To Chat with me click here

Wednesday, July 24, 2013

SHIRIKA LA MSALABA MWEKUNDU TANZANIA KUGAWA VYANDARUA 68,000 KWA WAKIMBIZI




Shirika la Msalaba Mwekundu nchini Tanzania (TRCS) litasambaza vyandarua 68,000 vilivyowekwa dawa ya kuua mbu kwa wakimbizi wanaoishi kwenye kambi ya Nyarugusu mkoani Kigoma.

Shirikisho la Kimataifa la Msalaba Mwekundu na Mwezi Mwekundu linafadhili usambazaji huo, ambao utaanza tarehe 30 Julai kwa kushirikiana na kampeni ya Wakfu wa Umoja wa Mataifa ya "Si Chochote ila Vyandarua tu" na mashirika washirika ya misaada.

"Malaria ni ugonjwa pekee inaouwa watu wengi kabisa kwenye kambi hii ya wakimbizi, yakiwaathiri zaidi wanawake wajawazito na watoto walio chini ya umri wa miaka mitano," alisema Rais wa TRCS, George Nangale.

Zaidi ya matukio 11,000 yalirikodiwa kwenye kambi hiyo kati ya mwezi Januari na Aprili mwaka huu, na malaria ni sababu ya asilimia 60 ya matibabu ya kiafya, alisema.

Wengi wa wakimbizi kwenye kambi ya Nyarugusu wanatoka Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

No comments:

Post a Comment