 |
|
Maofisa wa usalama wa Kenya Jumatatu wakionyesha
silaha zilizokamatwa wakati wa mapigano ya koo katika wilaya ya Rhamu, Kaunti
ya Mandera.
|
Polisi
huko kaskazini mashariki mwa Kenya wameimarisha usalama katika kaunti ya Wajir
kuzuia vurugu zilizoenea kutoka Kaunti jirani ya Mandera baina ya koo za
Degodia na Gare.
Vurugu
za hivi karibuni ziliibuka huko Wajir zilianza Ijumaa iliyopita (tarehe 21
Juni) wakati wanaume washukiwa wa koo za Degodia walipovamia malori mawili
katika kijiji cha Eldas, na kuua wanaume wanne wa koo za Gare, Mkuu wa Kaunti
ya Wajir Naftali Mung'athia alisema.
Katika
kulipiza kisasi kwa mfululizo wa mashambulio ya hivi karibuni dhidi ya Gare, wanaume
wenye silaha walivamia kambi ya watu wasio na makazi ndani ya nchi katika
wilaya ya Banisa ya Kaunti ya Mandera, na kuua watu 14 ikiwa ni pamoja na ofisa
polisi Jumapili. Waliokufa, ni pamoja na wanawake na watoto, wote kutoka ukoo
wa Degodia.
 |
| Baadhi ya Familia zilizokosa makazi. |
Jumatatu,
kundi la watu kutoka katika ukoo wa Degodia waliwalenga watu kutoka ukoo wa
Gare katika ghasia kwenye mji wa Wajir, walimuua mwanamke mmoja na mwingine
kujeruhiwa vibaya baada ya kukanyagwa na msafara uiokuwa ukibeba familia
zilizokuwa zikikimbia vurugu hizo.
Kuepusha
mapigano zaidi baina ya koo mbili hizo, mamlaka zinazohusika zimesambaza
maofisa usalama na askari katika viunga vyote vya jirani na Wajir, Mung'athia
alisema. Alitoa wito kwa wakaazi wa Wajir kuwa watulivu wakati serikali ya
Kaunti ikifanya kazi kutatua mzozo huu, akiongezea kwamba upigaji marufuku wa
muda wa mikusanyiko imetekelezwa.
"Tunafanya
kazi mchana na usiku kuzuia mzozo kutokuendelea," Mung'athia alisema.
"Tumewataka viongozi wa ndani na maulamaa kuungana katika kurejesha amani
baina ya koo hizi."
Historia yenye vurugu
Wimbi
la hivi karibuni la vurugu hizi lilianza mwezi Machi wakati wa gari la kampeni
linalomilikiwa na mgombea seneta Billow Kerrow, ambaye anatoka katika ukoo wa
Gare, lilipomgonga na kumuua mfanyabiashara kutoka katika ukoo wa Degodia huko
Rhamu. Baadhi ya wanachama wa jumuiya ya Degodia walidai ajali ilikuwa
imepangwa.
Kutoka
hapo, mapigano ya koo, na mashambulizi ya kulipiza kisasi yameshaua watu zaidi
ya 50 na kufanya mamia ya familia kukosa makazi.
Vurugu
baina ya koo mbili hizio yamekuwa yakipamba moto siku hadi siku, na yalianza
kuongezeka kutoka mwaka 1984 wakati ukame uliposababisha mzozo wa maeneo ya
malisho, kwa mujibu wa Mkuu wa Kaunti ya Mandera Michael ole Tialal.
Gare
ni ukoo unaotawala huko Mandera, wakati Degodia ni wengi huko Wajir.
Usambazaji
mdogo wa maji na ardhi ya malisho yamekuwa ni maeneo ya mzozano kati ya koo
hizo, Tialal alisema, akiongeza kwamba kuenea kwa bunduki katika mpaka wa
Somalia na Ethiopia kumeongeza vurugu katika tatizo la usalama la mkoa.
"Ni
mara ya kwanza kwa ukoo kutumia chombo cha kurushia maguruneti katika mapigano
yao ya koo," Tialal alisema, akirejea shambulio kwenye kambi katika wilaya
ya Banisa. "Vurugu hizo pia zilihusisha kuchoma nyumba na kuvamia
magari."
"Kwa
sasa tunatoa kikundi cha walinzi cha wasindikizaji wenye silaha na magari
yanashauriwa kusafiri kwa kusindikizwa na ulinzi ili kupunguza [uwezekano wa]
shambulio,".
Siku
ya Jumatatu, Inspekta Jenerali wa Polisi wa Kenya David Kimaiyo aliwaita
viongozi waliochaguliwa wa kaunti za Mandera na Wajir katika idara ya Uchunguzi
wa Makosa ya Jinai kuhusiana na ripoti za upelelezi zikionyesha kwamba
mashambulizi "yalichochewa kisiasa".
Baada
ya kukutana Nairobi siku ya Jumatatu na viongozi wa kaunti zote mbili, Rais
Uhuru Kenyatta alisema serikali ya Kenya inaweza kutumia nguvu kurejesha amani
katika mkoa wa kaskazini-mashariki, akiagiza jamii zinazopigana kusalimisha
silaha haramu.
"Kama
jamii za kaunti za Mandera na Wajir hawatarejesha amani wao wenyewe, serikali
itakuwa haina lingine la kufanya bali kutumia operesheni ya ulinzi ambayo
inaweza kutokuwa na matokeo yasiyodhamiriwa," rais alisema.
Pia
Kenyatta aliahidi kufanya kazi na serikali ya Ethiopia kuhakikisha kuishi
pamoja kwa amani miongoni mwa jamii nyingine za kikabila zilizoenea katika mkoa
ambako mipaka ya Kenya, Ethiopia na Somalia inakutana.