To Chat with me click here

Wednesday, April 11, 2012

MSIBA WA KANUMBA ....

Maelfu ya waombolezaji wakiwa wanausindikiza mwili wa marehemu Kanumba katika makazi yake ya milele katika makaburi ya Kinondoni Dar-es-Salaam.
Mwili wa marehemu Steven Kanumba ukiteremshwa kwenye nyumba yake ya milele mara baada ya taratibu zote za kumuuga kumamilishwa katika viwanja vya leaders club hapo jana.
Mwili wa aliyekuwa muugizaji wa Filamu Tanzania ndg. Steven Kanumba mara baada ya kuwasili katika makaburi ya Kinondoni Dar es Salaam, kwa ajiili ya mazishi yake hapo jana jioni majira ya saa kumi jioni.
Mwili wa Marehemu Steven Kanumba ukiondolewa katika viwanja vya Leaders Club ukielekea makaburi ya Kinondoni kwa ajili ya mazishi yake, huku kila aliyekuwepo akitaka hata kugusa gari lililokuwa limebeba mwili huo.
Kila mtu alikuwa akitaka hata alisogelee au hata kushika au kuiona tu picha ya marehemu kanumba, kwa kweli alikuwa akipendwa na watu. 
Mwili wa Marehemu Kanumba ukianza kuondolewa tayari kwa kuanza safari yake ya mwisho kuelekea katika makaburi ya kinondoni kwa ajili ya kwenda kuupumzisha katika makao yake ya milele.
Mhe. Joseph Mbilinyi (a.k.a SUGU) akiwa na baadhi ya viongozi na aliye kada wa CCM pia mfadhili wa CHADEMA ndugu; Sabodo wakielekea kutoa heshima zao za mwisho kwa marehemu Steven Charles Kanumba katika viwanja vya Leaders Club hapo jana
Mhe. Ghalib Bilali akiongoza viongozi wengine wa kiserikali na watanzania kwa ujumla katika kutoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa gwiji wa sanaa ya filamu Tanzania Steven Kanumba, katika viwanja vya Leaders hapo Jana.  
Baadhi ya wasanii wa filamu Tanzania wakiwa wameketi karibu kabisa na Jeneza la aliyekuwa muugizaji maarufu wa Filamu Tanzania ndg. Steven Kanumba, tayari kwa kuanza misa ya kumwombea marehemu kama wanavyoonekana pichani.
Wasanii wa Tansia ya Filamu Tanzania wakiwa wamezunguka Jeneza la mpendwa wao Steven Charles Kanumba huku wakijadili jambo, mara baada ya kuuwasilisha mwili huo katika viwanja vya Leaders Club kwa ajili ya kuutolea heshima za mwisho.
Steven Nyerere aliyebeba msalaba wa wajina wake marehemu Steven Charles Kanumba walipokuwa wakiuingiza mwili wa marehemu katika viwanja vya leaders kwa ajili ya kutoa heshima zao za mwisho.
Kwaya ambayo marehemu Steven Charles Kanumba aliyokuwa ni mshiriki ikiimba na kuomboleza katika msiba huo, ambapo marehemu alikuwa akiagwa na watanzania wote kwa ujumla.
Mwili wa marehemu Steven Charles Kanumba ukiwa tayari kwa kuombewa mara baada ya kuwasili kwenye viwanja vya Leaders Club hapo jana.
Mwili wa aliyekuwa Gwiji wa sanaa za uigizaji wa Filamu Tanzania Steven Charles Kanumba ukiwa umebebwa na baadhi ya wasanii wenzake wa Tansia hiyo ya Filamu mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Leaders Clubu hapo jana.
Dada wa marehemu Steven Charles Kanumba akisaidiwa na baadhi ya wasanii mara baada ya kuwasili viwanja vya Leaders huku akiwa ajiwezi kutokana na majonzi makubwa ya kuondokewa na mpendwa kaka yake.
Hili ndilo Jukwaa Kuu ambalo walilokuwa wameketi waheshimiwa Viongozi waliojitokeza ili kuuaga mwili wa Marehemu Steven Charles Kanumba siku ya Jumanne katika viwanja vya Leaders Club.
Mhe. Ghalib Bilali, Makamu wa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, naye akiwasiri katika viwanja vya Leaders Club kwa kumuaga Mpendwa wetu Steven Charles Kanumba. Makamu wa Rais ndiye aliyekuwa mgeni rasmi katika shughuli hiyo.
Mhe. M. Sadick-Mkuu wa Mko wa Dar-es-Salaam, akiongozana na Mhe. Zungu Mbunge wa Ilala, akiwa anawasili katika viwanja hivyo vya leaders kwa ajili ya kumuuaga marehemu Steven Charles Kanumba.

No comments:

Post a Comment