia wa Tanzania. Utaratibu huu umekuwa ukiendelea mwaka hadi mwaka. Napenda Mheshimiwa Waziri Mkuu akumbuke historia baada ya Vita vya Kwanza vya Dunia kati ya mwaka 1918 na mwaka 1924 Kigoma haikuwa sehemu ya Tanganyika. Kigoma ilikuwa inatawala kama inavyotawaliwa tofauti sasa hivi Burundi kama inavyotawaliwa sasa tofauti Rwanda. Kwa muda mrefu sana Mkoa wa Kigoma umeachwa nyuma katika kila kitu eneo la maendeleo.
Mimi nimeona lami ya kwanza ya highway mwaka 2008. Miaka zaidi ya 40 baada ya uhuru. Leo hii watu wa Kigoma wa maeneo ya Kusini mwa Kigoma wa maeneo ya Kaskazini mwa Kigoma wanasombwa kwenye maboti, wanasomwa kwenye magari wakiambiwa kwamba siyo raia wa Tanzania. Hatuwaoni Wamakonde wakiambiwa kwamba siyo raia wa Tanzania na wanapakana na Msumbiji. Hatuwaoni Wamasai wanaambiwa siyo raia wa Tanzania na wanapakana na Kenya. Hatuwaoni Wachaga wanaambiwa siyo raia wa Tanzania wanapakana na Kenya. Hatuwaoni Wanyakyusa wanaambiwa siyo raia wa Tanzania wanapakana na Zambia na vile vile wanapakana na Malawi.
Kwa nini suala hili liwe ni kwa watu wa Kigoma na watu wa Katavi peke yake? Kwa nini tunatumia fedha za nchi, polisi wa nchi kwenda kusumbua watu wa Kigoma. Nilikuwa naomba Mheshimiwa Waziri Mkuu operesheni inaendelea sasa hivi katika Mkoa wa Kigoma kuwanyanyasa Raia wa Kigoma waonekane ni Raia wa Tanzania wa daraja B ikome mara moja na viongozi wa Kisiasa, Wabunge wote  wa Mkoa wa Kigoma na Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa tukae tuweze kuangalia kwa sababu kuna uonevu wa hali ya juu sana katika operesheni ambayo inaendelea hivi sasa.
Mheshimiwa Spika, nilikuwa naomba niyaseme hayo vizuri na ninarejea kwamba tumefundishwa na wazee wetu kwamba sisi kati ya mwaka 1918 na mwaka 1924 hatukuwa sehemu ya Tanganyika iliyokuwa inatawaliwa na Mwingereza. Ninaomba nirejee sisi ni watu wa Kigoma kwanza kabla hatujawa wa Tanganyika, kabla hatujawa Watanzania. Ninaomba nilisisitize hili na watu wa Kigoma wananisikia kwa sababu tumenyanyaswa sana. Ninaomba masuala ya uraia yaangaliwe kwa karibu sana. Huu ni ujumbe ambao nimepewa na watu wa Kigoma nimeombwa niueleze na naomba Ofisi ya Waziri Mkuu, Mkuu wa Kigoma yupo hapa, Wakuu wa Wilaya, Kamanda Mkuu wa Mkoa wa Polisi wa Mkoa wa Kigoma na IGP waweze kuliangalia jambo hili kuweza kuhakikisha kwamba tunawalinda raia wa Kigoma.
Wenye Mabilioni Uswisi(Switzerland)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, Mheshimiwa Waziri Mkuu kumekuwa na taarifa ambazo zimeandikwa katika vyombo vya habari toka wiki iliyopita. Lilianza Gazeti la The East African baadaye wakaja Gazeti la The Citizen na leo nimesikia kwamba Gazeti la Mwananchi limezungumza kwamba kuna Watanzania 6 wana fedha katika akaunti kule Uswisi zaidi ya shilingi bilioni 303. India walipopata taarifa hizi kutoka Benki ya Uswisi waliwataja majina watu wote wana siasa na wafanyabiashara wenye fedha nje na fedh zile zikachunguzwa zile ambazo zimepatikana kwa haramu zikarejeshwa India. Nilikuwa naomba Mheshimiwa Waziri Mkuu uagize TAKUKURU na vyombo vyote vya Ulinzi na Usalama kwanza tutambue ni Watanzania gani hawa na fedha hizi zimepatikana kwa njia zipi na zile ambazo zimepatikana kwa njia ya wizi na ufisadi zirejeshwe nchini mara moja. Kwa sababu hatujaanza kunyonya utajiri huu wa gesi tayari kuna watu ambao wameshaanza kutajirika nao.
Tutakapoanza kunyonya hali itakuwaje? Kwa hiyo, nilikuwa naomba suala hili Serikali ilichukulie kwa uzito mkubwa ili itume salaam kwa mtu yeyote ambaye anatarajia kwamba atafaidika na utajiri wa rasilimali ya nchi kama gesi na madini na kadhalika ajue kwamba kokote atakapoficha fedha zake tutazifuata na zitarudi katika nchi hii. Nilikuwa naomba Waziri Mkuu aweze kuliangalia jambo hili kwa ukaribu sana.
Zuia Makampuni ya Kigeni kwenye Ulinzi
Mheshimiwa Mwenyekiti, la tatu hivi sasa Kiongozi wa Upinzania amezungumza jana kuna meli ziko Pwani ya Mkoa wa Pwani, Lindi na Mtwara zinatafuta mafuta. Mheshimiwa Waziri Mkuu hakuna kampuni hata moja ya mafuta inayonunua hata mchicha kutoka Tanzania. Meli zote ambazo ziko Bandari Mtwara zinakwenda kupeleka huduma kwenye maeneo ambayo yanatafuta mafuta yanapata mchele, nyanya, vitunguu, mchicha, mafuta ya kula na kadhalika kutokea Kenya kwa sababu hatujaweka utaratibu wa kufanya nchi yetu iweze kufaidika na utaraji huu mwanzoni. Kwa sababu hatua hizi za mwanzoni hakuna kodi ambayo tunapata kwa sababu mafuta bado yanatafutwa.
Hatua hizi za mwanzoni tunatakiwa tufaidike na fedha inayokuja, watu waweze kutumia fedha za kutoka ndani. Lakini hali ilivyo hivi sasa ni kwamba makampuni ya mafuta yanatumia zaidi ya dola milioni 161 kwa ajili ya shughuli za ulinzi na makampuni yanayolinda, ni makampuni ya nje. Yanabeba silaha kubwa kubwa, siku yakiamua kutugeuka na Navy yetu ilivyo tutapata shida. Nilikuwa naomba tutenge resources za kutosha na hata kama hatujaziweka kwenye bajeti sasa hivi, tuangalie, tuimarishe Navy na tupige marufuku, tuandike sheria kabisa kwamba itakuwa ni marufuku kwa raia yeyote wa kigeni kubeba silaha zozote kubwa ili kuweza kuhakikisha kwamba ulinzi ama unafanywa na watu wa ndani au unafanywa na Navy yetu tuweze kulinda mipaka yetu vizuri.
Utafutaji Mafuta Zanzibar Uendelee
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili kuna suala ambalo halijaisha na Kiongozi wa Upinzani Bungeni jana amelizungumzia la mafuta na gesi katika masuala ya muungano. Nilikuwa naomba jambo hili tulimalize kwa haraka. tulimalize kwa haraka na mimi sioni ubaya kwa kweli, sioni ubaya hata kidogo kama tukiamua kwamba shughuli zote commercial not upstream, sio masuala ya regulation, sio masuala ya vibali, sio masuala ya kutoa leseni, masuala yote commercial yanayohusiana na mafuta na gesi, kila upande wa muungano ushughulike na masuala yake.
Hakuna sababu ya kunga’gania jambo hili kama sisi tuna dhahabu, tuna tanzanite, tuna madini hayapo sehemu ya muungano, kwa nini mafuta na gesi yawe sehemu ya muungano? Hili ni jambo ambalo tulimalize, liishe tuimalize hii kero, vikao na vikao havitasaidia, tuimalize hii kero, tu-move forward watu wa Zanzibar waanze utaratibu wao wa kufanya utafutaji wao, waangalie kama watayapata hayo mafuta au hawatayapata, sisi tayari huku Bara tumeshapata, tuna matrilioni ya gesi, basin a wenyewe tuwaache waendelee na utaratibu wao. Hakuna sababu ya kuchelewesha jambo hili tuweze kulimaliza mapema.
TZS 40 Bilioni kwa Kiwira
Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho ni suala la Kiwira na baadae nitakuwa na mazungumzo na baadhi ya Mawaziri kuhusiana na suala hili tuliangalie kwa makini. Tumetenga shilingi bilioni 40 kwenye fedha ya maendeleo Wizara ya Nishati na Madini kwa ajili ya nini? Kuna fedha ambayo tunaenda kuwalipa watu ambao wameuharibu mgodi. Kwa nini tulipe watu ambao wameuharibu mgodi?
Lakini tunaenda kulipa bilioni 40 sio kwa Kiwira nzima..

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Saturday, June 23, 2012

LEARNING TO LIVE WITH POSITIVE THINKING – KATTIKIRO


Why there are so many variations in the way people thinking? Why similar circumstances do brings about different reactions?  To a greater extent, this is due to the fact that different persons perceive and process information in very different ways. John gets upset when it rains: ‘Rain makes me nervous; umbrellas are nuisance, traffic slows down, people slip and hurt themselves....’ he said. On the other hand Jane assesses the fact differently: “I like the smell of wet soil, rain cleans the air, birds are happier and plants and flowers grow”. Their respectively attitudes touch their work, family friends and everyday events. As a result, John experiences the bitter side of things while Jane enjoys the sweetness of life. 

Healthy and optimistic thinking:

      Causes of good mood:
·         Helps maintain optimal social interactions
·         Increases school achievement and work performance
·         Blocks anxiety
·         Enhances self-esteem
·         Reduces pain and other somatic symptoms
·         Strengthens the immune system
·         Helps patients recover from illness and from surgical treatments.

HOW TO THINK POSITIVELY
To reject negative thoughts and substitute them with alternative positive options constitutes a good way to obtain a positive thinking style.
Pessimistic thoughts tend to take over the person automatically and without following any logical pattern. It is therefore important to learn to identify such thoughts and to change the thinking style. Positive thinking must be an on going, permanent style of mental activity. It should also extend to all (or most all) life aspects.

The following areas need considerations:- 

·         Positive thinking about one self:
Try and avoid building your self-concept by comparing your self with TV stars and individuals from public life. They all portray unreal images. Accept your limitations and do something to improve these.  Above all, do not forget to underline your values and abilities. Stop and reject self-deprecating thoughts.

·         Positive thinking about the post:
The past can not be changed. Accept it even though it may contains unpleasant events. But do not blame the past for your present difficulties. That is useless. Never get obsessed with the disagreeable past. And as far as past positive events and anecdotes, remember them and enjoy them. Your attitude will improve and turn more positive.

·         Positive thinking about the future:
The future can be changed. Your attitude today affects tomorrow’s events. When you think with confidence and hope about tomorrow, you are increasing the probability of a much more successful future. And if something negative approaches, make plans now to prevent it instead of becoming anxious.

·         Positive thinking about people and the environment:
Put your “rose-coloured glasses” and look around. Not everything is perfect, but there are beautiful things and pleasant experiences. Do not grow suspicious of other people. Trust them and respect them and make efforts to feel affection towards them. Try to understand problem of others. Help them and you will see how your attitude becomes sweeter.
Many are dominated by irrational beliefs – ideals without logical sense that are able to cause unhappiness and even disorders. For example:
o   We are permanently surrounded by dangers and risks; it is natural to always feel worried and fearful.
o   Unhappy and unfortunate people can do nothing to improve their situation.
o   In order for me to be happy and to live in peace with myself, I must be loved and receive approval from everyone who knows me.’
o   There is always a perfect solution to every problem and if that solution is not realized, disastrous consequences follow.’ 

The above statements are fallacies and those living by them may experience psychological pain and even unhappiness. Make every effort to identify and analyses your favorite irrational beliefs. Reason logically I order to reject these thoughts and accept better alternatives. 

HOPE AS A FACTORS IN GOOD THINKING
Filling our mind with spiritual thoughts and themes   can be a safe way to attain mental peace. A peaceful conscience and a serene mind bring about an optimal mood. Meditation  in the sacred messages contained  in the Bible produces  mental peace  (read  the quotes  included  in the  following  tables  several  times). Try praying to God and tell him of your painful experiences. Trust in God. He will take care of you.

MIND CONTROL
People carry a general tendency to either positive or negative thinking. This tendency depends, to a great extent, on the continuous and automatic inner dialogue style that takes place within the person. In order to eliminate adverse thinking habits and search for positive alternatives to help solve situations, it is absolutely necessary to know the types of dialogue within ourselves.
Consider the following thoughts and their alternative options. Then think of your own typical mental reactions and write them down together with a good thinking alternative: 

Negative self-dialogue
Alternative
‘All this is horrible’
‘It is not that bad. It could be worse’
‘This is useless’
‘There must be something good.....’
‘This man is a pain’
‘I can learn something from this man’
‘My cold will end up in pneumonia’
‘I’ll soon recover from my cold’







"Dear Blog viewers; thank you very much for following me on my blog, please leave me with some comments about my posts below this post, as well as contribute and ask questions as to make me improve the contents of my blog as to benefit you all. I guarantee to reply to your comments and contribution as soon as I read it". 

Friday, June 22, 2012

Lengo la Kuomba Mwongozo - Sakata la Madaktari

Kwanini niliomba muongozo-Sakata la Mgomo wa Madaktari

Leo nilitaka kuomba muongozo wa Spika kwa mujibu wa Kanuni 49 (2) baada ya Waziri wa Afya kutoa kauli juu ya utekelezaji wa madai ya madaktari. Kanuni hiyo inataka kauli isiwe ya kuzua mjadala lakini aliyoyaeleza waziri juu ya uboreshaji wa maslahi ya madaktari yanazua mjadala kwa kuwa yanatofautiana na majibu ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda aliyoyatoa bungeni jana, (Juni 21, 2012) na pia hayana uhalisi. Mathalani, wakati serikali ikidai imeongeza posho ya kuitwa kazini (on call allowance) toka Februari, 2012 na kutumia bilioni 7.9 kwa miezi michache, imetenga kwa watumishi wa Afya bilioni 18.9 tu kwa mwaka mzima wa 2012/2013 kiwango ambacho hakitoshi.


Hivyo nilitaka kuomba muongozo Spika awezeshe kauli hiyo ijadiliwe kama ilivyokuwa kwa kauli juu ya fedha za rada. Nakusudia kumuandikia barua Spika kushauri aelekeze kamati ya bunge ya huduma za jamii kauli hiyo ya waziri.


Pia bunge halipaswi kunyimwa fursa ya kutumia mamlaka yake kwa mujibu wa ibara ya 63 ya kuishauri na kuisimamia serikali kusuluhisha mgogoro na madaktari ili kuepusha mgomo wenye athari kwa nchi na wananchi kwa kisingizio cha kusudio la serikali kupeleka mgogoro mahakama kuu kwa kuwa mpaka leo taarifa iliyotolewa bungeni bado hakuna shauri katika kitengo cha kazi. Hivyo, Spika anapaswa kutoa jukumu kwa kamati husika ya bunge kuendelea na usuluhishi kabla ya serikali kukimbilia mahakamani.


Wabunge tupewe nakala ya taarifa ya majadiliano ya pande mbili yaliyochukua zaidi ya siku 90 badala ya kupewa hotuba ya nusu saa ya upande mmoja wa serikali pekee.


Hata serikali ikizuia mgomo wa wazi kwa zuio la kimahakama ieleweke kuwa mgomo wa chinichini kwa watumishi wa afya ambao una athari ya muda mrefu kwa maisha ya wananchi nchini.


Mwisho, serikali ipunguze matumizi yasiyo ya lazima na ipanue wigo wa mapato.


John John Mnyika.

Mbunge Jimbo la Ubungo (CHADEMA)
22 Juni, 2012

UPINZANI KUKATAA BAJETI

Gazeti la Majira la tarehe 21 Juni 2012 limebeba kichwa cha habari “Siri ya kukataa bajeti yafichuka: Yadaiwa hilo ni shinikizo la nchi za magharibi; lengo ni kupora gesi, mafuta na madini ya urani”: Nilipotolewa bungeni tarehe 19 Juni 2012 nilieleza kwamba nitatoa tamko la kina ya sababu za kutoa kauli bungeni kuwa “tumefika hapa kwa sababu ya udhaifu wa Rais Kikwete, uzembe wa Bunge na upuuzi wa CCM”; nimeacha mpaka sasa kutoa tamko kuwapa nafasi Rais Kikwete, Wabunge na CCM watafakari mchango niliotoa bungeni na kuchukua hatua zinazostahili za kuondoa bajeti na kuwezesha marekebisho ya msingi.


Wakati nikisubiri hatua hizo amenukuliwa tarehe 21 Juni 2012 Mbunge wa Iramba Magharibi Mwigulu Nchemba ambaye pia ni Katibu wa Fedha na Uchumi wa CCM akitoa madai ya uongo ambayo yanaendelea kudhihirisha kile nilichokieleza bungeni; hivyo katika muktadha huo iwapo Rais Kikwete na Bunge halitarekebisha udhaifu uliojitokeza nitaendelea kuungana na wabunge wengine wa upinzani kukataa bajeti na kuchukua hatua zaidi na kutoa tamko la kina siku chache zijazo.


Kwa sasa nieleze tu kuwa Nchemba anapaswa kuyataja kwa majina hayo mataifa ya magharibi na kuwataja kwa majina wabunge na wanasiasa anaodai wamewezeshwa kifedha ili kukataa bajeti kuwezesha kuporwa kwa gesi, mafuta na madini ya urani. Aidha, Waziri wa Mambo ya Nje, Benard Membe anapaswa kutoa kauli kwa umma iwapo maneno hayo ya uzushi ndio msimamo wa Serikali ya Tanzania inayoongozwa na CCM.


Wananchi ambao wametutuma wabunge kuikataa bajeti wanajua kwamba bajeti hii inakataliwa kwa kutokuweka misingi ya kutimiza ahadi ya Rais Kikwete na CCM ya maisha bora kwa kila mtanzania na badala yake kuongeza ugumu wa maisha kutokana na kushindwa kukabiliana na matatizo ya mfumuko wa bei.


Aidha, wabunge tumekubaliana na maoni ya kambi ya upinzani ya kuikataa bajeti kwa kuwa imeshindwa kuzingatia Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa Miaka Mitano ambao ulipitishwa kwa azimio la bunge ambao ulipaswa kuiongoza serikali kuweka mkazo katika kuendeleza nchi kwa kutumia fedha za ndani. Nikinukuu ukurasa wa 92 kifungu cha 4.3.1 “Kwa kuelewa kuwa wakati wote kutakuwa na miradi ya uwekezaji nje ya mpango, serikali kuanzia sasa itakuwa inatenga asilimia 35 ya makadirio ya mapato yake ya ndani kwa ajili ya kugharamia bajeti ya maendeleo kila mwaka”. Wabunge tunayakataa makadirio ya bajeti ya serikali kwa mwaka wa fedha 2012/2013 kwa sababu Serikali imetenga asilimia sifuri ya mapato ya ndani kwa ajili ya kugharamia bajeti ya maendeleo.


Ndio maana katika mchango wangu bungeni tarehe 19 Juni 2012 kabla ya kutolewa bungeni nilieleza kwamba nakataa bajeti kwa kuwa bajeti haikuweka vipaumbele vya msingi vya maendeleo ya wananchi na nikataja mifano ya masuala ambayo wananchi wa Ubungo walionituma kuwawakilisha ya kutaka fedha za kutosha kutengwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo ya maji na barabara za pembezoni za kupunguza msongamano wa magari katika Jiji la Dar es salaam. Katika mchango huo ambao unaweza kurejewa katika taarifa rasmi za bunge (Hansard) nilieleza namna ambavyo bajeti iliyowasilishwa haitekelezi ilani ya CCM kwa ukamilifu wala kutenga viwango vya fedha kama ilivyotakiwa na mpango wa taifa wa miaka mitano.


Miradi hiyo ya Ubungo na Dar es salaam kwa ujumla ya maji na barabara ilipitishwa na baraza la mawaziri ili kutengewa fedha Mwenyekiti akiwa Rais Kikwete na ilitokana na ahadi za Rais Kikwete lakini haijatengewa fedha za kutosha huku bajeti ikiwa na matumizi mengi ya kawaida yasiyokuwa ya lazima ambayo yangeweza kupunguzwa na kuelekezwa kwenye miradi ya maendeleo. Badala ya Nchemba kufanya propaganda chafu alipaswa kumshauri Rais Kikwete na CCM kutekeleza ahadi na kutimiza wajibu ipasavyo kwa kuiondoa bajeti na kuirejesha baada ya kuifanyia marekebisho ya msingi ili isikataliwe.


Nchemba anapaswa kufahamu kwamba wabunge wa upinzani kabla na hata katika bunge la kumi tumekuwa tukiungana pamoja kupinga ufisadi na kutetea rasilimali za taifa ambazo Serikali ya CCM kwa muda mrefu imeachia zimeporwa na mataifa na makampuni ya kigeni kwa madai ya uwekezaji kutoka nje. Nchemba ni vyema tu akarejea uchambuzi wa wasemaji wa kambi rasmi ya upinzani kuhusu udhaifu wa kisera na kisheria pamoja na mikataba mibovu ambayo inalikosesha taifa mapato kwenye gesi, mafuta na madini ambao umetolewa kwa nyakati mbalimbali.


Hivyo, Serikali isipotoa kauli ya kukubaliana na maoni ya kambi rasmi ya upinzani tuliyoyatoa tarehe 15 Julai 2011 wakati wa bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2011/2012 na Hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani kuhusu mapendekezo ya makadirio ya mapato na matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2012/2013; katika masuala ya gesi, mafuta na madini kwa nafasi yangu ya uwaziri kivuli wa Nishati na Madini nitatumia njia za kibunge katika mkutano huu wa nane wa bunge unaoendelea kusimamia uwajibikaji kwa maslahi ya umma. Nchemba anapaswa kufahamu kwamba kutokana na udhaifu uliopo hivi sasa, Tanzania haina sheria ya gesi asili huku uvunaji wa rasilimali hiyo ukiendelea kiholela na ufisadi uliobainika na kuanikwa hata bungeni mpaka sasa haujashughulikiwa.


Madai ya Nchemba kuwa wabunge wameshiriki kuandaa bajeti katika hatua ya kamati hivyo hawana uhalali wa kuipinga bungeni hayana ukweli wowote kwa kuwa kwenye kamati wabunge hujadili bajeti za Wizara za kamati husika; bajeti kuu hupelekwa baadaye kwa mujibu wa kanuni ya 96 ya Kanuni za Kudumu za Bunge ambayo hata yenyewe kwa mwaka huu haikutekelezwa ipasavyo.


Aidha, ifahamike kwamba wabunge tulikoseshwa fursa ya kutumia ipasavyo mamlaka ya kibunge ya Ibara ya 63 ya katiba ya kuishauri na kuisimamia serikali katika kupanga mipango ya maendeleo kutokana na kanuni ya 94 ya bunge kutokuzingatiwa ambayo ilitaka bunge likae kama kamati ya mipango katika mkutano wa Bunge wa Mwezi Februari kutoa mapendekezo ya vipaumbele na hivyo kufanya mpango huo kujadiliwa hivi sasa wakati mapendekezo ya bajeti yameshaandaliwa bila kuzingatia mpango wa taifa wa miaka mitano.
Wakati nilipohoji kuhusu suala hilo miezi ya Februrari, Machi na Aprili Nchemba hakuwahi kuunga mkono wala kuishauri CCM na serikali kuzingatia hatua muhimu za upangaji wa bajeti ambazo zingeepusha bajeti kukataliwa katika hatua ya mwisho kwa kutokidhi matakwa ya umma.


Kauli ya Nchemba ya kwamba wabunge wa upinzani tunataka kuikwamisha bajeti ili bunge livunjwe twende kwenye uchaguzi imedhihirisha tahadhari niliyoitoa ya kwamba wananchi wasitarajie wabunge wa CCM kuikataa bajeti kwa kuwa ubovu wa katiba ibara ya 90 umetoa mamlaka makubwa kwa Rais ya kulivunja bunge, na kwamba wabunge wengi wa CCM wana hofu juu ya uchaguzi kurudiwa hivyo wataipitisha bajeti kwa kura ya NDIYO hata kama inaongoza ugumu wa maisha kwa wananchi na haiwezeshi utekelezaji wa haraka wa miradi ya maendeleo. Hivyo, suluhisho katika hali hiyo kabla ya mabadiliko ya katiba ni Rais kuondoa udhaifu na kutumia nguvu kubwa aliyonayo kwa mujibu wa katiba kuiondoa bajeti na kuirejesha ikiwa imefanyiwa marekebisho makubwa kwa kuzingatia michango ya wabunge na maoni ya kambi rasmi ya upinzani bungeni.


John Mnyika
Mbunge wa Jimbo la Ubungo
Bungeni-Dodoma (21/06/2012)

SHAHADA YA UFISADI NA UCHAKACHUAJI


Ndugu watanzania wenzangu, je ni kweli kuwa hawa viongozi wetu, walihitimu shahada hiyo kama ionekanavyo hapo pichani? 

Tafadhali toa maoni yako!!

MGOMO UPO PALE PALE - MADAKTARI

LICHA ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kuwataka madaktari nchini kurejea katika meza ya mazungumzo, kwa maelezo kuwa baadhi ya madai yao yameshughulikiwa, wataalamu hao wamemjibu wakisisitiza kwamba mgomo wao upo pale pale kuanzia kesho. 

Madaktari hao wamesema kuwa Waziri Mkuu, amelidanganya Bunge jana wakati akijibu maswali ya papo kwa hapo, kwa kuesema kuwa kati ya madai yao kumi waliyowasilisha, matano yameafikiwa na kila upande.
 Kwa mujibu wa madaktari, wiki mbili za mgogoro na serikali walizozitoa zinamalizika leo, hivyo kuanzia kesho kada zote wanaingia katika mgomo usiokuwa na kikomo. Majibu ya madaktari hao, yalitoka na kauli ya Pinda bungeni jana wakati akijibu swali la Kiongozi wa Kambi ya Upinzani, Freeman Mbowe (CHADEMA), aliyetaka kujua malumbano kati ya serikali, madaktari na walimu yatatatuliwa lini ili kuepusha mgomo.

Katika hilo, Pinda, alilieleza Bunge kuwa tangu awali serikali iliunda kamati maalumu ya kushughulikia suala hilo ambapo miongoni mwa madai yao kumi, matano yameafikiwa na kila upande. “Ninajua uzito wa hili jambo na lilipotokea tulijitahidi kuhakikisha tunaunda kamati maalumu ili kuweza kushughulikia masuala haya, na kwa mujibu wa kamati ni mambo matano kati ya kumi, tumeafikiana kwa pamoja,” alisema na kuongeza kuwa: “Baada ya hatua zote hizo kwa mujibu wa sheria ni lazima makubaliano yao yasajiliwe na Tume ya Usuluhishi (CMA), na kwamba hilo limefanyika ambapo tume ya serikali  na upande wa madaktari wamemaliza kazi yake.

“Hata hivyo mambo matano yaliyobaki, nilimuagiza tena Waziri wa Afya awaandikie barua madaktari ili waweze kukutana, lakini hadi juzi wanajibu barua ile wanasema hawazezi kukutana tena na serikali kwa sababu haijatelekeza madai yao,” alisema Pinda.
Kwamba kati ya madai waliyotaka na serikali imeyatekeleza ni pamoja na kuondolewa kwa mawaziri wa wizara hiyo, kuongezwa posho ya kuitwa kazini, kufanya uchunguzi wa maiti na nyinginezo.

“Lakini pamoja na hali hii serikali ilifungua kesi ikilalamikia mgomo wa madaktari  uliotokea mwanzoni mwa mwaka huu, tume ya usuluhishi ilizitaka pande mbili, kamati ya serikali na wawakilishi wa madaktari kukaa meza moja na kuzungumza Juni 19, mwaka huu,” alisema.
Alifafanua kuwa mambo matano waliyoafikiana ni serikali kukubali kuongeza posho ya kuitwa kazini kutoka sh 10,000 hadi sh 15,000 kwa madaktari walio kwenye mafunzo kazini na sh 20,000 kwa madaktari na sh 25,000 kwa madaktari bingwa.

“Pia serikali iliongeza posho ya uchunguzi wa maiti kutoka sh 10,000 hadi 100,000 kwa madaktari na sh 50,000 kwa wasaidizi,” alisema Waziri Mkuu Pinda.
Aliongeza kuwa serikali ilikubali kuwapa kadi ya Bima ya Afya ya rangi ya kijani ambayo ina hadhi ya huduma za daraja la kwanza kwa madaktari, pia kutoa chanjo ya ugonjwa wa ini ambapo fedha za chanjo hiyo zimo kwenye bajeti ya mwaka ujao wa fedha 2012/2013.

Hata hivyo, maelezo yake ylipingwa na Chama cha Madaktari (MAT), ambapo kwa niaba yao, Mwenyekiti wa Jumuiya ya wanataaluma hao, Dk. Steven Ulimboka, alisema kuwa hawako tayari kupeleka suala hilo katika Mahakama ya Kazi kama alivyoeleza waziri mkuu.
Alisema ni jambo la aibu kwa viongozi wakuu wa serikali kuamua kwa makusudi kulidanganya Bunge wakati wakijua wazi hakuna utekelezaji wa aina yoyote uliofanywa.
Mwenyekiti huyo alisema kuwa katika madai yote ya madaktari hakuna dai hata moja ambalo limetekelezwa kama inavyoelezwa na viongozi.

Alisema kitu cha kushangaza hata taarifa ya ufafanuzi wa madai yao hakuna eneo ambalo serikali imeweka saini. “Mgomo huu ni wa madaktari wa ngazi zote nchini ambao hauna kikomo na tunachohitaji ni kuelezwa na serikali hatua waliyofanya kuliko wanavyoendesha propaganda na kuweka siasa katika madai yetu,” alisema.

Alisema pamoja na madai yaliyotolewa na madaktari lakini kitu cha ajabu kilichofanywa na serikali ni kuamua kuchomeka dai la posho ya uchunguzi wa maiti ambalo halijawahi kutolewa na madaktari. “Serikali inataka kutafuta ionekane imetenda mema kwa madaktari kwa kudai kupandisha kima cha posho ya uchunguzi wa maiti kutoka sh 10,000 hadi sh 100,000 wakati sisi hatujawahi kuomba posho hiyo,” alisema.
Alisema posho hiyo si muhimu kwa madaktari kwa kuwa wapo baadhi ya madaktari wanaoweza kufanya kazi kwa zaidi ya miaka 30 bila kufanya uchunguzi huo.
Dk. Ulimboka alisema kuwa Watanzania hawapaswi kuwalaumu madaktari kwa kuwa anayepaswa kubebeshwa lawama hizo ni serikali iliyoshindwa kuboresha afya pamoja na kutatua migogoro.

Alisema walitegemea kwa siku 90 walizokaa katika meza ya majadiliano na kamati iliyoundwa na serikali wangepata ufumbuzi wa madai yao, matokeo yake imekuwa ni matatizo zaidi. “Kuhusu huduma za dharura katika maeneo nyeti watakaa na kutafuta ufumbuzi hapo baadaye,” alisema.

MBOWE, LISSU, MDEE WAMZIMA NGEREJA

MAKEKE ya aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja (CCM), jana yalizimwa na wabunge watatu wa CHADEMA, Freeman Mbowe, Tundu Lissu na Halima Mdee, huku wakimtaka Spika wa Bunge amchukulie hatua kwa kupoteza muda.
Ngeleja aliyekuwa akichangia hotuba ya bajeti ya mwaka wa fedha 2012/2013 muda mfupi baada ya Mbowe, alitumia muda mwingi kuishambulia hotuba ya maoni ya bajeti ya Kambi ya Upinzani akidai ni mbovu na haitekelezeki.
Huku akishangiliwa na wabunge wenzake wa CCM, Ngeleja ambaye pia ni Mbunge wa Sengerema, alikwenda mbali zaidi akinuku hotuba hiyo iliyowasilishwa na Waziri kivuli wa Fedha, Zitto Kabwe, na kusema kuwa wana vyanzo vya ukusanyaji mapato ambavyo vinaonesha shilingi sifuri. Kama hiyo haitoshi, mbunge huyo aliitaka Kambi ya Upinzani kuwaomba radhi Watanzania akidai wamewapotosha kutokana na kuandaa bajeti iliyowahadaa wakati wameshindwa kuainisha uwiano wa vyanzo vya mapato na matumizi.
Hatua hiyo, ilimfanya mnadhimu mkuu wa kambi hiyo, Lissu kusimama na kuomba mwongozo wa Spika akisema kuwa kwa mujibu wa kanuni za Bunge, bajeti iliyoko mbele yao ambayo inapaswa kujadiliwa ni ile iliyowasilishwa na serikali.
“Sisi wapinzani tunawasilisha maoni yetu kuhusu bajeti ya serikali ili yafanyiwe kazi na si bajeti kivuli wala mbadala kama baadhi ya wabunge wanavyojaribu kupotosha,” alisema Lissu na kuungwa mkono na Spika.


Spika Anne Makinda alifafanua kuwa hakuna bajeti kivuli wala mbadala na badala yake kambi hiyo hutoa hoja ya kuhusu bajeti ya serikali inayokuwa imesomwa ikionesha kama wao wangekuwa madarakani wangeipanga hivyo.


Hata hivyo Ngeleja aliikataa taarifa hiyo na hivyo kuzidi kushikilia msimamo wake, jambo lililomlazimu Mbowe, kuomba mwongo wa Spika akiuliza kiti chake kinawachukulia hatua gani wabunge kama hao wanaopoteza muda kwa jambo lililokwisha kufafanuliwa.
Wakati Spika akijaribu kumaliza ubishi huo, Mbunge wa Kawe, Mdee, aliinuka na kuomba kumpa taarifa Ngeleja na kusema kuwa kipengele anachokisemea mbunge mwenzake kilishatolewa ufafanuzi kwamba kulikuwa na kasoro za uchapaji.
“Huyu ana uchungu wa kutemwa katika Baraza la Mawaziri,” alisema Mdee lakini kabla ya kuendelea Spika alimtaka afute maneno hayo kwanza. Mdee alidai kuwa hatua hiyo inaonesha ni jinsi gani Ngeleja haudhurii vikao, kwani asingepoteza muda kuhoji jambo ambalo walikwisha kulifanyia masahihisho.


Awali wakati wa mchango wake, Ngeleja alisema kuwa hali ya uchumi wa nchi yetu kwa sasa inachangiwa na upungufu wa chakula ambapo bei ya bidhaa hiyo imepaa na kuongeza makali ya maisha kwa wananchi. Ngeleja alisema pia tatizo la nishati limekuwa chanzo cha kuongeza makali ya maisha kwani bei ya nishati imekuwa ikipaa mara kwa mara.
Naye Mbowe katika mchango wake, mbali na kulalamikia deni la taifa na kuitaka serikali ifanye juhudi za makusudi kuwaondoa wananchi kwenye umaskini walionao sasa, pia alikemea lugha za matusi kwa baadhi ya wabunge, hivyo kumtaka spika na wasaidizi wake kutenda haki kwa pande zote.


Katika hali nyingine: 


Shellukindo awasifu wapinzani

Akichangia hotuba hiyo, Mbunge wa Kilindi, Beatrice Shellukindo, (CCM), alianza kwa kuipongeza kambi ya upinzani bungeni akisema kuwa inafanya kazi yake vizuri kwa kuishauri na kuikosoa serikali. Shellukindo aliwataka wabunge wenzake wa chama tawala kuweka mambo ya vyama pembeni na kuangalia masilahi ya taifa, kwani kazi ya wabunge wote bila kujali itikadi za vyama ni kuishauri serikali katika masuala ya kuwaletea maendeleo wananchi.


Alisema hakuna Bunge katika nchi yoyote ambalo ni la chama tawala wala cha upinzani, huku akiwapongeza wapinzani kuwa wanakitakia mema CCM kwa kuwakosoa ili warekebishe. Aidha, mbunge huyo alikosoa sera ya Kilimo Kwanza huku akibainisha kuwa haimlengi mkulima wa kawaida bali ni wakulima wakubwa. Mbunge wa Kigoma Mjini, Peter Selukamba (CCM), alisema mfumuko wa bei unachangiwa na ubovu wa miundombinu jambo ambalo husababisha mazao yanayotoka shambani ambako ni vijijini kufika mjini na kuwa katika bei ya juu kuliko yalivyozalishwa. Selukamba alibainisha kuwa mazao au bidhaa ikitoka kijijini inapofika mjini huuzwa kwa bei ya juu zaidi kutokana na gharama kubwa kutumika katika usafirishaji wake.


Filikunjombe aigomea bajeti

Mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe (CCM), naye amekuwa kama mwenzake wa Kisesa, Luhaga Mpina, kwa kugoma kuiunga mkono bajeti ya serikali akitaka maelezo ya serikali kuhusu fedha za miradi ya maendeleo zilizotengwa katika Wizara ya Uchukuzi.


“Katika bajeti iliyopita tulisema na serikali kupitia waziri mkuu, ikatangaza kuongeza sh bilioni 90 kwa Wizara ya Uchukuzi na kati ya hizo sh bilioni sita, zilipelekwa katika sekta ya meli Ziwa Nyasa na fedha zilizoletwa ni sh milioni 200 pekee,” alisema. “Nawaomba wabunge wenzangu tuwe wakweli, kwa hili  lazima tuihoji, na kwa serikali hii ya CCM ni yetu, kama hatutafanya hivyo tutakuwa hatuna maana ya kuwapo kwetu hapa bungeni,” alisema Filikunjombe.

MKONO AIBUA UFISADI KIWIRA

Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono, ameibua ufisadi unaodaiwa kufanywa katika mgodi wa Kiwira na kulitaka Bunge kuunda kamati maalumu ya uchunguzi.

Mkono alidai kuwa sehemu moja ya mgodi huo yenye utajiri mkubwa imeuzwa kwa bei ya kutupwa kwa kampuni moja ya Australia.

Alisema uuzaji huo ni kinyume cha makubaliano yaliyofikiwa na Bunge  mwaka 2007 ambapo liliagiza kuwa mgodi wa Kiwira uliokuwa umeuzwa kwa Kampuni ya Tan Power urudishwe serikalini baada ya kuwa umeuzwa kwa dola laki saba tu.

Hata hivyo, Mkono alisema kuwa katika hali ya kushangaza Kampuni ya Tan Power ambayo ilikuwa imeingia ubia na serikali iliuzwa kwa Waustralia  kiasi cha mabilioni ya dola. “Mheshimiwa Spika, Kiwira kulikoni? Lini Bunge litaunda kamati ya kwenda kuangalia Kiwira?” alihoji na kusema kuwa pamoja na yote hayo, sasa serikali imetenga sh bilioni 40 kwa ajili ya mradi wa Kiwira na kuhoji nani aliteketeza fedha za awali zilizotolewa kwa ajili hiyo.

Tuesday, June 19, 2012

Msimamo wa Mnyika wa sasa juu ya Kauli yake bungeni!


Nitatoa tamko la kina baadae kuhusu kilichotokea lakini kwa ufupi ubovu wa bajeti hii ni matokeo ya udhaifu wa Rais Kikwete, yeye ndiye aliyesaini Mpango wa Taifa wa miaka mitano kama Kiongozi Mkuu wa Nchi tena kwa wino mwekundu kama Amiri Jeshi Mkuu. Na yeye ndiye Mwenyekiti wa baraza la mawaziri, bajeti hii iliyoacha kuzingatia mpango wa Taifa imepita kwenye baraza aliloliongoza, pia kushindwa kutekelezwa kwa bajeti iliyopita ni matokeo pia ya udhaifu wa taasisi ya Urais.  

Pia kwa mujibu wa Katiba Rais ndiye ambaye anapeleka bajeti bungeni, Waziri mwenye dhamana anapeleka tu kwa niaba. Rais amepewa mamlaka makubwa juu ya bajeti ibara ya 99 imeweka mipaka kuhusu mambo ambayo bunge lina mamlaka nayo huku ibara ya 90 inasema bunge likikataa bajeti rais ana mamlaka ya kuvunja bunge. Hivyo Rais Kikwete anapaswa kuagiza Waziri wa Fedha bajeti iondolewe irudi kwenye baraza la mawaziri ikafanyiwe marekebisho!


John Mnyika
19 Juni 2012

MAELEZO YA BAJETI KIVULI

Mh. Zitto Kabwe akiwasili viwanja vya Bunge kuwasilisha bajeti ya Upinzani.
Mh. Zitto akiwasilisha hotuba ya bajeti kivuli. 
 
Katika mjadala unaoendelea Bungeni kuhusu Bajeti, baadhi ya wabunge wameeleza kwamba Bajeti Kivuli haikuonyesha vyanzo vya mapato na hivyo kuita ni vyanzo sifuri. Ukweli ni kwamba tumeweka vyanzo vya mapato ya ndani kwa ujumla bila kuainisha mapato ya kikodi ni ngapi, mapato yasiyo ya kikodi ni ngapi na mapato ya Halmashauri ni kiasi gani. Hivyo tunakiri kosa hili na tumechukua hatua ya kuainisha mapato hayo Kama inavyoonekana kwenye jedwali hili hapa chini.

  MAPATO
SHILINGI MILIONI
A Mapato ya ndani

11,889,078
  i)mapato ya kodi (TRA)
10,232,539

  ii)Mapato yasiyo ya kodi
1,163,533

B Mapato ya Halmashauri
493,006


Mapato haya yamo ndani ya Hotuba ya Bajeti Mbadala lakini kwa makosa ya kihariri hayakuonyeshwa kwenye jedwali na hivyo kuleta usumbufu kwa Wabunge na Watanzania wengine waliopata fursa ya kusoma Hotuba yetu. Tunaomba radhi kwa usumbufu. Nawashukuru walioona tatizo hili na hii inaonyesha kuwa wabunge wanasoma kwa makini Bajeti ya Upinzani.

Ninawatakia mjadala mwema wa Bajeti.

Kabwe Zuberi Zitto,Mb
Waziri wa Fedha na Uchumi Kivuli
19.06.2012


Monday, June 18, 2012

HOTUBA YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI BUNGENI NDUGU KABWE ZUBERI ZITTO (MB), WIZARA YA FEDHA NA UCHUMI, KUHUSU MAPENDEKEZO YA MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA SERIKALI KWA MWAKA WA FEDHA 2012/2013


I. UTANGULIZI

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Kambi ya Upinzani, ninatoa maoni ya Kambi ya Upinzani kuhusu Bajeti ya Nchi ya mwaka wa fedha2012/2013 kwa mujibu wa Kanuni za Bunge Kifungu cha 99(7) toleo la Mwaka 2007. 

Mheshimiwa Spika, Natoa pongezi za dhati kabisa kwa Ndugu William Augustao Mgimwa, Mbunge wa Jimbo la Kalenga mkoani Iringa kwa kuteuliwa na Rais kuwa Waziri wa Fedha na Uchumi.

Vile vile nawapongeza Ndugu Saada Mkuya na Ndugu Janeth Mbene kwa kuteuliwa kwao kuwa Wabunge na baadaye kuwa Manaibu Mawaziri  katika Wizara hii nyeti sana. Ninawapa pole pia maana Wizara ya Fedha sio Wizara lelemama. Kambi ya Upinzani itaendelea kuisimamia Wizara hii kwa ukaribu sana kama ilivyofanya katika kipindi cha miaka miwili iliyopita. Mtakapofanya vizuri tutawapongeza ili muongeze juhudi, mtakapoharibu tutawawajibisha.

Mheshimiwa Spika, Ni dhahiri kwamba Mwaka wa Fedha uliopita ulikuwa mwaka mgumu sana kwa Watanzania. Ni mwaka ambao gharama za maisha zilipanda kwa kasi kubwa sana na juhudi za Serikali kuwakwamua wananchi na hasa wananchi wanyonge kutoka kwenye lindi la ufukara ziligonga mwamba. Kambi ya Upinzani inawapa pole Watanzania kwani hili ndilo walilochagua.

Saturday, June 16, 2012

PRESIDENT JAKAYA MRISHO KIKWETE OPENS THE 4TH FORUM OF THE GLOBAL NETWORK OF THE RELIGIONS FOR CHILDREN (GNRC)

President Dr Jakaya Mrisho Kikwete opening the 4th Global Network of Religions for Children (GNRC), at the Serena Inn  in Dar es salaam today June 16, 2012. 

President Dr Jakaya Mrisho Kikwete and the President of the Arigatou International Global Network of Religions for Children (GNRC), pose with some of children participants from different countries and religious constintuences after opening the 4th GNRC forum  at the Serena Inn  in Dar es salaam today June 16, 2012.

The GNRC's fourth quadrennial forum will emphasize interfaith solutions to poverty's impact on children. The global gathering has brought  together some 250 religious leaders, child-rights workers, and civil society representatives from around the world.

NWONGOZO WA BAJETI SEHEMU YA MWISHO.


Changamoto
Zipo changamoto nyingi unazoweza kukutana nazo pale unapoamua kushiriki kikamilifu katika mchakato wa bajeti. Baadhi ya changamoto hizi ni kama zilivyoainishwa katika sehemu inayofuata.

Changamoto

Ukosefu wa takwimu sahihi ambazo imekuwa ngumu kuzipata: Hii inamaanisha kwamba serikali za mitaa zimekuwa hazina uhakika kuhusu kiwango cha fedha zinazotakiwa kupokelewa katika halmashauri. Hali hii imekuwa kikwazo katika upangaji wa mipango endelevu.

Upotevu wa vipaumbele: Hii hutokea kwa sababu bajeti hujadiliwa na ofisi nyingi na katika ngazi tofauti tofauti na hivyo kusababisha baadhi ya mipango iliyopangwa hapo awali kusahaulika. Fedha zinazotolewa na serikali kuu zinaweza kuelekezwa mradi ambao wananchi hawakuuchagua.

Fursa na changamoto za maendeleo pamoja na makundi ya pembezoni pia yanaweza kusahaulika.

Kuchelewa kwa mpango wa maendeleo katika halmashauri huchelewesha pia miongozo ya bajeti katika kata na vijiji.

Serikali kuu kuchelewa kutuma fedha katika halmashauri: Hali hii husababisha miradi ya maendeleo kuchelewa kuanza na vilevile kuchelewa kumalizika kwake.

Ni muhimu utambue changamoto hizi kabla ya kuchukua hatua yoyote. Kumbuka kuwa ushiriki wa raia na uhitaji wa uwajibikaji ni mambo muhimu katika kuleta mabadiliko yoyote. Una haki ya kupata taarifa na kujibiwa maswali yako.

Mahali tunapoweza kupata Taarifa zaidi.
Halmashauri zinawajibika kisheria kubandika taarifa kuhusu bajeti kwenye mbao za matangazo zilizopo katika halmashauri husika. Pia taarifa kuhusu bajeti hutangazwa kupitia vyombo vya habari. Vyombo hivyo hutoa taarifa muhimu kuhusu bajeti. Kwa mfano hutangaza kuhusu kiasi cha fedha kilichopokelewa na halmashauri kutoka serikali kuu. Afisa mipango wa wilaya na wajumbe wa halmashauri, Kata pamoja na maofisa watendaji wa vijiji wana wajibu wa kukupatia taarifa kuhusu mipango ya bajeti, maendeleo yake pamoja na taarifa zingine muhimu. Kwa bahati mbaya baadhi ya maofisa wa serikali hawatoi ushirikiano mzuri hasa linapokuja suala la kutoa taarifa muhimu kuhusu bajeti.

Kumbuka
Kama hutashiriki kuna madhara yake vilevile. Kitendo cha wewe kutoshiriki kitasababisha serikali itelekeze mipango yake ya maendeleo bila kuangalia mahitaji yako. Ushiriki hukufanya ujisikie kwamba miradi ya maendeleo ni mali yako na inaendelezwa kulingana na vipaumbele ulivyojiwekea.

o   Kupata huduma za jamii ni haki yako na wala si hisani.
o   Hata pale ambapo rasilimili zitakuwa hazitoshi ni lazima zigawiwe kwa usawa kwa kuzingatia haki.
o   Dola ina wajibu wa kutumia rasilimali zake kuhakikisha kuwa raia wanatambua haki zao pamoja na uwezo wao.
o   Wale wanaodhibiti fedha za umma pamoja na wale wanaohusika katika kutoa huduma, wanawajibika katika kutoa maelezo ni kwa nini wameshindwa kuwatumikia wananchi kwa ufanisi.
o   Pale rasilimali za umma zinapotumiwa vibaya au kuharibiwa, vyombo vya udhibiti kama vile Bunge pamoja na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali vinapaswa kuchukua hatua.
o   Raia wana haki kuhakikisha kuwa fedha za umma zinatumiwa kama zilivyopangwa. Kama kutakuwa na matumizi mabaya ya fedha za umma, watumishi wanapaswa kuhojiwa.
o   Maendeleo huanzia pale unapokuwa na shauku ya kujua wapi kodi yako inapelekwa.
o   Ushiriki na matendo huleta mabadiliko.

Wadau mbalimbali wanaweza
o   Kubadilishana mawazo na wewe kuhusiana na jinsi ya kutatua matatizo yako.
o   Kukuunganisha na Asasi zenye rasilimali ambazo zinaweza kukusaidia kuleta mabadiliko.
o   Kuunga mkono juhudi zako ili uweze kutambua haki zako.
o   Kufanya kazi na wewe ili kuendeleza uwezo wako.

NB: 
Watanzania wenzangu, nashukuru sana kwa kuwa umekuwa nami katika mfululizo wa mwongozo wa bajeti tangu sehemu ya kwanza mpaka sehemu hii ya mwisho. Kuelewa, kushiriki pamoja na kuifuatilia bajeti ni jambo la muhimu kwa kila mtanzania mwenye kupenda maendeleo ya kweli. 

Hivyo napenda kuwaasa watanzania wote kwa ujumla kuwa, tusichoshwe wala kupuuzia juu ya ufuatiliaji wa bajti za halmashauri zetu ili kujua ni jinsi gani pesa zetu za kodi zinavyotumika na kama zinakidhi haja na kutekeleza vipaumbele vyetu katika maendeleo ya halmashauri zetu na Taifa kwa ujumla. 

Unaweza kunitumia email: kattymax2001@yahoo.com au kunifuatilia katika blog hii ili kuendelea kupata elimu zaidi. 

Mungu ibariki Tanzania na watu wake.

Friday, June 15, 2012

BAJETI MWONGOZO - SEHEMU YA 3.


Mzunguko wa bajeti katika Serikali za Mitaa


Bajeti ya Serikali za Mitaa hufuata utaratibu ule ule unaotumiwa na bajeti ya serikali kuu. Hatua ya 1 na 2 inahusu upangaji wa bajeti na hatua ya 3 na 4 inahusu matumizi  na ufuatiliaji. Jedwali lifuatalo linafafanua zaidi kuhusu Mzunguko wa Bajeti ya Serikali za Mitaa. 

Hatua
Mwezi
Shuguli
Mhusika
Hatua

Hatua ya 1 na 2: Kupanga
Novemba – Desemba
OFISI YA WAZIRI MKUU- TAMISEMI huwasiliana na wizara husika. Hutoa miongozo ya Bajeti kwenye serikali za mitaa (LGAs)
OFISI YA WAZIRI MKUU-TAMISEMI

Hatua ya 3  na 4: matumizi na ukaguzi
Januari
LGA ina 50% ya fedha kwa ajili ya matumizi kutoka katika mfuko wa maendeleo wa serikali za mitaa (MKUKUTA.) Huandaa bajeti.  Kamati za maendeleo za Kata na viji nazo hupatiwa asilimia 50 nyingine ya fedha kwa ajili ya matumizi katika kata na vijiji.
Halmashauru ya wilaya/Kamati ya Maendeleo ya kata/Halmashauri ya kijiji.
Februari
Wana vijiji huchagua vipaumbele na huandaa bajeti kwa kutumia mchakato wa kuangalia fursa na vikwazo vya maendeleo. Maofisa wa kata wa wilaya husaidia katika kuandaa bajeti. Mipango hukubaliwa na halmashauri ya kijiji na mkutano mkuu wa kijiji
Halmashauri ya kijiji/mkutano mkuu wa kijiji
Machi
Kamati ya Maendeleo ya Kata huijadili na kuiunganisha mipango ya vijiji katika mipango ya kata. Mipango hupelekwa katika halmashauri ya wilaya, miji, manispaa na jiji.
Mamlaka ya serikali za mitaa na kamati ya maendeleo ya kata
Machi-Aprili
Mamlaka ya serikali za mitaa huijadili mipango ya kata na kuiunganisha katika mipango yake
Idara ya mipango ya halmashauri ya wilaya, mji, manispaa au jiji.

Aprili
Halmashauri huipitia, huijadili pamoja na kuipitisha mipango ya mamlaka ya serikali za mitaa. Sekretariati ya Mkoa huichambua mipango hiyo. Baada ya hapo mipango hiyo hupelekwa ofisi ya waziri mkuu TAMISEMI.
Halmashauri ya wilaya, kamati ya mipango ya wilaya, Sekretariati ya Mkoa (RS), ofisi ya waziri mkuu TAMISEMI

Mei
Ofisi ya waziri mkuu-TAMISEMI huchambua mipango yote ya Mamlaka za Serikali za Mitaa (LGA) na kuiunganisha kwenye bajeti ya taifa ambayo huwasilishwa bungeni.
Ofisi ya waziri mkuu TAMISEMI .Bunge

Juni –Julai
Bunge hujadili na kupitisha bajeti ya ofisi ya waziri mkuu-TAMISEMI.
Ofisi ya waziri mkuu TAMISEMI /Bunge

Agosti
Ofisi ya waziri mkuu-TAMISEMI huziarifu halmashauri kuhusu bajeti. Fedha za kila mwezi huanza kusambazwa katika halmashauri.
Ofisi ya waziri mkuu TAMISEMI /Bunge

Septemba
Halmashauri huzifahamisha kata pamoja na vijiji kuhusu bajeti. Utekelezaji wa miradi huanza kufanyika.
Halmashauri / kata/vijiji

Hatua ya 1 na 2: 
Kupanga Matumizi ya Fedha
Ubainishaji wa fursa na vikwazo katika mchakato wa maendeleo (O&OD) unalenga kuhakikisha kuwa vipaumbele vya vijiji vinajumuishwa katika bajeti ya taifa. Ni muhimu kushiriki katika mchakato huu ili kuhakikisha kuwa mahitaji pamoja na sauti zenu zinasikika.

Mchakato wa kuangalia fursa na vikwazo vya maendeleo hufanyika kwa muda wa siku 9 Wanakijiji hujadili mahitaji yao ya kimaendeleo pamoja na changamoto wanazokumbana nazo katika kufikia maendeleo yao. Kwa mfano ukosefu wa maeneo kwa ajili ya ujenzi wa vyoo katika shule za msingi; au ukosefu wa vifaa kwa ajili ya kufukia mashimo yaliyopo barabarani. Mpango huu huratibiwa na halmashauri ya kijiji kabla ya kuwasilishwa katika mkutano mkuu wa kijiji kwa ajili ya kupitishwa. Afisa mtendaji wa kata pamoja na muwezeshaji wa O&OD husimamia mchakato mzima.

Hatua ya 3: 
Matumizi ya Fedha
Wizara ya fedha (MoF) hupelekea fedha halmashauri kila mwezi. Kiwango cha fedha kinachopelekwa katika halmashauri hutangazwa kupitia magazeti. Halmashauri huvifahamisha vijiji, kata na mitaa kuwa fedha zimeletwa na serikali. Mchanganuo mzima wa fedha hizo huwekwa katika mbao za matangazo. Halmashauri huandaa utaratibu wa jinsi fedha hizo zitakavyotumika katika kata, vijiji na mitaa. Utekelezaji wa miradi huanza mara moja.

Kama kutakuwa na mabadiliko katika bajeti iliyopitishwa mwanzo, basi halmashauri ina wajibu wa kukufahamisha kuhusu mabadiliko hayo na una haki kuhoji sababu za mabadiliko katika bajeti hiyo.

Fedha zinazotumika katika kununua vitu pamoja na huduma kama vile vifaa vya ujenzi, vitabu mashuleni, pampu za maji pamoja na kulipa wataalamu mbalimbali huitwa manunuzi. Manunuzi yote lazima yaratibiwe na bodi ya zabuni ya wilaya na yanatakiwa kufanyika kwa haki, ushindani na kwa uwazi zaidi. ‘Fedha za umma’ lazima zithaminiwe na wala si urafiki.   

Hatua ya 4: 
Kuhakiki kama fedha zilizotengwa zinatumika katika miradi iliyopangwa.
Halmashauri huwasilisha ripoti katika ofisi ya waziri mkuu-TAMISEMI kila baada ya miezi mitatu kuelezea kama fedha zilizopokelewa zimetumika kwa usahihi na kufuata bajeti iliyopangwa. Ripoti hii huwasilishwa mbele ya kikao cha halmashauri   na lazima iwekwe wazi.

Halmashauri ya kijiji (VC), Baraza la Mtaa (MC) na halmashauri ya kata hukutana kila baada ya miezi mitatu lengo likiwa ni kuratibu mipango ya maendeleo katika halmashauri. Halmashauri ya kijiji na baraza la mtaa zinawajibika kuwasilisha ripoti katika mkutano mkuu wa kijiji au mtaa ambao huwahusisha watu wazima wote katika kijiji au mtaa huo. Mahesabu ya halmashauri hukaguliwa na Mdhibiti Mkuu wa Fedha za Serikali (CAG). Fedha zingine kama vile za mradi wa Barabara, Afya, Maendeleo ya Elimu (MMEM), maboresho ya serikali za mitaa pamoja na fedha zinazotolewa na wahisani, wenyewe hukaguliwa tofauti. Fedha zinazotolewa na LGCDG hukaguliwa kila mwaka ifikapo mwezi Septemba.  

Jinsi unavyoweza kushiriki
Ushiriki wako katika mchakato wa bajeti ni muhimu sana kwa sababu unakupa wewe fursa ya kuhakikisha maoni yako yameingizwa katika maamuzi ya bajeti. Ushiriki wako utawezesha vipaumbele vyako kuzingatiwa katika bajeti. Unaweza kushiriki katika hatua zote za mchakato wa bajeti kama ifuatavyo.

Hatua ya 1 na 2: Kupanga jinsi ya kutumia fedha
Unaweza kuwashawishi waandaaji wa bajeti kwa kuwaeleza kuhusu masuala yanayotakiwa kupewa kipaumbele. Labda unaweza kufikiria kuwa kuwaongezea walimu mshahara ni jambo muhimu au kutoa ruzuku kwa dawa pamoja na usambazaji wake.

o   Mchakato wa fursa na vikwazo vya maendeleo: Huu ni mpango shirikishi ambapo kila mwanakijiji anapaswa kushirikishwa kuanzia hatua ya awali. Ni vizuri uhudhurie vikao ili kutoa maoni yako kuhusu mambo yatakayoamuliwa kuhusu maendeleo na mahitaji ya kijiji chako. KILA MMOJA lazima ashiriki: wanawake, wanaume, vijana, wazee, wasiojiweza pamoja na masikini. Kila mmoja ana haki ya kushiriki na ana haki ya kusikilizwa. Vipaumbele vya kijiji ni lazima vizingatiwe wakati wa kuandaa bajeti.

o   Mikutano mikuu ya kijiji: Mikutano hii huitishwa kila mwezi. Wanawake na wanaume wote wanaoishi katika kijiji husika ni muhimu kuhudhuria. Unaweza kuuliza maswali na kudai masuala muhimu uliyoyapendekeza yawepo kwenye bajeti.

o   Kamati ya maendeleo ya kata (WDC): Mikutano ya WDC ipo wazi kwa wananchi wote kuhudhuria. Unapaswa uhudhurie ili kuhakikisha kuwa mipango ya maendeleo ya kijiji chenu imeingizwa kwenye mpango wa maendeleo wa Kata. Mpango huu hupelekwa kwenye halmashauri.

o   Mjadala wa Baraza na upitishaji wa bajeti: Unaweza kuhudhuria vikao vya Baraza la halmashauri ya wilaya ili kuhakikisha kuwa vipaumbele vilivyojadiliwa katika kijiji chenu vinatetewa na diwani wenu. Wananchi wanaweza kuwahamasisha madiwani wao ili watetee maslahi ya jamii zao pamoja na kuhakikisha kuwa mambo yote yaliyokubaliwa yamejumuishwa katika bajeti na mpango wa maendeleo wa wilaya.

Hatua ya 3 na 4: Kutumia fedha na kuhakikisha kama inatumika kwa usahihi.

Unaweza kufuatilia matumizi ya fedha ili kuhakikisha kama fedha zilizoombwa zinatumika kwa usahihi: kwa mfano kama mwanafunzi mmoja ametengewa Dola kumi za Marekani kwa mwaka kwa ajili ya shule, basi unaweza kukagua kama shule imepokea fedha hizo kutoka serikalini na iwapo zinatumika kama zilivyopangwa. Vile vile unapaswa uhakikishe kuwa huduma zilizotolewa kwa ubora unaotakiwa na kwa wakati muafaka.

Wananchi kwa kushirikiana na Asasi za Kiraia (CSO) wana nguvu na mamlaka katika kusimamia utendaji wa halmashauri (LGA). Kama unapenda, ni muhimu kuwasiliana na Asasi za Kiraia iliyo karibu nawe ili kusaidia kufanikisha mchakato huu. Kuna namna nyingi za kufanya; udhibiti wa matumizi ya Fedha za umma (PETS), usimamizi wa huduma za jamii na usimamizi wa matumizi ya fedha.

o   Usimamizi wa matumizi ya Fedha za umma: Hii hufiatilia matumizi ya Fedha kuanzia pale serikali inapozipokea hadi mwisho. Unaweza kuuliza maswali kama vile: Je, fedha zinatumika kama zilivyopangwa? Je, fedha zimefika kwa wakati? Je, kiwango cha fedha kilichopokelewa ni sahihi? Je, fedha zilizotengwa kwa ajili ya mradi fulani zimetumika kama ilivyopangwa? Je, huduma zimeboreshwa?

Mfano wa mbinu za kutumia katika kufuatilia matumizi ya umma ni kupitia kadi za viwango za kijamii (PIMA Cards). Jamii huandaa kadi maalumu zinazoonesha kiwango cha kuridhishwa ama kutoridhishwa na huduma zinazotolewa. Maswali huandikwa kwenye kadi. Huu ni mfano mojawapo wa kupima ni kwa jinsi gani kilimo kimeboreshwa. Kuna kamati maalum ambayo huchaguliwa na kupewa mafunzo ya jinsi ya kukusanya habari kutoka kwa raia wengine. Taarifa hiyo huratibiwa na kuwasilishwa katika halmashauri. 

KILIMO NA MASOKO - UZALISHAJI
B1
HUDUMA
B1 . 1
JE, HUDUMA GANI ZA KITAALAMU ZILIZOTOLEWA MWAKA JANA KATIKA KIJIJI CHAKO?
JE, ULIRIDHISHWA NA HUDUMA HIZO?

UDHIBITI WA WADUDU,
MBEGU ZILIZOBORESHWA,
USHAURI WA KITAALAMU,
USHAURI WA UTUNZAJI WA NAFAKA,
TIBA YA MIFUGO,
UTUNZAJI WA MAZINGIRA,
KUZUIA MMOMONYOKO,
KUANZISHWA VYAMA VYA MSINGI,
MBINU ZA UMWAGILIAJI,
UHIFADHI WA MAZAO,
UHIFADHI WA MAZAO YA MIFUGI
HAZIKUTOLEWA
HAFIFU
INARIDHISHA
VIZURI




 
 o   Ufuatiliaji wa uwajibikaji wa kijamii: Hii husimamia na kufuatilia utoaji wa huduma za kijamii kwa kuhakikisha kuwa serikali inatoa huduma kwa wakati muafaka, kwa ufanisi na kwa kulingana na thamani halisi ya fedha zilizotengwa. Kinyume na hivyo, viongozi wa serikali wanapaswa kuwajibika. Ni muhimu kuhakikisha kuwa fedha zilizotengwa zinatumika kwa uangalifu na kwa ufanisi. Watumishi au idara zinazoshindwa kutoa huduma kwa ubora ni muhimu waeleze ni kwa nini huduma zinazotolewa hazina ubora. Unaweza kusimamia utendaji wao.

o   Usiamamizi wa fedha: Unaweza kuisoma na kuifanyia kazi ripoti ya kila mwaka inayotolewa na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za serikali (CAG). Katika kipindi cha mwaka 2006 na 2007, Taasisi mbalimbali mfano mzuri: HakiElimu, ziliandaza machapisho yanayoelezea mapato pamoja na taarifa kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) katika mfumo rahisi. Idara za serikali kuu pamoja na halmashauri zilizowekwa katika viwango vya ubora katika utendaji kuanzia Idara ya kwanza kiufanisi hadi mwisho. Machapisho haya yalisaidia kuongeza uelewa juu ya usimamizi wa fedha za umma. Unaweza kupata taarifa kamili ya bajeti kutoka katika ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) au kwa kusoma machapisho ya vyombo mbalimbali vya habari. Kama utakuwa hujaridhika unaweza kuomba maelezo zaidi kutoka kwenye halmashauri yako kama changamoto.   

NB: Usikose kesho kupata sehemu ya mwisho wa Mwongozo wa Bajeti.