To Chat with me click here

Sunday, June 1, 2014

TANZIA: MAMA MZAZI WA ZITTO KABWE AFARIKI DUNIA!


Mhe. Zitto akiwa na mama yake mzazi B. Shida Salum enzi za uhai wake,kabla mauti kumkuta leo asubuhi katika hospitali ya AMI iliyopo Masaki,, jijini Dar Es Salaam.

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Walemavu Tanzania (CHAWATA), Bi Shida Salum, na Mjumbe wa kamati Kuu ya chama cha CHADEMA, aliyekuwa amelazwa chumba cha Wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalum (ICU), katika Hospitali ya AMI, Masaki jijini Dar, ameaga Dunia.



Kwa habari zilizotufikia katika vyombo vyetu vya habari, vimesema kuwa, mama wa Zitto alifariki leo asubuhi katika hospitali hiyo ya AMI baada ya kulazwa hapo kwa muda ambapo alikuwa akisumbuliwa na ungonjwa wa KANSA mpaka mauti ilipomkuta asubuhi ya leo. Bi. Shida Salum, mbali na kuwa amekuwa akitibiwa AMI  mpaka umauti ulipomkuta, lakini vilevile amneshawahi kwenda kutibiwa ng’ambo ya nchi kama vile India bila mafaniko. 


Habari hizi za kufariki kwa mama yake Zitto zilielezwa na Zitto Kabwe mwenyewe kupitia mtandao wake wa twitter, akiripoti kuondokewa na mzazi wake huyo.

Watu na baathi ya viongozi mbalimbali wametoa salamu zao za rambi rambi kwa Mhe. Zitto kama ifuatavyo:-


Bernard Membe:
Zitto Kabwe pole sana kwako na ndugu kwa msiba huu mzito. Tunawaombea subira na Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi, Amina. 

William Ngereja:           
Nimepokea taarifa za msiba wa Bi. Shida Salum (mama mzazi wa Zitto Zuberi Kabwe) kwa masiitiko makubwa. Nawapa pole familia nzima ya ndugu yetu Zitto katika kipindi hiki cha majonzi, Mwenyezi Mungu awape wepesi na pia, natoa pole kwa wote walioguswa na msiba wa George Otieno aliyefariki jana, tuendelee kuziombea familia hizi na nyingine zenye misiba ili wapate faraja kutoka kwa Mwenyezi Mungu ambaye ndiye mfariji mkuu. 

Maxmillian Kattikiro (TEDA):
Napenda kuungana na wengine wote walionitangulia kutoa salamu za pole kwa ndugu, rafiki, jamaa, kamanda na mpambanaji mwenzutu, Mhe. Zitto Ruyagwa Kabwe pamoja na CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA), kwa kuondokewa na Mama yake mzazi Bi. Shida Salum, na mjumbe wa Kamati Kuu CHADEMA. Katika wakati huu mgumu na majonzi, tunakuombea ili Mungu aendelee kukutia nguvu na kukuongoza vyema. Tunaungana nawe katika kuomboleza msiba huu na Mwenyezi Mungu ampumzishe kwa amani mama yetu, Amina.

David Kafulila:
Nimepokea kwa huzuni kubwa msiba wa mama yetu Bi Shida Salum. Ni mama mzazi wa zitto. Alinipenda sana na nilikuwa karibu nae sana wakati wa uhai wake. Aliugua kwa muda kansa. Akapata matibabu india kwa muda bila mafanikio sana na akaendelea kupata matibabu akiwa Dar kupitia hospitali bora kabisa ya AMI. Nitambuka kwa ukaribu wangu kwake. Alipenda kuwa karibu na mimi. Alikaa namimi mpaka usiku mwingi wa sanane tunazungumza.alikuwa mama mcheshi, mwenye upeo na mwenye kufikiri kimkakati siku zote. Alipenda kufunga na kusali. Nimepoteza kitu kikubwa kwa mama yetu huyu. Mapenzi alokuwa nayo kwa watu wote. Naamini ametangulia kwa Mungu wa upendo. Na hakika tutamkuta tufurahi nae pamoja siku moja.

Halima Mdee:
Pole sana mh. Zitto kabwe, kwa kufiwa na mama yako mzazi Shida Salum,
Najua hilo ni pigo kubwa katika maisha yako , lakini mungu amempenda zaidi, nakuomba uwe na moyo wa uvumilivu katika kipindi hiki kigumu, yote ni mipango ya Mungu, cha msingi ni kumuombea ili Mungu, aweze kumpokea mahari pema peponi amin. R.I.P Shida Salum.

No comments:

Post a Comment