To Chat with me click here

Monday, June 10, 2013

KANYE CELEBRATES HIS BIRTHDAY IN NYC — WITHOUT KIM




Kanye West

It was a happy birthday indeed for Kanye West, who celebrated turning 36 with a star-studded party on Saturday night in New York City. One face that was notably absent from the festivities, however? Oh, just the mother of his unborn child.

That's right, West, who was in town in advance of his performance at the Governors Ball music festival on Sunday, left his (extremely) pregnant girlfriend, Kim Kardashian, at home — back in Los Angeles. Throughout her pregnancy the couple has often been apart, which we spotlighted here, with Kanye recording an album in France and Kim back in L.A. with her reality TV family. However, he did attend her baby shower, arriving with a hooded sweatshirt pulled over his head.

While Kim sent Twitter messages of love and devotion to her man, West partied at the Caribbean-themed hot spot Miss Lily's with Kim's bestie Jonathan Cheban, Scott Disick, Nas, Jay-Z, and BeyoncĂ© (who took the opportunity to further combat pregnancy rumors by sporting a sexy midriff-baring top that flashed her flat, toned abs).

As the A-list crew (presumably) ate, drank, and enjoyed being merry, Kim tweeted, "Happy Birthday to my best friend, the love of my life, my soul!!!! I love you beyond words!"

Happy Birthday to my best friend, the of my life, my soul!!!! I love you beyond words! instagram.com/p/aTgfI-OS-a/—Kim Kardashian (@KimKardashian) June 8, 2013
 
For added emphasis, she included a very crafty photo collage of some of their most lovey-dovey shots (see below).

As for West, he seemed to keep his soiree relatively low-key. The snaps from the evening show everyone looking relaxed and happy. Well, except for the fact that deep down they must all have been missing Kim … right?

Granted, the brunette beauty is too far along in her pregnancy to be allowed to fly, but then why not have a party in the good ol' City of Angels? Though Kim didn’t seem put off by being excluded, something tells us she would have preferred to spend the night by West's side.

Good thing there's always next year!

Tuesday, June 4, 2013

MADHARA YA PROPAGANDA CHAFU ZA UDINI UCHAGUZI MKUU MWAKA 2010



Dar es Salaam,Tanzania

Rais wa Tanzania, Ndg. Jakaya Mrisho Kikwete.
SAKATA la Video inayodaiwa kuwa ilitoboa siri ya Rais Kikwete kutinga Ikulu kwa msaada wa kura za Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF) Profesa Ibrahim Lipumba, imeendelea kukigawa chama hicho baada ya Naibu Katibu Mkuu Chama hicho Tanzania Bara, Julius Mtatiro kukataa kuzungumzia video hiyo, alikataa katakata na kuwashauri waandishi wawasiliane na Profesa Lipumba amabye pia aliwahi kukataa kuzungumzia video hiyo.

Itakumbukwa kuwa kumekuwepo tuhuma dhidi ya Rais Kikwete na CCM kuwa mwaka 2010 waliendesha propaganda chafu za udini zenye lengo la kuwagawa Watanzania hususan Wakristo na Waislamu kwa manufaa yao ya kisiasa.

Mwelekeo huo wa kisiasa wa Rais Kikwete na CCM unadaiwa kutokana na hatua ya viongozi wa Kanisa Katoliki nchini kupitia Idara ya Uchungaji kutoa waraka maalumu uliowataka Watanzania kuchagua viongozi waadilifu.

Waraka huo haukuifurahisha CCM, ambayo imekuwa inagubikwa na tuhuma nyingi za ufisadi. Makada na viongozi wa CCM walijaribu kuupinga kwa kuupotosha, wakisema unaingiza mambo ya dini katika siasa.

Kanisa Katoliki lina utaratibu wa muda mrefu wa kutoka nyaraka kuelekeza waamini na wananchi juu ya mambo ya msingi katika jamii.

Katika hali hiyo, Rais Kikwete na CCM wanadaiwa kukimbilia kwa viongozi wa Kiislamu na kuwaomba wawaunge mkono kwa kuwajaza maneno ya uongo, kwamba Wakatoliki walikuwa wamewaagiza waumini wao kupigia kura wagombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Inadaiwa waliwafitinisha zaidi kwa kuwaeleza kuwa aliyekuwa mgombea kiti cha rais wa CHADEMA katika uchaguzi huo, Dk. Willibrod Slaa ambaye ameshawahi kuwa Padri, alikuwa ametumwa na Kanisa Katoliki ili kuendeleza utawala wa Kikristo nchini.

Propaganda hizo hazikuishia kwa viongozi na waumini wa Kiislamu tu, bali zilielekezwa pia kwa viongozi na wafuasi wa CUF ambao walirubuniwa na kushawishiwa kumpigia kura “Muislamu mwenzao” Rais Kikwete, huku wakiahidiwa kuwa mwaka 2015 Waislamu wa CCM nao watampigia kura mgombea wa CUF kwa hoja kuwa CCM watakuwa wamesimamisha mgombea Mkristo. Licha ya madai hayo ya udini kuwa wazi kwa muda mrefu, lakini wakati wote Rais Kikwete na CCM wamekuwa wakikanusha tuhuma hizo na kuziita kuwa uongo na uzushi.

KAWAMBWA KITANZINI LEO, BAJETI YAKE HATARINI KUPITISHWA



Dodoma,Tanzania

Waziri wa Elimu na Mfunzo ya Ufundi,Dk Shukuru Kawambwa
WAKATI Watanzania wakijiandaa kufuatilia hotuba ya Bajeti ya Wizara ya  Mafunzo ya Ufundi leo Waziri wa Wizara hiyo, Dk Shukuru Kawambwa anatarajia kukutana na upinzani mkali, kutoka kwa wabunge wa pande zote mbili yaani Upande wa Upinzani na Wapunge wa CCM.

Habari zilizonaswa na Vyanzo vyetu vya habari zinadai kwamba, Wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wamejipanga kukwamisha hotuba ya Wizara hiyo, kwa madai kwamba Waziri huyo ameshindwa kusimamia sekta ya Elimu.

Vyanzo vya habari kutoka ndani ya CCM mjini Dodoma zinadai kwamba, Wabunge hao wamepania kukwamisha hotuba hiyo na kumtaka Waziri huyo ajiuzuru ili kukisafisha Chama hicho kutokana na aibu ya mkanganyiko wa kufeli kwa Wanafunzi mwaka huu.

"Hotuba ya Wizara ya Eilimu haiwezi kupitishwa kirahisi kama Kawambwa hata jiuzuru, hatuwezi kuendelea kuwa na mawaziri wanaoshindwa kuwajibika ipasavyo katika setka zao, kitendo cha mawaziri hao kushindwa kuwajibika ipasavyo ndiyo inayochangia kuharibu Chama"kilisema chanzo hicho kwa masharti ya kutotajwa majina yake na kuongeza:

"Huu mpango unaendelea kusukwa na wabunge wa CCM waliopania kurudisha heshma ya Chama, lakizima tuanzie ndani kuwajibishana wenywe kabla ya wapinzani kuanza, kwani tukishindwa sisi watatumia udhaifu wetu kuwashawishi wananchi na hatimaye watazidi kuichukia Serikali". Wakati Waziri Dk Kawambwa akiandaliwa mazingira ya kung'olewa, Necta inatarajia kutangaza matokeo yaliyoongeza kiwango  cha  ufaulu kufikia asilimia kati ya 54 na 57, wiki hii pamoja na yale ya kidato cha sita ambayo pia yamechelewa kutangazwa.