To Chat with me click here

Thursday, August 29, 2013

MWANAJESHI WA UN AUAWA NA WAASI (M23) DRC



Umoja wa Mataifa umesema kuwa mwanajeshi wake mmoja wa kutunza amani ameuawa na wengine watatu kujeruhiwa kufuatia mapigano makali kati ya na wapiganaji wa waasi Mashariki mwa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Wanajeshi wa serikali ya Congo
Msemaji wa Umoja wa Mataifa mjini New York, Farhan Haq, hata hivyo hajatangaza uraia wa wanajeshi waliouawa au kujeruhiwa.

Wanajeshi hao wa Umoja wa Mataifa walitumia ndege za helicopta kuwasukuma nyuma wapiganaji wa M23 karibu na mji wa Goma, ambao ndio mji mkubwa zaidi katika eneo hilo la Mashariki. Watu themanini waliuawa kwenye mapigano hayo wiki iliyopita.
 
Mwaka wa 2012, waasi wa M23 waliuteka mji huo kwa muda kabla ya kuondoka kufuatia shinikizo kutoka kwa jamii ya kimataifa. Umoja wa Mataifa Umetuma kikosi maalum katika eneo hilo lenya utajiri mkubwa wa madini kukabiliana na waasi hao.
 
Wanajeshi hao wa Umoja wa Mataifa MONUSCO, wanapambana na wapiganaji hao wa waasi kwa ushirikiano na wanajeshi wa serikali. Jeshi hilo la Monusco limelazimika kufanya mashambulio ya anga na ardhini ili kuzuia waasi hao wa M23 kukaribia Goma na ripoti zinasema mapigano makali yanaendelea katika maeneo ya milima ya Kibati, takriban kilomita kumi na tano Kaskazini mwa Goma.
 
Watu wapatao laki mbili wanasemekana kuishi katika eneo hilo la Kibati. Wapiganaji wa M23 wamesema kuwa wanajeshi wa Congo na wenzao wa Umoja wa Mataifa walifanya mashambulio ya anga na ardhini katika maeneo wanayoyadhibiti, Kaskazini mwa Goma.
 
Daktari mmoja mjini Goma, Isaac Warwanamiza, ameliambia shirika la habari la AP kuwa aliona miili ya watu themanini na wawili, ishirini na tatu zikiwa za wanajeshi wa serikali. Umoja wa Mataifa una zaidi wanajeshi elfu kumi na nane nchini Congo.

No comments:

Post a Comment