To Chat with me click here

Thursday, June 27, 2013

KENYA YATISHIA KUCHUKUA HATUA KALI DHIDI YA VURUGU ZA KOO


Maofisa wa usalama wa Kenya Jumatatu wakionyesha silaha zilizokamatwa wakati wa mapigano ya koo katika wilaya ya Rhamu, Kaunti ya Mandera.

Polisi huko kaskazini mashariki mwa Kenya wameimarisha usalama katika kaunti ya Wajir kuzuia vurugu zilizoenea kutoka Kaunti jirani ya Mandera baina ya koo za Degodia na Gare.


Vurugu za hivi karibuni ziliibuka huko Wajir zilianza Ijumaa iliyopita (tarehe 21 Juni) wakati wanaume washukiwa wa koo za Degodia walipovamia malori mawili katika kijiji cha Eldas, na kuua wanaume wanne wa koo za Gare, Mkuu wa Kaunti ya Wajir Naftali Mung'athia alisema.

Katika kulipiza kisasi kwa mfululizo wa mashambulio ya hivi karibuni dhidi ya Gare, wanaume wenye silaha walivamia kambi ya watu wasio na makazi ndani ya nchi katika wilaya ya Banisa ya Kaunti ya Mandera, na kuua watu 14 ikiwa ni pamoja na ofisa polisi Jumapili. Waliokufa, ni pamoja na wanawake na watoto, wote kutoka ukoo wa Degodia.
Baadhi ya Familia zilizokosa makazi.

Jumatatu, kundi la watu kutoka katika ukoo wa Degodia waliwalenga watu kutoka ukoo wa Gare katika ghasia kwenye mji wa Wajir, walimuua mwanamke mmoja na mwingine kujeruhiwa vibaya baada ya kukanyagwa na msafara uiokuwa ukibeba familia zilizokuwa zikikimbia vurugu hizo.

Kuepusha mapigano zaidi baina ya koo mbili hizo, mamlaka zinazohusika zimesambaza maofisa usalama na askari katika viunga vyote vya jirani na Wajir, Mung'athia alisema. Alitoa wito kwa wakaazi wa Wajir kuwa watulivu wakati serikali ya Kaunti ikifanya kazi kutatua mzozo huu, akiongezea kwamba upigaji marufuku wa muda wa mikusanyiko imetekelezwa. 

"Tunafanya kazi mchana na usiku kuzuia mzozo kutokuendelea," Mung'athia alisema. "Tumewataka viongozi wa ndani na maulamaa kuungana katika kurejesha amani baina ya koo hizi."

Historia yenye vurugu

Wimbi la hivi karibuni la vurugu hizi lilianza mwezi Machi wakati wa gari la kampeni linalomilikiwa na mgombea seneta Billow Kerrow, ambaye anatoka katika ukoo wa Gare, lilipomgonga na kumuua mfanyabiashara kutoka katika ukoo wa Degodia huko Rhamu. Baadhi ya wanachama wa jumuiya ya Degodia walidai ajali ilikuwa imepangwa.

Kutoka hapo, mapigano ya koo, na mashambulizi ya kulipiza kisasi yameshaua watu zaidi ya 50 na kufanya mamia ya familia kukosa makazi. 

Vurugu baina ya koo mbili hizio yamekuwa yakipamba moto siku hadi siku, na yalianza kuongezeka kutoka mwaka 1984 wakati ukame uliposababisha mzozo wa maeneo ya malisho, kwa mujibu wa Mkuu wa Kaunti ya Mandera Michael ole Tialal.

Gare ni ukoo unaotawala huko Mandera, wakati Degodia ni wengi huko Wajir.
Usambazaji mdogo wa maji na ardhi ya malisho yamekuwa ni maeneo ya mzozano kati ya koo hizo, Tialal alisema, akiongeza kwamba kuenea kwa bunduki katika mpaka wa Somalia na Ethiopia kumeongeza vurugu katika tatizo la usalama la mkoa. 

"Ni mara ya kwanza kwa ukoo kutumia chombo cha kurushia maguruneti katika mapigano yao ya koo," Tialal alisema, akirejea shambulio kwenye kambi katika wilaya ya Banisa. "Vurugu hizo pia zilihusisha kuchoma nyumba na kuvamia magari." 

"Kwa sasa tunatoa kikundi cha walinzi cha wasindikizaji wenye silaha na magari yanashauriwa kusafiri kwa kusindikizwa na ulinzi ili kupunguza [uwezekano wa] shambulio,".

Siku ya Jumatatu, Inspekta Jenerali wa Polisi wa Kenya David Kimaiyo aliwaita viongozi waliochaguliwa wa kaunti za Mandera na Wajir katika idara ya Uchunguzi wa Makosa ya Jinai kuhusiana na ripoti za upelelezi zikionyesha kwamba mashambulizi "yalichochewa kisiasa".

Baada ya kukutana Nairobi siku ya Jumatatu na viongozi wa kaunti zote mbili, Rais Uhuru Kenyatta alisema serikali ya Kenya inaweza kutumia nguvu kurejesha amani katika mkoa wa kaskazini-mashariki, akiagiza jamii zinazopigana kusalimisha silaha haramu. 

"Kama jamii za kaunti za Mandera na Wajir hawatarejesha amani wao wenyewe, serikali itakuwa haina lingine la kufanya bali kutumia operesheni ya ulinzi ambayo inaweza kutokuwa na matokeo yasiyodhamiriwa," rais alisema.
Pia Kenyatta aliahidi kufanya kazi na serikali ya Ethiopia kuhakikisha kuishi pamoja kwa amani miongoni mwa jamii nyingine za kikabila zilizoenea katika mkoa ambako mipaka ya Kenya, Ethiopia na Somalia inakutana.

Rasilimali, siasa za mafuta zaleta ugomvi

Licha ya jitihada za kuzuia vurugu katika ngazi za kaunti na taifa, mlipuko wa vurugu umeendelea kujitokeza.

Siku ya Jumanne (tarehe 25 Juni), viongozi wa ulinzi katika kijiji cha Guba walimpiga mtu mmoja risasi na kumuua wakati wakipigana na wanaukoo wenye silaha ambao walikuwa wanatuhumiwa kupanga shambulizi kwa wanakijiji, alisema Naibu wa Mkuu wa Kaunti ya Mandera Sammy Mwati.

Katika miezi iliyopita, vikosi vya usalama viliwakamata watu zaidi ya 90 kuhusiana na mashambulizi hayo, Mwati alisema, na baadhi ya viongozi wa jamii pia wamekuwa wakihojiwa kwa kutuhumiwa kuhusika katika mapigano. 

Sheikh Mohamed Deeq, imamu wa msikiti wa Jamia Salaam katika mji wa Wajir, alisema baadhi ya viongozi wa jamii wanachochea mgogoro kupitia kauli za kuchochea. 

"Baadhi ya viongozi wa jamii kutoka katika mkoa huo sio wakweli kwa wito wao wa amani," aliiambia Sabahi. Viongozi wanahubiri amani lakini wanachochea vita kwa kujificha na katika mioyo yao." 

Ingawa viongozi wa dini wamekutana kusaidia kurejesha utulivu katika kaunti zote, jitihada kubwa inahitajika, alisema.

"Kama viongozi wa dini, inaonyesha pia hatukutimiza wajibu wetu kikamilifu," alisema. "Tutakutana kama viongozi wa dini mara moja kutathmini mafundisho yetu. Tunahitaji sana kuboresha jitihada zetu katika kuwafundisha watu mafundisho ya Mungu."

Utatuzi wa Kimila kwa vurugu za koo

Magavana wa kaunti hizo mbili pia wanashirikiana kumaliza vurugu.
Gavana wa Kaunti ya Wajir Ahmed Abdullahi na Gavana wa Kaunti ya Mandera Ali Ibrahim Roba walikubaliana wakati walipokutana na Kimaiyo tarehe 28 Mei kuwazuia watu wa koo zao kufanya vurugu. Wametoa wito pia kukomeshwa mara moja vurugu za kikabila katika Kaunti ya Mandera.

"Kuna faini ya shilingi milioni 10 (dola 116,000) kwa jamii nzima itakayochochea vurugu," Abdullahi aliiambia Sabahi. "Serikali ilipaswa kutekeleza mapendekezo na tunaunga mkono."

Faini inazingatiwa kamamaslah, kitendo cha kimila kinachofanyika huko kaskazini mashariki nchini Kenya ambako familia zilizopoteza wapendwa wao katika vurugu za kikabila zinapata malipo kwa ajili ya uharibifu kutoka katika ukoo unaokwaza, alisema.

"Mgogoro huu unatutishia kutofanya shughuli za maendeleo kwa ufanisi," Roba aliiambia Sabahi. "Ndiyo sababu mimi binafsi ninajitolea kumaliza vurugu."

Aidha, jamii zote zitazingatiwa katika kazi za serikali za kaunti na kuingizwa katika ajenda ya maendeleo, alisema.

Familia za Degodia ambazo zilikimbia makazi yoa kwa sababu ya vurugu za koo zimekuwa zikikaaa katika kambi nje ya ofisi za mkuu wa wilaya ya Rhamu katika Kaunti ya Mandera tangu mwezi Machi.

Ibrahim Kullow Ahmed, mkaazi wa Rhamu mwenye umri wa miaka 24, alisema alikimbia makazi yake kwa sababu yeye na majirani zake walikuwa wakiishi wakiwa na hofu ya kushambuliwa.

"Nyumba zetu zilichomwa moto na sasa tumepiga kambi katika ofisi za serikali za mitaa," aliiambia Sabahi. "Watu wanahofu sana kwa sababu mashambulizi yanafanyika hata mchana."

"Watoto wanakabiliana na wasiwasi usiku na misikitini," alisema, akiongeza kwamba wanakosa chakula na maji.

Info Source: Sabahi Online

No comments:

Post a Comment