To Chat with me click here

Friday, July 26, 2013

UTAFITI: SERA YA UWEKEZAJI MADINI HAINUFAISHI JAMII



Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo cha Uhasibu Arusha na Mchumi, Balozi Morwa alitoa mapendekezo hayo juzi, wakati akiwasilisha utafiti kuhusu wajibu wa kampuni kwa jamii(CSR),uliofanyika katika machimbo ya Tanzanite Mirerani, wilayani Simanjiro Mkoa wa Manyara.

ARUSHA, Tanzania: 

Serikali imeshauriwa kubadili sera ya uwekezaji nchini kwa kulazimisha kisheria kampuni za wawekezaji hasa wa Sekta ya Madini, kutekeleza miradi ya jamii inayozunguka maeneo yao ya uchimbaji badala ya suala hilo kuwa ni la hiari.

Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo cha Uhasibu Arusha na Mchumi, Balozi Morwa alitoa mapendekezo hayo juzi, wakati akiwasilisha utafiti kuhusu wajibu wa kampuni kwa jamii(CSR),uliofanyika katika machimbo ya Tanzanite Mirerani, wilayani Simanjiro Mkoa wa Manyara.

Morwa akiwasilisha utafiti huo ,ambao uliratibiwa na Mtandao wa Mashirika yasiyo ya kiserikali ya Mkoa wa Arusha kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa la Finnish NGO Platform, alisema wamebaini kuwa jamii zinazozunguka migodi ya Tanzanite hazinufaiki ipasavyo.

Morwa alisema utafiti huo, ulihoji watu 350 na nyaraka kukusanywa,wamebaini,wajibu wa kampuni ya wawekezaji kwa jamii ukiwa wa kisheria kama Ghana, utawanufaisha na ikishindika ifutwe na kampuni hizo zilipe kodi kubwa kama nchi nyingine.

No comments:

Post a Comment