Dar es Salaam,Tanzania
![]() |
Rais wa Tanzania, Ndg. Jakaya Mrisho Kikwete. |
SAKATA
la Video inayodaiwa kuwa ilitoboa siri ya Rais Kikwete kutinga Ikulu kwa msaada
wa kura za Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF) Profesa Ibrahim Lipumba,
imeendelea kukigawa chama hicho baada ya Naibu Katibu Mkuu Chama hicho Tanzania
Bara, Julius Mtatiro kukataa kuzungumzia video hiyo, alikataa katakata na
kuwashauri waandishi wawasiliane na Profesa Lipumba amabye pia aliwahi kukataa
kuzungumzia video hiyo.
Itakumbukwa
kuwa kumekuwepo tuhuma dhidi ya Rais Kikwete na CCM kuwa mwaka 2010 waliendesha
propaganda chafu za udini zenye lengo la kuwagawa Watanzania hususan Wakristo
na Waislamu kwa manufaa yao ya kisiasa.
Mwelekeo
huo wa kisiasa wa Rais Kikwete na CCM unadaiwa kutokana na hatua ya viongozi wa
Kanisa Katoliki nchini kupitia Idara ya Uchungaji kutoa waraka maalumu
uliowataka Watanzania kuchagua viongozi waadilifu.
Waraka
huo haukuifurahisha CCM, ambayo imekuwa inagubikwa na tuhuma nyingi za ufisadi.
Makada na viongozi wa CCM walijaribu kuupinga kwa kuupotosha, wakisema
unaingiza mambo ya dini katika siasa.
Kanisa
Katoliki lina utaratibu wa muda mrefu wa kutoka nyaraka kuelekeza waamini na
wananchi juu ya mambo ya msingi katika jamii.
Katika
hali hiyo, Rais Kikwete na CCM wanadaiwa kukimbilia kwa viongozi wa Kiislamu na
kuwaomba wawaunge mkono kwa kuwajaza maneno ya uongo, kwamba Wakatoliki walikuwa
wamewaagiza waumini wao kupigia kura wagombea wa Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (CHADEMA).
Inadaiwa
waliwafitinisha zaidi kwa kuwaeleza kuwa aliyekuwa mgombea kiti cha rais wa
CHADEMA katika uchaguzi huo, Dk. Willibrod Slaa ambaye ameshawahi kuwa Padri,
alikuwa ametumwa na Kanisa Katoliki ili kuendeleza utawala wa Kikristo nchini.
Propaganda
hizo hazikuishia kwa viongozi na waumini wa Kiislamu tu, bali zilielekezwa pia
kwa viongozi na wafuasi wa CUF ambao walirubuniwa na kushawishiwa kumpigia kura
“Muislamu mwenzao” Rais Kikwete, huku wakiahidiwa kuwa mwaka 2015 Waislamu wa
CCM nao watampigia kura mgombea wa CUF kwa hoja kuwa CCM watakuwa wamesimamisha
mgombea Mkristo. Licha ya madai hayo ya udini kuwa wazi kwa muda mrefu,
lakini wakati wote Rais Kikwete na CCM wamekuwa wakikanusha tuhuma hizo na
kuziita kuwa uongo na uzushi.
No comments:
Post a Comment