To Chat with me click here

Wednesday, July 24, 2013

SHIRIKA LA MSALABA MWEKUNDU TANZANIA KUGAWA VYANDARUA 68,000 KWA WAKIMBIZI




Shirika la Msalaba Mwekundu nchini Tanzania (TRCS) litasambaza vyandarua 68,000 vilivyowekwa dawa ya kuua mbu kwa wakimbizi wanaoishi kwenye kambi ya Nyarugusu mkoani Kigoma.

Shirikisho la Kimataifa la Msalaba Mwekundu na Mwezi Mwekundu linafadhili usambazaji huo, ambao utaanza tarehe 30 Julai kwa kushirikiana na kampeni ya Wakfu wa Umoja wa Mataifa ya "Si Chochote ila Vyandarua tu" na mashirika washirika ya misaada.

"Malaria ni ugonjwa pekee inaouwa watu wengi kabisa kwenye kambi hii ya wakimbizi, yakiwaathiri zaidi wanawake wajawazito na watoto walio chini ya umri wa miaka mitano," alisema Rais wa TRCS, George Nangale.

Zaidi ya matukio 11,000 yalirikodiwa kwenye kambi hiyo kati ya mwezi Januari na Aprili mwaka huu, na malaria ni sababu ya asilimia 60 ya matibabu ya kiafya, alisema.

Wengi wa wakimbizi kwenye kambi ya Nyarugusu wanatoka Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Monday, July 22, 2013

MIILI YA WANAJESHI WALIOUAWA DARFUR KUAGWA LEO




Miili ya askari saba wa Jeshi la  Wananchi wa Tanzania (JWTZ) waliouawa kwa kupigwa risasi katika Jimbo la Darfur, nchini Sudan, wakiwa kwenye operesheni za Jeshi la Kulinda Amani la Umoja wa Mataifa (Unamid), itaagwa leo katika viwanja vya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), vilivyoko Upanga, jijini Dar es Salaam.

Miili hiyo ya Sajini Shaibu Othman, Koplo Oswald Chaula, Koplo Mohamed Ally, Koplo Mohamed Chikilizo, Private Rodney Ndunguru, Private Peter Werema na Private Fortunatus Msofe, iliwasili juzi nchini na kuhifadhiwa katika Hospitali Kuu ya Kijeshi ya Lugalo.

Kaimu Msemaji wa JWTZ, Meja Joseph Masanja, alisema jana kuwa ratiba ya kuiaga miili ya wanajeshi hao itaanza leo mapema. “Ratiba itaanza asubuhi majira ya saa tatu.

Kwa hiyo, siyo vibaya wananchi kwa jumla wakafika kuanzia majira ya saa mbili na nusu asubuhi kuwaaga mashujaa wetu. Na ninatarajia itaendelea mpaka mchana,” alisema. Wanajeshi hao waliuawa hivi karibuni wakiwa sehemu ya askari 36 na ofisa wao mmoja, baada ya kushambuliwa na wanaosemekana kuwa waasi, wakati wakisindikiza msafara wa waangalizi wa kijeshi kutoka eneo la Khor Abeche kwenda Nyala, ambako wenzao 17 vile vile walijeruhiwa.

Jitihada zinazofanywa na Umoja wa Mataifa (UN), ikiwa ni pamoja na Rais Jakaya Kikwete, kuzungumza na Rais wa Sudan, Omar al Bashir, akimtaka kuwasaka, kuwakamata na kuwafikisha mbele ya vyombo vya sheria wale wote waliohusika na mauaji hayo, bado hazijafanikiwa hadi sasa.

Tanzania ina wanajeshi 850 kwenye kikosi cha UN cha kulinda amani katika Jimbo la Darfur.

MNYIKA ANUSURIKA KUUWAWA KWA BOMU




Mhe. John Mnyika
YASADIKIKA KUWA LILIRUSHWA NA POLISI ALIPOSIMAMA
VITUKO na matukio ya hatari kwenye mikutano ya CHADEMA vimeendelea kushika kasi. Jana Mbunge wa Ubungo, John Mnyika alinusurika kupigwa na bomu la machozi lililorushwa na polisi waliokuwa wakizuia kufanyika mkutano ulioitishwa na chama hicho.

 
Tukio hilo lilitokea katika eneo la Mabibo kwenye viwanja vya Sahara ambapo bomu hilo lilimpata mtu aliyekuwa karibu na Mnyika anayeitwa Thomas Jerome, aliyejeruhiwa sehemu ya paja.

Baada ya kurushwa kwa bomu hilo, polisi walitaka kumchukua majeruhi huyo ili wamweke kwenye gari lao apelekwe hospitalini, lakini Mnyika aliwaelekeza wafuasi wa CHADEMA kumchukua kwa madai kitendo kilichofanywa na askari hao kililenga kuficha ushahidi wa jambo hilo.

Polisi waliokuwemo eneo la tukio waliamua kukubaliana na matakwa ya wafuasi wa CHADEMA waliomchukua Jerome na kumpeleka hospitali ambako hali yake inadaiwa inaendelea vizuri.

Akielezea hali ilivyokuwa akiwa katika mkutano mwingine uliofanyika Ubungo, Mnyika alisema polisi walifika katika viwanja vya Sahara wakiwa na magari matatu kwa lengo la kutawanya wafuasi wa CHADEMA wasifanye mkutano wakidai haukuwa na baraka za jeshi hilo.

Mnyika alisema polisi hao walisema sababu ya kuuzuia mkutano huo ni uwepo wa ziara ya Makamu wa Rais katika Wilaya ya Kinondoni, hivyo walikuwa wameelekeza nguvu zao katika ziara hiyo, kwamba hawakuwa na uwezo wa kuulinda mkutano wa CHADEMA.

“Nikiwa nimejiandaa kupanda jukwaani ndiyo polisi walikuja kusema tuache tusifanye mkutano, nilisogea karibu na gari kumlalamikia ofisa wa polisi kwani kitendo cha kuahirisha mkutano kwa barua waliyoileta saa sita mchana siku ya mkutano wakati sisi tuliwapa taarifa siku nne zilizopita ilikuwa sio haki.

“Nilimwambia ofisa huyo wa polisi kuwa nilikuwa najadiliana kwa simu na viongozi wakuu wa Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam na Inspekta Jenerali wa Polisi Said Mwema kumlaumu kutumika vibaya kwa Jeshi la Polisi.

“Nilipokuwa bado najibizana naye bila fujo zozote, bomu lilirushwa kutoka ndani ya gari ya polisi na kupita karibu na mimi likamjeruhi mtu aliyekuwa karibu yangu, ki ukweli nimeshangazwa sana na matumizi mabaya ya silaha za moto,” alisema.

Aliongeza kuwa katika purukushani zilizotokea baada ya bomu kupigwa, alipoteza nyaraka mbalimbali alizokuwa amebeba kama ushahidi kuwaonyesha wafuasi wa chama hicho hasa jinsi serikali ya CCM na wabunge wake walivyopitisha kodi ya huduma za simu, na kodi ya laini za simu.

Slaa anena
Aidha katika mkutano huo ambao awali ulitangazwa kuwa ungehutubiwa na Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa, haukuweza kuhutubiwa naye kwa kile alichosema kuwa watu wake wa usalama walimwambia mapema hali si salama kwenye mkutano huo.

“Nilipata taarifa kutoka vyanzo vyangu kuwa polisi walikuwa na mpango wa kuleta fujo, hivyo nikaona kwa kuwa wanatuwinda nisingeenda kuhutubia, pengine bomu lililomkosa Mnyika lilikusudiwa kwangu au kwa mwingine,” alisema Dk. Slaa alipozungumza na gazeti hili kwa njia ya simu baada ya kutoonekana mkutanoni.

Monday, July 8, 2013

SOLAR PLANE COMPLETES US CROSS-COUNTRY FEAT



The Solar Impulse touched down at JFK International Airport after a historic two-month journey.

The first-ever manned planed that can fly by day or night on solar power has finished the final leg of a historic US cross-country journey.

Solar Impulse touched down at New York's John F Kennedy International Airport at 11.09pm on Saturday after leaving California in early May.

The plane has previously flown from Europe to Africa, but its creators said this was the first successful cross-continent flight.

The flight plan for the revolutionary plane, powered by some 11,000 solar cells, had called for it to pass the Statue of Liberty before landing early Sunday at New York.

But an unexpected eight-foot tear discovered on the left wing of the aircraft on Saturday afternoon forced officials to scuttle the fly-by and proceed directly to JFK for a landing three hours earlier than scheduled.

Pilot Andre Borschberg said: "It was a huge success for renewable energy. The only thing that failed was a piece of fabric."

"It was supposed to be the shortest and easiest leg. It was the most difficult one," said Bertrand Piccard, one of the two pilots.

The aircraft soars to 30,000 feet and can reach a top speed of 45mph.
Most of the 11,000 solar cells are on the super-long wings that seem to stretch as far as a jumbo jet's.

It weighs about the size of a small car and soars with what is essentially the power of a small motorised scooter.

The Solar Impulse has made stopovers in Phoenix, Dallas-Fort Worth, St Louis, Cincinnati and Dulles during its two-month journey.

The cross-country flight is a rehearsal for a planned 2015 flight around the globe with an upgraded version of the plane.

Solar Impulse's creators view themselves as green pioneers, promoting lighter materials, solar-powered batteries, and conservation as adventurous.

Wednesday, July 3, 2013

ZIARA YA RAIS WA MAREKANI BARRACK OBAMA NCHINI TANZANIA KATIKA PICHA!


Rais Barack Obama wa nchini Marekani na Mkewe Michelle Obama wakiwa sambamba na watoto zao, wakiwasili kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere,jijini Dar es Salaam mchana huu kwa ziara ya siku mbili hapa nchini

Rais Dkt.Jakaya Kikwete akiwa na mgeni wake Rais Barrack Obama wa Marekani muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam siku ya tar. 1. Nyuma ya Rais na mgeni wake ni Mke wa Rais Mama Salma Kikwete na mke wa Rais wa Marekani Mama Michelle Obama.
Rais. Jakaya Kikwete akiwa na Mgeni wake Rais wa Marekeni Baraka Hussein Obama, huku picha ya juu ikionesha wake za marais hao nao wakiwa pamoja.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimtambulisha kwa Rais Barrack Obama wa
Marekani Rais wa Zanzibar Dr.Ali Mohamed Shein muda mfupi baada ya
kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini
Dar es Salaam siku ya tar. 1. Huku Mke wa Rais Mama Salma Kikwete na Mke wa Rais wa Marekani Michelle Obama Wakiangalia.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimtambulisha kwa Rais Barrack Obama wa
Marekani makamu wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Iddi muda mfupi baada ya
Rais huyo wa Marekani kuwasili nchini kwa Ziara ya kikazi ya siku
mbili.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akimtambulisha kwa Rais Barrack Obama wa
Marekani Spika wa baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe. A. Kificho muda mfupi baada ya Rais huyo wa Marekani kuwasili nchini kwa Ziara ya kikazi ya siku mbili.
Rais. Barrack Obama wa Marekani akipokea salamu ya heshima kutoka kwa mkuu wa Majeshi ya ulinzi na usalama Brig. Gen. Davis Mwamunyange, baada ya kutambulishwa kwake na mwenyeji wake Rais. Kikwete.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho kikwete akiwatambulisha baadhi ya viongozi waandamizi wa serikali kwa Rais Barrack Obama na mkewe katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.

Rais. Barrack Obama na Mwenyeji wake wakipokea heshima na kupigiwa nyimbo za mataifa yao, baada ya kuwasili na kupokelewa na mwenyeji wake Rais. Kikwete.
Rais. Barrack Obama akikagua gwaride la heshima lililoandaliwa kwa ajili yake na wanajeshi wa JWTZ.
Rais Barack Obama wa Marekani na mwenyeji wake Rais Jakaya Mrisho Kikwete wakipokewa kwa Shangwe Ikulu, Jijini Dar es salaam.

Kwa habari zaidi  katika Picha akiwa Ikulu ...

Monday, July 1, 2013

WAKATI TUKISUBIRI MASAA MACHACHE KUMPOKEA RAIS BARRACK OBAMA LEO HII, ZITTO AFUNGUKA FB


Mhe. Zitto Kabwe
Hatimaye Barack Obama, Rais wa Marekani anatembelea tena bara la Afrika. Hii itakuwa ni mara ya pili Obama kutembelea Bara hili alikotoka baba yake baada ya ziara yake ya kwanza mwaka 2009. Mwaka huo alitembelea Ghana na Misri ilhali mwaka huu anatembelea Senegali, Afrika Kusini na Tanzania. 

Ziara hiyo itakayoanza tarehe 26 mwezi Juni, itamfikisha Tanzania tarehe 1 Julai na kuondoka siku ya pili yake.

Uchaguzi wa Obama kuwa Rais wa Marekani ulipokolewa kwa shangwe Afrika nzima. Wakati Waziri wa mambo ya nje wa Nigeria alilia kwa furaha, nchi ya Kenya ilitangaza siku ya mapumziko na Rais wa zamani wa Afrika Kusini ndugu Nelson ‘Madiba’ Mandela alisema ‘ushindi wa Obama unawafanya Waafrika wathubutu kuota ndoto (Jarida la The Economist). Hapa Tanzania kulikuwa kuna shamra shamra za kila namna na magazeti yaliweka vichwa vya habari kana kwamba ni Rais wa Tanzania aliyechaguliwa. Waafrika walikuwa na matumaini makubwa sana na bwana Obama. Yamefikiwa?

Ni vema ifahamike kuwa Barack Obama ni Rais wa Marekani na siku zote atalinda maslahi ya Marekani tu. Kuwa na matumaini makubwa kwamba labda yeye angeliweza kuiweka Afrika mbele sana ilikuwa ni kujifurahisha tu nafsi. Maslahi ya Marekani ni ya kipaumbele kuliko kitu kingine chochote kwa Rais Obama. Kwa wengi Obama amekuwa kama amewavunja moyo.

Obama wakati akiwa Senegal
Tanzania inapokea kiongozi wa Taifa kubwa duniani wa pili sasa ndani ya kipindi cha miezi 3 tu. Kwanza alikuja Rais wa China na sasa wiki hii anakuja Rais wa Marekani. Maneno ya mtaani na kwenye mabaraza ya majadiliano ni kwamba viongozi hawa wanakuja kugombea maliasili tulizo nazo kama gesi asilia na madini. Nadhani haya ni maneno ya kusema katika kupiga soga maana kunyonywa kwa rasilimali hakuhitaji Rais wa Marekani aje Tanzania.

Makampuni yote makubwa yanayochimba dhahabu hapa nchini ni makampuni ya nje na marais wao hawakuja ili waweze kupata mikataba minono ya kuvuna utajiri wetu. Katika kitalu namba 2 cha utafutaji wa mafuta na gesi huko Bahari Kuu kampuni ya kimarekani ya ExxonMobil ina ubia na kampuni ya Norway ya StatOil. Kampuni hiyo haikusubiri Rais wa Marekani aje ili wapate mikataba.

Kuna makampuni mengi sana ya kichina yanajenga barabara zetu hapa nchini yakiwa na mikataba minono sana. Kule Mchuchuma na Liganga kuna kampuni ya kichina inajiandaa na uchimbaji wa chuma na makaa ya mawe. Makampuni yote haya hayakusubiri Rais wao aje.

Hoja inayojengwa hapa ni kwamba ujio wa Marais mbalimbali nchini ni ujio wa kujijenga kidiplomasia na wakati mwingine kama sehemu ya kutuma ujumbe Fulani kwa dunia. Nchi inayotembelewa pia inaweza kuona kuwa diplomasia yake inaheshimiwa na mataifa yanayoitembelea.

Hata hivyo hii haiondoi ukweli kwamba Obama anakuja kwa ajili ya maslahi ya nchi yake kama ilivyo kwa wachina walivyokuja. Tumesikia Rais Obama ataambatana na mamia ya wafanyabishara kutoka Marekani kwa ajili ya kupata fursa za kuwekeza nchini. Pia tutasikia matangazo kuhusu msaada wa pili wa Millenium Challenge ambapo Wamarekani wanaendelea kumwaga pesa nchini kusaidia miundombinu lakini pia kushawishi kuungwa mkono na nchi zetu kwenye maamuzi Fulani Fulani jumuiya za kimataifa.

Tumesikia Obama atakwenda kutembelea mitambo ya kampuni ya Symbion. Hii ni mitambo ambayo miaka 4 iliyopita ilipigiwa kelele kuwa ni mitumba na hivyo TANESCO wasiinunue. Hawakununua na badala yake kampuni hiyo ya kimarekani ikainunua, wakaingia mkataba na TANESCO kuwauzia umeme unaozalishwa na mitambo hiyo hiyo chakavu. Wakati tunasuburi kulipa takribani tshs 105 bilioni kwa Dowans baada ya kutubwaga kwenye kesi, tunasubiri kuona wanasiasa watakaokwenda kumsindikiza Obama kwenye matembezi hayo ya kutembelea mitambo chakavu.