To Chat with me click here

Friday, June 20, 2014

MAJINA YA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO HAYA HAPA!



Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) imetangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano kwa mwaka 2014 ambao waliomaliza kidato cha nne mwaka 2013

Wanafunzi waliochaguliwa wanatakiwa kuripoti kwenye shule walizopangiwa kuanzia tarehe 10 Julai 2014 na mwisho wa kuripoti ni tarehe 30 Julai 2014. 

Aidha, hakutakuwa na mabadiliko ya wanafunzi kubadilishiwa shule walizopangiwa, hivyo wanafunzi wote wanatakiwa kuripoti katika shule walizopangiwa kama inavyoonekana katika matokeo haya.



MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO MWAKA 2014

 






Maxmillian Kattikiro Blog  inapenda kuwapongeza wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano na sita kwa mwaka 2014. Pia tunapenda kuwatia moyo wale wote ambao hawakuchaguliwa kuwa, wasikate tama, bado wanayo nafasi nzuri ya kurekebisha pale ambapo walitereza, na vilevile watambue kuwa elimu haina mwisho.
 

No comments:

Post a Comment