To Chat with me click here

Saturday, August 31, 2013

FIB TANZANIA (SPECIAL FORCES IN CONGO) YAICHUKUA NGOME KUU YA M23!



FIB Tanzanian Special Forces (part of MONUSCO) imeichukua ngome kuu ya waasi wa M23 ya Kibati (Nyirangongo Territory - Goma, Eastern DRC).

Mizinga ya wapiganaji wetu ilirindima na kutembeza mabomu mfululizo huku askari wetu wa miguu wakipanda mlima ulio eneo hilo na kisha kuichukua ngome hiyo.

Yadaiwa vijana wa jeshi letu JWTZ wamepeleka mashambulizi makali ya mabomu yaliyopelekea waasi wa kundi la M23 kuikimbia ngome yao na hivyo kuanza kukosa mwelekeo.



Kwakweli napenda kutumia fursa hii kwa niaba yangu binafsi, Blog hii (Maxmillian Kattikiro Blog), wadau mbalimbali na wapenda AMANI wote kuwapongeza sana wanajeshi wetu kwa ushujaa wao na kujitolea kwao katika kutetea haki za raia wasio na hatia wa jirani zetu wa CONGO, na Afrika kwa ujumla. 

Mungu awabariki, awalinde na kuwasimamia, huku akiwashindia katika mapigano hayo. Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika na watu wake. 
 

No comments:

Post a Comment