To Chat with me click here

Wednesday, May 13, 2015

RAIS NKURUNZINZA APINDULIWA!!




Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi, aliyepinduliwa hivi punde toka madarakani
akiwa mazungumzoni nchini Tanzania.
Meja Jenerali Godefroid Niyombareh amewaambia waandishi wa habari mjini Bujumubura, kuwa kumeundwa kamati maalum ya kuiokoa Burundi itakayotawala taifa hilo kwa kipindi cha mpwito.

Kulingana na taarifa iliyopeperushwa na redio Isanganiro, serikali ya Nkurunziza imeon'golewa madarakani.

Meja Generali Niyombareh amesema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa rais huyo kugombea kwa  awamu ya tatu.

Jenerali huyo alitimuliwa na Nkurunziza mwezi februari anasema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa.

Kwa sasa rais Nkurunziza yuko nchini Tanzania alipokuwa anatarajiwa kujumuika na viongozi wa kanda hii ya Afrika Mashriki kutafuta suluhu ya mgogoro wa Burundi tangu Nkurunzinza atangaze nia yake ya kuwania awamu ya tatu.


Raia wa Bujumbura wakishanilia tangazo la generali Niyombareh
  


    
Maafisa wa jeshi la Burundi wanaonekana wakiweka usalama mitaani
katikati ya Jiji la Bunjumbura
Polisi wa Bunjumbura wakiwa wamembeba mwenzao aliyeumizwa katika purukushani hizo, baada ya kuamliwa na Jeshi kutoka mitaani.
Raia wanashangilia mjini Bujumbura
Waandamanaji Bujumbura




No comments:

Post a Comment