To Chat with me click here

Thursday, August 29, 2013

BUNGE LA EALA LAKWAMA BAADA YA WABUNGE KUSUSIA KIKAO!


Wabunge wa Tanzania kwenye bunge la Afrika Mashariki(EALA) wakitoka ndani ya ukumbi wa bunge hilo jana kupinga wabunge wenzao wanaoshinikiza hoja zao kwa kutoka kwenye vikao vya bunge. Kutoka kushoto ni Mh.Twaha Taslima, Mh.Shyrose Bhanji,Mh.Abdullah Mwinyi na Mhe Nderakindo Kessy
Chemba ya Bunge la Afrika Mashariki inavyoonekana wakati kikao kikiendelea

 Arusha. Kikao cha Bunge la Afrika Mashariki (EALA), jana kilivunjika kwa mara ya pili baada ya Wabunge wa Tanzania, kutoka ndani ya ukumbi wakipinga kanuni kuvunjwa juzi.

Baada ya wabunge wa Tanzania kutoka nje, Spika wa Bunge hilo, Margareth Zziwa aliahirisha Bunge kwa dakika 15 ili kuweka mambo sawa, lakini jitihada za kuwashawishi ziligonga mwamba na kuamua kuahirisha Bunge hadi leo.

Hata hivyo, Mbunge wa Tanzania, Makongoro Nyerere hakuungana na wenzake kugoma kwani alibakia ukumbini na kuungana na wabunge 32 wa Burundi, Kenya, Uganda na Rwanda.

Awali, Mbunge Abdullah Ali Hassan Mwinyi alitoa msimamo wa wabunge wa Tanzania kuwa walitoka, kupinga kitendo cha wabunge wengine kudharau kiti cha Spika juzi na kutoka nje ili kushinikiza hoja yao.

Mwinyi alisema ili kushinikiza kuheshimiwa kiti cha Spika, wameamua kutoka nje ya ukumbi huo kwa kuonyesha hawaungi mkono, tabia ya baadhi ya wabunge kushinikiza hoja zao, kujadiliwa na Bunge hata kwa kukiuka kanuni na taratibu.

“Jana(juzi) ilikuwa ni mara ya pili wenzetu, kudharau kiti cha Spika na kutaka kutoa hoja na kujadiliwa bila kufuata kanuni, sasa tumeona ni vizuri na sisi kwa kupinga kuvunjwa kanuni, tutoke ili kuonyesha tunapinga mchezo huu,” alisema Mwinyi.

Mwinyi alisema kitendo cha wabunge wenzao kutoka nje ya ukumbi kwa kukataliwa kuvunja taratibu, kinadhalilisha kiti cha Spika na hata wabunge wenyewe.

Mbunge mwingine wa Tanzania, Twaha Taslima alisema kanuni zipo wazi kuwa kama mbunge ana hoja na kutaka Bunge lijadili mambo ambayo si ya dharura ni lazima aiwasilishe saa 24 kabla kwa Spika.

“Sasa jana(juzi), Mbunge wa Kenya, Peter Mathuki alitaka hoja yake ya kutaka utaratibu wa kufanyika bunge kwa mzunguko ijadiliwe kitu ambacho hakikuwa sahihi,” alisema Taslima.

Muthuki, juzi aliungwa mkono na nchi zote wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), isipokuwa Tanzania.

Jana aliwasilisha hoja hiyo kwa kufuata utaratibu lakini haikujadiliwa baada ya wabunge wa Tanzania kutoka nje.

Katika hoja hiyo, msimamo wa wabunge wa Tanzania na Kamati ya Uongozi ya Bunge ni kuwa vikao vyote vifanyike katika ukumbi wa Bunge, Arusha baada ya kukamilika.

Wabunge wa Tanzania ambao jana walitoka ni Shyrose Bhanji, Profesa Nderakindo Kessy na Taslima. Wabunge wanne hawakuwapo.

Kwa mujibu wa kanuni za Bunge hilo, kama wabunge watatu wa nchi moja, wakitoka nje kupinga jambo lolote basi kikao kinaahirishwa kwa dakika 15 na wasiporejea bunge linaahirishwa.

Akizungumzia mgogoro huo, Ofisa Habari wa EALA, Bobi Odiko alisema kilichotokea jana si ukiukwaji wa taratibu na kuongeza kuwa ana imani mambo yatakuwa sawa na vikao vitaendelea leo kwa amani.

KUMBE! JEURI, KIBURI CHA KAGAME VINATOKA KWA WAZITO!



Paul Kagame; Rais wa Rwanda
Aliyekuwa Rais wa Marekani Bill Clinton, hivi majuzi amemtetea Kagame kutokana na tuhuma zinazomkabili za kuwasaidia waasi wa M23 nchini DRC.

Kwa muda wa miezi takriban minne kumekuwa na maneno ya kejeli kutoka kwa Serikali ya Rwanda na kwa hakika maneno hayo yanatoka mdomoni mwa Rais Paul Kagame na maofisa wa ngazi za juu katika Serikali yake.

Kagame amekuwa mbogo baada ya Rais Jakaya Kikwete kumshauri afanye mazungumzo na wapiganaji wa Kihutu waliokimbilia Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) baada ya kutuhumiwa kufanya mauaji ya kimbari nchini mwake mwaka 1994.

Inakadiriwa kuwa Watutsi na Wahutu 800,000 wenye msimamo wa wastani waliuawa wakati huo, ingawa takwimu hizo zina utata, kwani wako wanaodai kuwa nchi hiyo wakati huo ilikuwa na idadi ndogo ya watu ambao idadi hiyo inasemekana ndio waliouawa.

Pia, wapo wale ambao wanaweza kushangaa kwa nini Kagame amekuwa hivyo na kuikosea heshima Tanzania, nchi ambayo imekuwa mstari wa mbele kupokea wakimbizi wake toka miaka ya 1960 na kwa nini Rais Kikwete alitoa ushauri huo.

Kagame hakupendezwa na ukweli huo kwani kila mara amekuwa akikataa kuwa hana mkono katika mapigano yanayoendeshwa na vikundi vya msituni vinavyoanzishwa nchini DRC kila inapotokea hali kutulia.

Kikwete amekuwa akijua jambo hili kwa muda mrefu kwani amekuwa Waziri wa Mambo  ya Nje kwa kipindi cha miaka kumi na amekuwa akihudhuria mikutano ya kutafuta amani ya DRC bila mafanikio kwa sababu kila kikundi kinapoingizwa katika jeshi la DRC na kudai kuwa kimemaliza vita kinazuka kikundi kingine ambacho nacho kinaanzisha mapambano dhidi ya serikali.

Kofi Annan, Katibu Mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa (UN) alikuwa mkuu wa shughuli za kijeshi za umoja huo kabla hajapanda cheo na kuwa katibu mkuu wa umoja huo, alipotembelea Rwanda baada ya kumalizika kwa vita ya wenyewe kwa wenyewe, msafara wake ulirushiwa nyanya.

 Hiyo ilikuwa ni kama kumpa ujumbe kuwa hakuna alichofanya wakati  ule Watutsi walipouawa na Wahutu mwaka 1994.

Masikini! Annan angefanya nini wakati alipokuwa akiyaomba mataifa makubwa kuingilia kati ili kusitisha mauaji kila moja lilikuwa likiangalia maslahi yake na ulikuwepo mpango wa uchelewashaji wa makusudi.

Baadaye Annan alipokuwa akigombea Ukatibu Mkuu wa UN ni Rwanda pekee katika nchi za Afrika ndiyo iliyopinga na hata alipokuwa akiomba kuongezewa muda ni nchi hiyo iliyokuwa kinara wa kumpinga wakati ukweli ni kuwa mambo yote yaliyokuwa yakifanyika wakati huo Kagame alikuwa akiyajua.

Aliyekuwa Mkuu wa Majeshi ya Rwanda, Meja Jenerali Kayumba Nyamwasa, alinukuliwa na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC)  akiwa uhamishoni Afrika Kusini akithibitisha kuwa vikundi vyote vimekuwa vikianzishwa na Kagame kwa nia ya kuhakikisha kuwa Wahutu na jeshi la zamani la nchi hiyo ambalo kwa sehemu kubwa linaundwa na waliokuwa vijana wa Inteharamwe hawapati muda wa kujijenga.

Kwa maneno mengine, Kagame ameifanya ardhi ya DRC kama uwanja wa mapambano kati yake na wapinzani wake ambao wako mashariki mwa nchi hiyo.

Jenerali Nyamwasa, ambaye kabla ya kukimbilia Afrika Kusini alikuwa Balozi wa Rwanda nchini India anasema kuwa Kagame ndiye aliyeamrisha kutunguliwa kwa ndege iliyokuwa imebeba ujumbe wa nchi hiyo  pamoja na Rais Juvenal Habyarimana na Cyprian Ntyaramira wa Burundi ambao ulikuwa umetokea Tanzania kwenye mkutano wa kujadili amani ya nchi hiyo.

Baada ya vita kumalizika na hatimaye RPF kuchukua uongozi, Ufaransa, mtawala  wa zamani wa Rwanda ilimtuhumu Kagame kwa kusababisha mauaji ya kimbari kwani Wahutu wasingianzisha chinja chinja ya Watutsi kwa wakati huo kwani mazungumzo yale yalikuwa yanaelekea ukingoni na hatua ya mwisho ingekuwa kwa RPF kuwa chama cha kisiasa ambacho kingeshiriki  kwenye uchaguzi.

Nia ya Kagame ilikuwa ni kuchukua uongozi Rwanda kwa nguvu kwa sababu kwa mizania ya siasa za nchi hiyo ambazo zimejikita zaidi kwenye ukabila ingekuwa vigumu kwa Watutsi walio wachache kushinda.

Sababu ya pili ambayo ndiyo iliyowafanya RPF wakatae au watumie nguvu ilikuwa ni juhudi ya Marekani ambayo ilikuwa mfadhili mkuu wa RPF kuhakikisha kuwa ushawishi wa Ufaransa katika eneo la Maziwa Makuu unaondoshwa kwa gharama yoyote.

Wednesday, August 7, 2013

UWANJA WA NDEGE WA JKIA ULIVYOTEKETEA



Moto mkubwa umewaka katika uwanja mkuu wa ndege wa Jomo Kenyata mjini Nairobi Kenya , na kulazimisha kufungwa na hivyo kusitishwa kwa safari za anga katika eneo la Afrika Mashariki.

Safari za mamia ya wasafiri zimevurugwa na kuachwa nje ya uwanja huo wenye shughuli nyingi zaidi Afrika mashariki . Nyingi kati ya safari za ndege zimeahirishwa huku ndege zinazoingia zikielekezwa katika uwanja wa ndege wa Mombasa.

MFANYABIASHARA MKUBWA WA MADINI NA MMILIKI WA SG HOTEL JIJINI ARUSHA AUWAWA KWA KUPIGWA RISASI


Habari zilizotufikia hivi punde Kutoka chumba chetu cha habari,zinaeleza kuwa mmoja wa Wafanyabiasha wakubwa wa Madini jijini Arusha,aliyejulikana kwa jina la Erasto Msuya na pia ni mmiliki wa SG HOTEL mkoani humo,amepigwa risasi zaidi ya sita na watu wasiojulikana na kufa papo hapo,habari zinaeleza na kubainisha zaidi kuwa Marehemu alikuwa akitokea KIA kwenda BOMA ambako alikuwa ameitwa na watu (ambao hawakujulikana mara moja) ili wakafanye biashara. 
 
Habari zaidi tuvute subra kidoogo,tutazidi kufahamishana kadiri ya taarifa zitakapokuwa zikiingia.
 
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi-Amen.

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

SERA, ITIKADI ZA VYAMA ZIKAE KANDO, KATIBA MALI YA WATANZANIA WOTE



Zanzibar.  Mabaraza ya Katiba yaliyosimamiwa na Tume ya Katiba kwa sehemu kubwa yametupa picha ya namna watu walivyokuwa wameyafikiria. Ingawa Tume ilitoa muongozo, wengi hawakuusoma au nisema hawakutaka kuelewa.

Tulichokiishuhudia ni baadhi ya wajumbe kutoka katika vyama vya siasa kushiriki katika mabaraza wakiwa na waraka mfukoni wenye maelekezo ya vyama vyao!

Ni jambo la kushangaza, lakini ndio demokrasia yenu ilipofikia kwamba watu wazima wanashindwa kujenga hoja wenyewe aina ya katiba wanaitakayo, wanasubiri kulishwa maneno kutoka kwa wanasiasa.

Ninaipongeza Tume ya Jaji Warioba kwa kuwa haikuruhusu taratibu na miongozo iliyowekwa na Tume hiyo kuvunjwa kwa makusudi, muda wote walisimama kwenye upande wa haki na pale alipozuka mtu akiwa na “waraka” wenye maelekezo alipigwa ‘stop’, ili aeleze ya kwake.

Siku chache baada ya kuanza kwa mabaraza tulimsikia Jaji Warioba akiwakosoa wajumbe wa mabaraza hayo waliokuwa wakienda  na matamko au nyaraka za vyama, badala ya maoni ya wananchi waliowachagua.

Inavyoelekea baadhi ya watu bado wana mawazo kuwa mfumo wa chama dola unaendelea katika nchi yetu na inawezekana mfumo huo umewalemaza baadhi ya watu kiasi cha kuingia woga hata katika yale mambo yenye uhusiano wa maisha ya kila siku.

Bado wanafikiri chama kushika hatamu katika wakati huu wa mfumo wa vyama vingi vya siasa. Wanasahau kuwa Katiba ni mali ya wananchi, na ni wao wenye haki na mamlaka ya kueleza wanataka namna gani nchi yao iongozwe.

Wananchi ndio wenye uamuzi wa mwisho kuamua Katiba yao iweje na wala sio watawala wala vyama vya siasa vinavyoweza kujigeuza au kupora mamlaka na nguvu za wananchi.

Kwa maana hii sera za vyama vya siasa hazina upenyo wa kwenye suala zima la Katiba Mpya maana wananchi wanaweza hata wakasema kwa mfano hawaoni ulazima wa kuwepo kwa vyama vya siasa na badala yake wakapendekeza aina nyingine ya mifumo ya kidemokrasia ambayo inakubalika.

Sisemi kuwa tuachane na vyama vingi, la hasha, isipokuwa ninachora picha kwamba nguvu ya mwisho ya uamuzi katika nchi yeyote ya kidemokrasia ni kwa wananchi wenyewe.

Tunasimama pamoja na Tume ya Jaji Warioba kwa kitendo chao cha ushupavu katika kuona Taifa letu linapata Katiba ambayo inatokana na matakwa ya wananchi badala ya wanasiasa.

Kamwe tusikubali kufanya mambo kwa ajili ya maslahi ya muda mfupi, lazima tutangulize uzalendo kwa ajili ya kupata Katiba bora inayotokana na matakwa ya watu wenyewe na sio kundi fulani.

Ni wajibu wa wajumbe wa mabaraza ya Katiba kujiepusha na makundi maslahi kwa kuwa mwisho wa siku hata wao watakuja kuona uzuri au ubaya wa Katiba waliyoiandika.

Katika hili pia sina budi kumpongeza Rais Jakaya Kikwete kwa nyakati tofauti amekuwa akisisitiza uhuru wa mawazo, kwamba kila mtu atoe mawazo yake mwenyewe bila ya woga wala wasiwasi.

Ni wajibu wake akiwa Rais wa watu wote kusimamia sheria na taratibu za nchi tulizojiwekea. Hapa Zanzibar wamejitokeza baadhi ya wajumbe wa mabaraza ya katiba wakiwa na maelekezo ya vyama vyao vya siasa, lakini tunashukuru Mungu Tume imesimama imara kuwaeleza haja ya wajumbe kuboresha Rasimu ya Katiba kwa mtazamo wao.
 
Sitaki kuamini kuwa mchakato wa Katiba tulioanza tangu mwaka jana ni kiini macho au kupoteza wakati na fedha, siamini hivyo kwa sababu suala la kuwa na Katiba mpya limepigiwa kelele siku nyingi,l akini pia tukiwa watu wazima hatuna sababu ya kudanganyana kwani Serikali ingeweza kujifungia na kuandika Katiba wanayoitaka kisha kuipeleka bungeni.

Kwa kuwa nchi yetu inaongozwa na Katiba na sheria pamoja na viongozi wenye dhamira ya dhati ya uongozi wao, hatuwezi kufanya mchezo wa aina hiyo ambao hauna faida kwao wala kwetu.

Ndio maana Rais Kikwete hakutoa matamshi ya kuwashurutisha wananchi kutoa maoni na mapendekezo yanayotakiwa na chama chake wala Serikali. Na wala serikali zote mbili –Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya  Mapinduzi Zanzibar hazikuwa na na msimamo wake katika suala la kupata Katiba mpya, wametuachia wananchi tuamue.
 
Ingekuwa Serikali ina maoni yake katika suala hili au ingetaka sera ya chama tawala ndio kiwe msingi wa kuandika Katiba mpya ingefanya hivyo na mambo kadhaa yangetokea;

Mosi, utoaji maoni ungekuwa ni wa kiini macho na kwamba Katiba hiyo isingekuwa imebeba matakwa ya wananchi bali maslahi ya watawala na kikundi fulani cha watu.

Suala la pili, hii ingedhihirisha kuwa wananchi bado lepe la usingizi halijawatoka, woga umetawala miongoni mwao na wanadhani Serikali ni mali ya watawala na kwamba mamlaka ya uendeshaji nchi haitoki kwao.

Hata hivyo, ukweli ni kuwa mamlaka ya uendeshaji nchi ni kwa wananchi wenyewe, lakini kwa kutokufahamu namna ya jinsi Serikali inavyopaswa kuendesha mambo yake au kwa sababu ya kutokujiamini kunakoambatana na utashi wa maslahi binafsi, baadhi ya watu wanaweza kuyumbishwa na wanasiasa au makundi maslahi.

Wapo wanasiasa na hata makundi maslahi yalijaribu kutaka kujipenyeza kwenye akili za wananchi, lakini hawakuweza kuwashawashi waliowengi na badala yake tumeona namna watu walivyotoa mawazo yao katika Tume ya Jaji Warioba.

Ni busara ya kawaida kwa wananchi tukaelewa kwamba vyama vyetu vya siasa havina mamlaka ya kuifanyia Katiba ya nchi mabadiliko, zile enzi za mfumo wa chama kimoja zimeshapitwa.

TENDWA AFUNGUKA BAADA YA KUSTAAFU!


Aliyekuwa Msajili wa Vyama vya Siasa Ndg. John Tendwa

Harare. Siku moja baada ya kutangazwa rasmi kwamba aliyekuwa Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa amestaafu kwa mujibu wa sheria, amejitokeza na kueleza yaliyo moyoni mwake.

Katika mahojiano maalumu na vyanzo vyetu vya habari jijini Harare jana, Tendwa alisema amepokea kwa mikono miwili kustaafu kutoka katika nafasi hiyo nyeti katika siasa za Tanzania, huku akisema anajiona mwenye bahati kufanya kazi na marais wawili katika nafasi yake.

Tendwa amefanya kazi chini ya uongozi wa Rais Mstaafu Benjamin Mkapa na baadaye Rais Jakaya Kikwete. Nafasi ya Tendwa, imechukuliwa na Jaji Francis Mutungi ambaye alikuwa jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma.

Akizungumzia kuhusu viongozi wa vyama vya upinzani kupokea kwa nderemo kustaafu kwake, Tendwa alisema wala hashangai kuyasikia hayo kwani inaonyesha kwamba kazi yake alikuwa akiifanya vyema na mujibu wa sheria.

“Unajua unapokuwa msajili na ukaona wadau wote wanakushangilia hapo ujue kuna tatizo kubwa, nimekuwa ninafanya kazi yangu vizuri sana kwa kuzingatia misingi ya sheria ambayo imewekwa kwa mujibu wa sheria na kanuni,”alisema Tendwa.

Alisema kwamba, “Unajua kuvilea vyama ni kazi kubwa sana ndugu yangu, maana kuna wakati hata Chama Cha Mapinduzi (CCM) walikuwa wanasema ninaegemea na kuvipendelea sana vyama vya upinzani. Leo nimestaafu nasikia vyama vya upinzani vinasema kwamba nilikuwa nawapendelea CCM, hiyo inaonyesha kwamba nilikuwa ninafanya kazi yangu sawa sawa.”

Kitu gani ambacho Tendwa hatakisahau?
Alisema kwamba katika miaka yake 13 ambayo amekuwa msajili hatomsahau waziri mmoja wa CCM.

Hata hivyo, vyanzo vyetu vya habari vilimbana kumtaja waziri huyo, lakini agoma kwa madai kwamba hapendi kuendeleza malumbano naye baada ya kustafu kwake utumishi wa umma.

Tendwa alisema katika utumishi wake, waziri huyo alikuwa akimpatia wakati mgumu sana kwa kumpakazia kwamba yeye ni mpinzani.

“Katika miaka yangu 13 ofisini sitaweza kumsahau huyo waziri maana alikuwa ananipakazia kwamba mimi ni mfuasi wa vyama vya upinzani. Ninamshukuru Mungu kwamba baadaye alikuja kuniomba msamaha, lakini ilikuwa imenisumbua sana katika kazi zangu,” alisema huku akionyesha masikitiko

Kwa nini vyama vinashuka?
Kuhusu kushuka na kupanda kwa vyama vya siasa hasa vile vya upinzani nchini baada ya uchaguzi kumalizika, Tendwa alisema katika kipindi chake cha uongozi aligundua kuwa migogoro ndani ya vyama hivyo ndio chanzo kikubwa cha kupoteza mvuto kwa wananchi.

“Tatizo la vyama vingi vya upinzani Tanzania vinadhani kuwapata wabunge basi ndio vinakuwa vimechukua Serikali, vinasahau kujizatiti na kujipambanua mbele ya macho ya wapigakura kuwa vinasimamia kitu gani, badala yake nimekuwa vikiishia kwenye migogoro isiyo ya lazima,” alisema Tendwa.

Tendwa alielezea jinsi ambavyo NCCR-Mageuzi ilivyokuwa na nguvu sana katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1995, lakini baada ya kuingia kwenye migogoro chama hicho kikapoteza mvuto.

“Badala ya kujiingiza kwenye migogoro vinatakiwa kujipanga kisayansi, lazima wajue kwamba siasa ni sanyasi,” alisema.

Alisema hata CUF kilianza kupoteza mvuto kwa jamii baada ya kupata wabunge na kuanza kuibuka migogoro ya ndani.