To Chat with me click here

Tuesday, June 11, 2013

WACHIMBA MIGODI 55 WAAFRIKA, JELA- GHANA




Polis nchini Ghana wamewatia nguvuni watu 55 raia wa nchi mbali mbali kutoka Afrika Magharibi wanaoshukiwa kuendesha shughuli haramu za uchimbaji haramu wa dhahabu, msemaji wa wizara ya uhamiaji alisema.

Kukamatwa kwao kunaashiria kuwa polisi wameelekeza nguvu zao sasa kwa wahamiaji wa Kiafrika kutoka kwa Wachina kama anavyo ripoti mwandishi wa BBC Akwesi Sapong akiwa nchini Ghana.

Serikali hiyo ya Ghana iliwaachilia washukiwa 124 raia wa Uchina wikendi na kuwaamuru waondoke nchini humo mara moja. Sheria za Ghana zimeharamisha mwananchi yeyote wa kigeni kuajiriwa katika migodi midogo midogo ya nchi hiyo. Ghana ndio nchi ya pili kwa uzalishaji mkubwa wa dhahabu barani Afrika baada ya Afrika Kusini.

MWINGILIO WA UCHINA

Wachina watoa dhahabu Ghana
Kukamatwa kwa wageni imepokewa vizuri na raia wa Ghana masikini wanaoamini kuwa wafanyikazi kutoka nje wanadakia nafasi zao za ajira, kwa mujibu wa mwandishi wetu.

Msemaji wa wizara ya Uhamiaji Francis Palmdeti ameambia BBC kuwa kati ya 55 waliokamatwa, 51 ni raia wa Niger, 3 wametoka Togo na mmoja kutoka Nigeria.

Wachina waliokamatwa Ghana
'Bado uchunguzi unafanywa wa asili ya washukiwa wengine watatu baada wamedai kuwa raia wa Ghana na kukana kuwa wametoka Mali kama tulivyo shuku awali' amesema msemaji huyo.

Mwandishi wa BBC anasema kuwa oparesheni kama hii inamaanisha kuwa serikali imeazimia kumaliza uajiri wa mtu yeyote ambaye siye raia wa Ghana katika machimbo ya nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment