To Chat with me click here

Tuesday, June 4, 2013

KAWAMBWA KITANZINI LEO, BAJETI YAKE HATARINI KUPITISHWA



Dodoma,Tanzania

Waziri wa Elimu na Mfunzo ya Ufundi,Dk Shukuru Kawambwa
WAKATI Watanzania wakijiandaa kufuatilia hotuba ya Bajeti ya Wizara ya  Mafunzo ya Ufundi leo Waziri wa Wizara hiyo, Dk Shukuru Kawambwa anatarajia kukutana na upinzani mkali, kutoka kwa wabunge wa pande zote mbili yaani Upande wa Upinzani na Wapunge wa CCM.

Habari zilizonaswa na Vyanzo vyetu vya habari zinadai kwamba, Wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamejipanga kukwamisha hotuba ya Wizara hiyo, kwa madai kwamba Waziri huyo ameshindwa kusimamia sekta ya Elimu.

Vyanzo vya habari kutoka ndani ya CCM mjini Dodoma zinadai kwamba, Wabunge hao wamepania kukwamisha hotuba hiyo na kumtaka Waziri huyo ajiuzuru ili kukisafisha Chama hicho kutokana na aibu ya mkanganyiko wa kufeli kwa Wanafunzi mwaka huu.

"Hotuba ya Wizara ya Eilimu haiwezi kupitishwa kirahisi kama Kawambwa hata jiuzuru, hatuwezi kuendelea kuwa na mawaziri wanaoshindwa kuwajibika ipasavyo katika setka zao, kitendo cha mawaziri hao kushindwa kuwajibika ipasavyo ndiyo inayochangia kuharibu Chama"kilisema chanzo hicho kwa masharti ya kutotajwa majina yake na kuongeza:

"Huu mpango unaendelea kusukwa na wabunge wa CCM waliopania kurudisha heshma ya Chama, lakizima tuanzie ndani kuwajibishana wenywe kabla ya wapinzani kuanza, kwani tukishindwa sisi watatumia udhaifu wetu kuwashawishi wananchi na hatimaye watazidi kuichukia Serikali". Wakati Waziri Dk Kawambwa akiandaliwa mazingira ya kung'olewa, Necta inatarajia kutangaza matokeo yaliyoongeza kiwango  cha  ufaulu kufikia asilimia kati ya 54 na 57, wiki hii pamoja na yale ya kidato cha sita ambayo pia yamechelewa kutangazwa.

No comments:

Post a Comment