To Chat with me click here

Thursday, March 14, 2013

POLISI WATANO KIZIMBANI WIZI WA SH. MILIONI 150

Baadhi ya askari polisi wanaotuhumiwa kuiba Sh. milioni 150 baada ya kuziokoa katika tukio la ujambazi eneo la Kariakoo jijini Dar es Salaam wakifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi
Askari watano wa Jeshi la Polisi wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, wakikabiliwa na shtaka la wizi wa Sh. milioni 150.

Washtakiwa hao walikwenda kuzuia tukuo la ujambazi wa kupora katika duka moja eneo la Kariakoo, lakini wakatuhumiwa kuiba fedha zilizoporwa na majambazi hao kisha kuzidondosha.

Washitakiwa hao walisomewa mashtaka yao jana mbele ya Hakimu Mkazi,  Emmilius Mchauru.

Washtakiwa hao ni Stafu sajenti D. 8845 Dancan Mwasabila (43),  Koplo E.9288  Geofrey (39), Koplo E. 5585  Rajabu Nkumkwa (46), Koplo E.29249 Kawanani  Humphrey (34)  na Koplo E. 5548 Kelvin Mohamed(44).

Wakili wa Serikali Mwandamizi, Bernad Kongola, alidai kuwa Desemba 18, 2012 katika eneo la Kariakoo Wilaya ya Ilala, jijini Dar es Salaam, washtakiwa hao kwa pamoja waliiba fedha taslimu Sh. milioni 150, mali ya Mire Artan Ismail.

Washtakiwa wote walikana shtaka hilo na upande wa mashtaka ulidai kuwa upelelezi bado haujakamilika na haukuwa na pingamizi ya dhamana dhidi yao.

Hakimu Mchauru alisema washtakiwa wanatakiwa kusaini hati ya dhamana ya  Sh. milioni tano, kuwasilisha fedha taslimu Sh. miloin 15 au hati ya mali isiyohamishika yenye thamani hiyo ya fedha.

Mbali na masharti hayo ya dhamana, pia kila mshtakiwa alitakiwa  kuwa na wadhamini wawili wanaoaminika  ambao kila mmoja wao angesaini bondi ya Sh. milioni tano.

Hata hivyo, mshtakiwa wa kwanza hadi wane walitimiza masharti hayo na mshtakiwa wa tano amekwenda mahabusu hadi Machi 27, mwaka huu itakapotajwa tena.

KIBANDA AANZA KUSIMAMA


Tanzania Editors Forum Absalom Kibanda.
MHARIRI Mtendaji wa Kampuni ya New Habari (2006), Absalom Kibanda, ameanza mazoezi ya kusimama. Kibanda amelazwa katika Hospitali ya Millpark iliyoko Johannesbaurg, Afrika Kusini baada ya kuteswa la kujeruhiwa vibaya wiki iliyopita.

Taarifa ya Katibu wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Neville Meena, Dar es Salaam jana, ilisema kwa ujumla afya ya Kbanda inaendelea kuimarika na madaktari na wauguzi katika hosipitali hiyo wameendelea kumuhudumia kwa karibu.

“Nafuu aliyoipata imemwezesha kuanza mazoezi ya kusimama na kutembea ndani ya chumba alimolazwa. Madaktari wanaomtibu wamesema wanafanya hivyo kuwezesha mwili wake kupata nguvu na kuujengea uwezo wa kujitegemea,” ilisema taarifa hiyo.

Kwa mujibu wa Meena, baada ya siku mbili au tatu kadri hali halisi itakavyokuwa, madaktari wanatarajia kuanza mazoezi ya kumtembeza nje ya chumba chake katika jitihada hizohizo za kuuwezesha mwili wake kupata nguvu.

Wakati huo huo, Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Mtwara (MTPC) imesema imepokea kwa masikitiko taarifa za kuvamiwa, kupigwa na kuteswa kwa Kibanda.

Katika taarifa yake jana, MTPC ilisema inampa pole Kibanda kwa tukio hilo na inamuombea kwa Mungu apone haraka majeraha aliyoyapata arejee kazini kuendelea na shughuli za upashanaji habari.

“Klabu unaungana na wadau wengine wa habari nchini kulaani vikali tukio hilo na mengine yanayohusisha utesaji wa wanahabari na inalitaka jeshi la polisi kuharakisha uchunguzi wahuska wakamatwe na wafikishwe mbele ya vyombo vya husika sheria ichukue mkondo wake.

“Sisi wanahabari wa Mtwara tunalichukulia tukio hilo kama njama za watu wachache za kutaka kufifisha taaluma na uhuru wa habari nchini kwa kubana wigo wa upashanaji habari za kweli na zenye maslahi kwa Watanzania,” ilisema taarifa hiyo.

CHADEMA YALISULUBU BUNGE

WANASHERIA wameunga mkono msimamo wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na wale wa NCCR- Mageuzi kupinga hatua ya Ofisi ya Bunge kuliagiza Jeshi la Polisi kuwakamata wabunge wake ili wakahojiwe.

Wakizungumza na Tanzania Daima, mwanasheria mashuhuri hapa nchini na wakili wa kujitegemea, Mathew Kakamba, alisema ni kinyume cha sheria na ni matumizi mabaya ya madaraka kwa Ofisi ya Bunge kutumia polisi kuwakamata wabunge katika masuala yanayolihusu Bunge.

Wanasheria hao walitoa maoni yao kuhusiana na mvutano mkubwa wa kisheria uliozuka baina ya CHADEMA na Ofisi ya Bunge ambayo imeagiza kukamatwa kwa wabunge kadhaa wa upinzani ili wakahojiwe na Kamati ya Haki, Kinga na Maadili ya Bunge, ambayo CHADEMA wanadai kuwa haipo.
Wakili Kakamba katika maoni yake alisema ni makosa kisheria kutumia nguvu za mhimili mwingine katika kuendesha masuala yanayohusu mhimili wa pili.

“Kuna mgogoro unaojulikana kwa  Watanzania karibu wote kuhusiana na vurugu zilizotokea katika mkutano wa Bunge lililokwisha, na kuvunjwa kwa kamati za kudumu za Bunge.

“Pamoja na kuvunjwa kwa kamati hizo, bado kama sikosei, wajumbe wake hawajateuliwa na kwa maana hiyo, kisheria utendaji wake haujaanza. Kwa lugha nyingine, haziwezi kuitwa kamati rasmi kwa sababu hazina wajumbe,” alisema Wakili Kakamba.

Kauli ya Wakili Kakamba imeungwa mkono na wakili mwingine, Aloyce Komba, ambaye  amekiita kitendo cha Ofisi ya Bunge kutumia polisi kuwakamata wabunge wao wa upinzani kuwa ni udhalilishaji mkubwa na uvunjaji wa haki za binadamu.

Komba anayetoka Kampuni ya Uwakili ya Haki Kwanza, alisema Bunge ni chombo kinachojitegemea na linazo sheria na kanuni zinazopaswa kutumika kumlazimisha mbunge kutimiza agizo la wito.
“Masuala yote ya Bunge yanatakiwa kuendeshwa kibunge bila kutegemea vyombo vingine vya nje, labda tu ikiwa kuna mwingiliano kutoka katika mhimili mwingine. “Si sahihi kwa spika kutumia polisi kuwakamata wabunge wakati wanazo kanuni na taratibu nzuri tu, na sidhani kama ni utaratibu mzuri na unaolenga kudumisha demokrasia.
“Mbunge akishindwa kufika, kwani hakuna sheria nyingine hata za kuzuiwa kuhudhuria vikao kadhaa vya Bunge, hadi leo wanataka kutumia polisi kuwakamata?” alihoji Komba.

Akizungumzia uhalali wa kamati hizo, Komba ambaye ni mtaalamu wa sheria katika mambo ya utawala, alisema kimsingi hazipo, kwa sababu tangu kuvunjwa kwake na kuundwa nyingine, bado spika hajateua wajumbe wa kamati mpya.

“Hajateua wajumbe wa kamati hizo, na ni sawa kabisa kuwa hazipo. Sasa wanaitwa kuhojiwa na kamati gani? Mtazamo wa kisheria ni kwamba hazipo.
Alikwenda mbali zaidi na kuilaumu Ofisi ya Bunge kwa madai ya kuvunja haki za msingi kwa sababu aliyetendewa kosa ni spika (kiti), anayelalamika ni spika, mteuzi wa kamati ni spika na ushahidi mwingi utatoka kwa spika, hivyo kupingana kabisa na haki za sheria ambazo mlalamikaji hapaswi tena kuwa mwendesha mashitaka.

Hata hivyo, mawakili hao walikubaliana na kuwataka wabunge wote waliopata barua za wito kutoka Ofisi ya Bunge kuitikia na si kukaidi. “Pamoja na kasoro hizo, kama wameitwa na Ofisi ya Bunge, wanatakiwa kwenda na si kugoma. Huko ndiko mahali pekee wanakotakiwa kuwakosoa hao wakubwa, na hata wanao uwezo wa kukataa kuzungumza hata kama kamati yenyewe ingekuwa hai kisheria,” walisema wanasheria hao.

CHADEMA wagoma
Juzi  Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa alimwagiza Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani Bungeni kuiandikia barua Ofisi ya Bunge ya kukataa wabunge wake kukamatwa na polisi ama kuhojiwa na kamati waliyodai ni hewa, kwa kuwa zilizokuwapo zilivunjwa na Spika Anne Makinda katika kikao kilichoisha mwezi uliopita.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Dk. Slaa alisema kisheria, kanuni na taratibu za Bunge, kamati ambazo zimeshavunjwa haziwezi kufanya kazi yoyote kwa kuwa ni batili mpaka hapo zitakapoundwa kamati nyingine.
Alilitaka Bunge kurejea kanuni za kudumu za Bunge namba 113 (7), inayozungumzia ukomo wa uhai wa kamati za Bunge, uhai wake unaishia Mkutano wa Kumi wa Bunge ambapo inakuwa ni nusu ya kwanza ya uhai wa Bunge lenyewe.

Dk. Slaa alisema kutokana na kifungu hicho, inaonesha dhahiri kwamba Spika Anne Makinda na wasaidizi wake wana matumizi mabaya ya sheria, kutoifahamu vizuri ama kulewa madaraka, hali ambayo CHADEMA haitakubaliana nao.

LWAKATARE AKAMATWA


JESHI la Polisi nchini limemkamata Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Wilfred Lwakatare, kwa tuhuma za kuhusika na matukio ya mashambulizi dhidi ya watu hapa nchini.

Taarifa kutoka Ofisi za Makao Makuu ya CHADEMA Kinondoni jijini Dar es Salaam zilieleza kwamba Lwakatare alikamatwa saa 7 mchana na watu wanne waliojitambulisha kama maofisa wa Jeshi la Polisi ambao walifika na gari aina ya Toyota Land Cruiser jeupe lenye namba za usajili T 140 BLA likiwa na chata ya kitalii.

Msemaji wa Jeshi la Polisi, Advera Senso, alisema Lwakatare amekamatwa kwa tuhuma zilizosambazwa kwenye mtandao. Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA Zanzibar, Hamad Yusufu Musa, ambaye alishuhudia tukio la kukamatwa kwake, aliliambia Tanzania Daima kuwa kiongozi huyo anatuhumiwa kupanga njama za matukio ya kushambulia raia yaliyotokea hapa nchini.

Hata hivyo Musa hakusema ni matukio gani yanayomhusisha kigogo huyo, lakini mtu aliyesambaza mkanda wa video katika mitandao ya kijamii jana aliandika chini yake maneno yasemayo: ‘Mikakati ya mateso ya Kibanda na mwandishi mwandamizi wa gazeti la Mwananchi, mhusika mkuu huyu hapa.’ akimaanisha Lwakatare.

Akizungumza na Tanzania Daima jana, Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa, alisema kukamatwa kwa Lwakatare na kuhusishwa na matendo hayo ya utekaji na kushambulia watu, kumedhihirisha kuwapo kwa njama chafu zenye lengo la kukichafua chama hicho mbele ya jamii.

Dk. Slaa alisema njama hizo zinaratibiwa na kigogo mmoja serikalini ambaye analitumia Jeshi la Polisi na vyombo vingine vya dola kuidhoofisha CHADEMA.

“Ikiwa ni kweli wanamshikilia kutokana na hiyo video, ni furaha kwetu, kwa sababu ukombozi wa nchi umekaribia,” alisema bila kufafanua.
Hata hivyo Dk. Slaa alisema ameshangazwa na uharaka wa polisi wa kumkamata Lwakatare siku moja tu baada ya video hiyo kuwekwa mtandaoni, na kuacha hata kumhoji mmoja wa mawaziri aliyetajwa na baadhi ya magazeti jana akihusishwa kutekwa na kuteswa kwa Kibanda.

“Waziri hajakamatwa wala kuhojiwa, alitekwa Ulimboka akamtaja ofisa wa Ikulu, lakini hajakamatwa wala kuitishwa gwaride la utambulisho. “Aliuawa kinyama Mwangosi (Daudi Mwangosi), katikati ya kundi la maofisa wa polisi na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa, lakini hakuna aliyechukuliwa hatua. Lakini kwa video ambayo haijulikani asili yake, polisi wameharakisha kumkamata na kumpekua nyumbani kwake, kulikoni?” alihoji Dk. Slaa.

Alisema ni wazi kwamba sasa lazima Watanzania wafumbue macho na wajue ukweli ulivyo na namna polisi wanavyotumika kuiangamiza CHADEMA, lakini akadai kuwa ukweli utajulikana muda si mrefu. Wakili wa Lwakatare, Nyaronyo Kicheere, akizungumza, alisema mteja wake majira ya saa 10 alikwenda kupekuliwa nyumbani kwake Kimara.

“Kwa sasa tumeshafika nyumbani kwa Lwakatare Kimara King’ong’o na maofisa wapatao saba wanaendelea na upekuzi katika nyumba yake,” alisema mwanasheria huyo.

POPE FRANCIS I ELECTED AS 266TH ROMAN CATHOLIC PONTIFF


Cardinal Jorge Bergoglio takes name of Francis after accepting his election as 266th head of Roman Catholic Church

The cardinals of the Roman Catholic church on Wednesday chose as their new pope a man from almost "the end of the world" – the first non-European to be elected for almost 1,300 years and the first-ever member of the Jesuit order.

Jorge Mario Bergoglio, the archbishop of Buenos Aires, becomes Pope Francis – the first pontiff to take that name – an early indication perhaps of a reign he hopes will be marked by inspirational preaching and evangelization.

But the cardinals' choice risked running into immediate controversy over the new pope's role in Argentina's troubled history. In his book, El Silencio, a prominent Argentinian journalist alleged that he connived in the abduction of two Jesuit priests by the military junta in the so-called "dirty war". He denies the accusation.

The new pope appeared on the balcony over the entrance to St Peter's basilica more than an hour after white smoke poured from the chimney above the Sistine Chapel, signalling that the cardinals had made their choice. Dressed in his new white robes, the bespectacled Argentinian prelate looked pensive and perhaps a little intimidated as he looked out at the sea of jubilant humanity in the square.

The former Cardinal Bergoglio was not among the front-runners. But he obtained more votes than any other candidate except former pope Benedict in the 2005 conclave, and – although his election came as a surprise – he was certainly not a rank outsider.

According to some accounts, he was not chosen eight years ago because he begged his fellow cardinals not to continue voting for him. As he uttered his first words – "buona sera" – and the cheering died away, he told the crowd that his peers had been tasked with finding a bishop of Rome. "And it seems that they went almost to the end of the world to find him. But we're here," he said with a smile.

After a prayer for his predecessor, Benedict XVI, the new pope invited the faithful in the square to "pray for the entire world". He added: "I hope that this path for the church will be one fruitful for evangelization."

Faced with a sharp choice between those cardinals who wanted a thorough shake-up of the Vatican and those who did not, it appeared the electors in the Sistine Chapel opted for compromise. Bergoglio has a reputation for both political canniness and reforming drive. Among the tests facing the 76-year-old will be the awesome managerial demands of the job.

The fumata bianca – the white smoke signal that marks the successful conclusion of a conclave – arrived after five ballots at the end of the second day of voting. The smoke that poured out of the comignolo, the copper and steel tube on the roof of the Sistine Chapel, was greeted with cries of delight and applause from the crowd below. Soon after, the bells of St Peter's rang out, confirming that a new pope had taken over the spiritual leadership of the world's 1.2 billion baptised Catholics.

Inside the Sistine Chapel after the final vote was cast, the most junior of the cardinals, James Harvey, a former prefect of the papal household, called in the secretary of the college of cardinals, Monsignor Lorenzo Baldisseri, and the master of papal liturgical ceremonies, Monsignor Guido Marini, to witness the new pope's acceptance of one of the most daunting jobs on Earth.

The most senior of the electors, Cardinal Giovanni Battista Re, approached the pope-to-be and – in accordance with tradition – asked him in Latin: "Do you accept your canonical election as supreme pontiff?"

Having obtained his consent, he will have asked: "By what name do you wish to be called?" The master of ceremonies, acting as a notary, will then have summoned two of his staff to act as witnesses, and prepared the document that certifies the new pope's acceptance.