To Chat with me click here

Wednesday, June 18, 2014

POLISI AFANYA SIASA ZA CCM




ASKARI Polisi, Mwashibanda Shibanda wa Wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma, anadaiwa kujihusisha na siasa za Chama Cha Mapinduzi (CCM), suala ambalo ni kinyume na taratibu za jeshi.

Kwa sasa Mwashibanda anasoma katika Chuo Kikuu cha Mzumbe, mkoani Morogoro, na katika kipindi chote anadaiwa kufanya shughuli za kisiasa za wazi.
Mwashibanda amepata kuwa mwenyekiti wa tawi maalumu la CCM Mzumbe, na mwenyekiti wa shirikisho la matawi ya CCM mkoani Morogoro mwaka 2012 – 2013.

Mtoa taarifa wetu amedokeza kuwa akiwa chuoni, anadaiwa kuwakamata wanachuo wenzake kwa kushirikiana na polisi wa kituo cha Mzumbe, hasa wale wenye mirengo tofauti na CCM.

Kwa mujibu wa kumbukumbu mbalimbali za picha ambazo gazeti hili limeziona, askari huyo anaonekana akiwa amevalia sare za CCM zenye rangi za njano na kijani akiwa na makada na viongozi tofauti wa kitaifa.

Askari huyo amewahi kuwa mkimbiza mwenge wa uhuru mwaka 2010 na akiwa mkoani Shinyanga, alikaririwa akimpigia kampeni aliyekuwa mgombea urais wa CCM, Jakaya Kikwete.  Mwashibanda anatajwa kuzitia dosari mbio za mwenge baada ya kuonyesha wazi kuipigia kampeni CCM wakati huo.

Kwa mujibu wa vyanzo vyetu, askari huyo alifanya kituko hicho katika Kijiji cha Wigelekelo, Shinyanga Vijijini wakati wa makabidhiano ya mwenge huo ukitokea Manispaa ya Shinyanga.

Alisema wilaya hiyo ni ya kihistoria, lakini imekuwa ikichanganywa na wanasiasa wanaotangatanga kama kumbikumbi wasiokuwa na makazi.

“Watu wa Maswa mtaonekana kuwa mmepotoka iwapo itaonekana mnampatia uongozi mtu aliyejiunga na kanisa jipya, kwani huyo ana tamaa ya uongozi, hakuna aliyezaliwa duniani kuwa kiongozi hadi kufa bali ni kuachiana zamu, sasa ni zamu ya mwingine,” alisema.

Kauli hiyo, ilionyesha wazi kumlenga Mbunge wa Maswa Magharibi, John Shibuda, aliyejiondoa CCM na kuhamia CHADEMA baada ya kushindwa katika kura za maoni.

Hili sio tukio la kwanza kwa askari kufanya siasa za wazi za CCM kwani katika mkutano mkuu wa nane wa uchaguzi wa Umoja wa Vijana (UVCCM) Oktoba mwaka 2012 , mmoja wa wagombea wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC), Stanley Mdoe, alitiwa mbaroni na polisi akibainika kuwa askari wa jeshi hilo.

Askari huyo mwenye namba F 7961 wa cheo cha konstebo, alitoka Kituo cha Polisi Mvomero, Morogoro.

No comments:

Post a Comment