To Chat with me click here

Tuesday, June 11, 2013

MLIPUKO WA MALARIA NCHINI TANZANIA UKO KWENYE MAENEO AMBAYO HAYAKUPULIZWA DAWA




Mlipuko wa hivi karibuni wa malaria mkoani Kagera, Tanzania, ulikuwa tu kwenye vijiji ambavyo havikujumuishwa kwenye Programu ya Kupuliza Dawa Majumbani, liliripoti gazeti la Daily News la Tanzania siku ya Jumatatu (tarehe 10 Juni).

Serikali imetuma timu ya watalaamu kwenye eneo hilo kuchunguza mlipuko huo wa malaria, ambao umeshaua kiasi cha watu 20, wengi wao watoto wadogo, tangu mwishoni mwa mwezi Mei. Vile vile, Wizara ya Afya, imeagiza dawa zaidi kutumwa kwenye hospitali ya karibu ya Rubya, ikikanusha taarifa kwamba mlipuko huo ulisababishwa na upungufu wa vidonge vya kupambana na malaria.

Kila siku kiasi cha watu 30 hadi 40 hufika Hospitali ya Rubya wakiwa na malaria. Wastani wa mtoto mmoja hadi wawili hufa kila siku, alisema Afisa wa Matibabu Hospitali ya Rubya, Diocles Ngaiza. "Katika siku ya kwanza ya mlipuko, vilirikodiwa vifo 16, vingi vikiwa vimesababishwa na watoto hao kufikishwa hospitalini ikiwa wameshachelewa sana," alisema.

No comments:

Post a Comment