To Chat with me click here

Saturday, October 18, 2014

MWANASHERIA MKUU MPYA ZANZIBAR AAPISHWA!




Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr.Ali Mohamed Shein amemuapisha mwanasheria mkuu mpya wa Zanzibar Said Hassan Said akichukua nafasi ya Bw. Othman Masoud.

Hafla ya kumuapisha Bw. Said ilifanyika ikulu ya Zanzibar Jana (Friday , 17th Oct , 2014) na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa seriklai akiwemo makamu wa kwanza wa Rais Malim Seif Sharrif Hamad, Waziri wa Bishara Viwanda na Masoko Mhe. Nassor Mazrui, mkuu wa mkoa wa Mjini Magharibu Abdullah Mwinyi, Mufti mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabi, Mstahiki Meya wa Zanzibar Mhe. Abdulrahman Khatibu na vingozi wengine wa serikali.

Uteuzi wa Bw Said Hasan Said ambaye kabla ya uteuzi huo alikuwa naibu mwanasheria mkuu imekuja baada ya Dr Ali Shein Rais wa Zanzibar kumfuta kazi mwanasheria mkuu wa Zanzibar Bw Othman Masoud Othman wiki iliyopita huku kukiwa hakuna sababau yeyote iliyotolewa na serikali.

Ingawa Duru za siasa zianoyesha wazi wazi kuwa kufutwa kwake kazi ni kutokana na kupinga baadhi ya vifungu vya Katiba Inayopendekezwa wakati wa upigaji kura na kabla ya hapo kujiondoa katika kamati ya uandishi wa Katiba hiyo.

No comments:

Post a Comment