To Chat with me click here

Tuesday, October 22, 2013

UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA UFANYIKE 2015


Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Warioba  

Jana  gazeti la Mwananchi lilichapisha habari katika ukurasa wa kwanza ikisema Tume ya Mabadiliko ya Katiba imeomba kuongezewa muda wa mwezi mmoja kutokana na ugumu wa kazi ya uchambuzi wa maoni yaliyotolewa na wananchi na asasi mbalimbali. Kama mambo yangekwenda kama ilivyotarajiwa hapo awali, Tume hiyo iliyoanza kazi Mei 1 mwaka jana, chini ya Jaji Joseph Warioba ingekamilisha kazi yake Novemba 1, mwaka huu.

Kwa mujibu wa Sura ya 83 ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Tume hiyo ilitakiwa kufanya kazi kwa miezi 18. Hata hivyo, Makamu Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Augustino Ramadhan alisema juzi kwamba wamepeleka serikalini ombi la kuongezewa muda wa kufanya kazi kutokana na kukabiliwa na kazi ya ziada ya kuchambua maoni hayo. Pamoja na Serikali kukiri kupokea ombi hilo, hadi tunakwenda mitamboni jana ilikuwa haijatoa jibu la kulikubali wala kulikataa.

Sisi hatuoni sababu yoyote inayoweza kuisukuma Serikali kulikataa ombi hilo, hasa kutokana na kujitokeza kwa mambo mengi ambayo hayakutarajiwa kabla na wakati wa mchakato wa Katiba Mpya. Mikutano ya Mabaraza ya Katiba iliyofanyika nchi nzima, kwa mfano ilizua tafrani kubwa ambapo wajumbe wa mabaraza hayo waligawanyika kwa misingi ya kisiasa na kiitikadi. Tume hiyo ililazimika kutumia muda mwingi kujielekeza katika kutoa tafsiri na kufafanua vifungu katika Rasimu ya Kwanza ya Katiba. Pia Tume ilitumia muda mrefu kuratibu mijadala ya Rasimu hiyo, kwani wajumbe wengi wa mabaraza hayo walikuwa wakijadili hoja zilizotokana na misimamo ya vyama vyao badala ya kujadili rasimu yenyewe.

Hivyo, Serikali haina budi kukubali ombi hilo la tume haraka iwezekanavyo, pamoja na ukweli kwamba kuiongezea tume mwezi mmoja kuchambua maoni ya wananchi na asasi mbalimbali ni kuongeza gharama za mchakato huo. Lakini, wahenga waliposema maji ukiyavulia nguo ni sharti uyaoge, walipatia kabisa usemi huo, kwani kama tumeamua kama taifa kupata Katiba Mpya itakayotuvusha miaka 50 mingine ijayo lazima tubebe gharama hizo za kutuletea demokrasia ya kweli.

Ni vyema tukatambua kwamba hatua ya tume ya kuomba kuongezewa mwezi mmoja siyo ya ajabu. Sheria inaipa tume hiyo fursa ya kuongezewa miezi miwili nje ya muda uliowekwa. Kinachotakiwa sasa ni Serikali kujipanga vizuri na kutekeleza mambo mbalimbali kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu wa 2015. Mambo hayo ni pamoja na kuandaa, kurekebisha na kupitisha sheria mbalimbali kwa lengo la kuondoa sheria kandamizi na kuweka sheria zitakazowezesha kuwapo mazingira linganifu ya ushindani wa kisiasa. Kwa mfano, inahitajika sheria mpya ya Tume Huru ya Uchaguzi.

Moja ya mambo muhimu ambayo Serikali inapata kigugumizi kuyatolea uamuzi ni suala la kufanya uchaguzi wa Serikali za Mitaa sambamba na Uchaguzi Mkuu wa 2015. Muda uliobaki kati ya sasa na 2014 (ambao ulipangwa kufanyika) hautoshi kufanya maandalizi na uchaguzi ulio huru na haki. Uchaguzi huo ni vyema usimamiwe na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi. Hivyo, Tamisemi iliyokuwa ikisimamia chaguzi za Serikali za Mitaa na kusababisha malalamiko mengi kutoka kwa wananchi itakuwa imeondolewa mzigo huo mzito. Kufanya uchaguzi huo wakati mmoja na Uchaguzi Mkuu kutapunguza gharama kwa kiasi kikubwa kama ilivyo katika nchi nyingi barani Afrika na kwingineko.

Monday, October 21, 2013

ZITTO ‘AMGEUZIA KIBAO’ CAG RUZUKU VYAMA VYA SIASA!

Mhe. Zitto Kabwe, Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya PAC
WAZIRI Kivuli wa Fedha na Uchumi, Zitto Kabwe ametaka Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), ichunguzwe kwa uzembe wa kushindwa kukagua hesabu za ruzuku za vyama vya siasa kwa muda wa miaka mitatu.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, Kabwe alisema CAG ameshindwa kukagua ruzuku ya Sh83 bilioni iliyotolewa kwa vyama vya siasa nchini tangu mwaka 2005 hadi 2010.

Alisema ingawa kuna tatizo katika Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, CAG hawezi kumtupia mzigo huo pekee yake kwani naye anahusika.

“Nikiwa Waziri Kivuli wa Fedha na Uchumi, ninamwomba CAG afanye audit (ukaguzi) kwa vyama vyote vya siasa kwa miaka mitatu iliyopita sasa na siyo baada ya miezi sita,” alisema Kabwe na kuongeza:

“Ruzuku ya vyama vya siasa ni eneo ambalo huwa haliangaliwi kabisa na fedha nyingi ya walipa kodi inakwenda katika vyama. Kuanzia mwaka 2005 mpaka 2010 jumla ya Sh 83 bilioni zimetolewa kama ruzuku kwa vyama vya siasa,” alisema Kabwe na kuongeza:

“Fedha zote hizi kwa miaka yote hii, hazikuwa zinakaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, (CAG).”

Kwa mujibu wa Kabwe, ubadhirifu unaoweza kujitokeza kwenye fedha za ruzuku zinazotolewa kwa vyama vya siasa, unatokana pamoja na mambo mengine na CAG kushindwa kukagua ruzuku hizo tangu vyama vianze kuipata mwaka 1996.

“Ndiyo maana kumekuwa na ubadhirifu mwingi wa fedha za ruzuku kwenye vyama takriban vyote hapa nchini,” alisema Zitto.

Alisema mwaka 2008, alipeleka pendekezo la mabadiliko ya Sheria ya Vyama vya Siasa katika Bunge la Novemba kutaka vyama vikaguliwe na CAG.

Alisema pendekezo lake lilisomeka: “Vyama vyote vitakaguliwa na CAG na itakuwa ni jukumu la vyama vya siasa kupeleka taarifa zao kwa CAG kwa mujibu wa sheria.”

“Hivyo tangu mwaka 2008 vyama vinatakiwa vikaguliwe na CAG kwa mahesabu yao lakini mpaka sasa hakuna chama ambacho kimeshakaguliwa,” alisema Zitto na kuongeza:

“CAG mwaka huu amelalama tu kwenye taarifa yake kuwa vyama havikupeleka taarifa zao kwa Msajili. Ametoa miezi sita ili wasahihishe makosa? miezi sita ili watafute nyaraka za kugushi ili kuyaweka mahesabu sawa?” alihoji.
Kabwe alisema kauli ya CAG kwamba hahusiki kuvikagua vyama vya siasa ni kukwepa majukumu kwani sheria ya sasa inamtaka afanye hivyo kwa kuteua wawakilishi.

“Hakuna sababu kwa CAG kutoa miezi sita kwa vyama, bali vyama sasa viheshimu Public Audit Act,(Sheria ya Ukaguzi wa Fedha za Umma), Public Finance Act (Sheria ya Fedha za Umma) and (na) Political Parties Act (Sheria ya Vyama vya Siasa)”

Kwa mujibu wa Kabwe, CAG anapaswa kudai mahesabu kutoka kwa vyama na wala si kusema kuwa hahusiki na watu binasi. “Vyama siyo ‘individuals’, vyama ni taasisi,” alisema.

“Kwa sheria mpya, wakaguzi wa vyama wanapaswa kuteuliwa na CAG na siyo vyama kwenda kuokota wakaguzi na kuweka hesabu zao kama ambavyo imezoeleka,” alisema.

Zitto alisema vyama vya siasa ndivyo vinavyounda Serikali, hivyo iwapo haviheshimu fedha za walipa kodi, Serikali wanazounda haziwezi kuheshimu fedha za walipa kodi.

“Ruzuku iliyotolewa kwa vyama mwaka 2010 ilikuwa ni mara tatu ya Bajeti ya Wizara ya Afrika Mashariki au ni zaidi ya Bajeti ya Wizara ya Viwanda na Biashara. CAG ni lazima afanye kazi yake,” alisema na kuongeza:

“Msajili wa Vyama naye achunguzwe, ofisi yake inafanya kazi kwa mujibu wa sheria, kwa nini hakuwa na taarifa za vyama vya siasa wakati yeye ndiye mwenye jukumu la kusimamia vyama.”
“Iwapo anashindwa kusimamia ruzuku kukaguliwa atawezaje kusimamia matumizi ya fedha kwenye uchaguzi wakati uchaguzi uligubikwa na matumizi ya fedha nyingi za kifisadi,” alidai Zitto.

Ripoti ya CAG iliyoishia Juni 30 mwaka 2010, imeeleza kuwa vyama sita vyenye wawakilishi bungeni vimeshindwa kuonyesha taarifa za matumizi ya ruzuku ya Sh17.14 bilioni.

Vyama hivyo ni CCM, CUF, Chadema, NCCR-Mageuzi, TLP na UDP. Katika hesabu za kawaida kuhusu fedha hizo, chama hicho tawala kimepata mgawo wa Sh12 bilioni kutokana na asilimia 70 ya mgawo.

CUF kinachopata asilimia 20 ya ruzuku kimepata mgawo wa Sh3.43 bilioni, Chadema chenye asilimia nane Sh1.37 bilioni na vyama vitatu vinavyoshikilia asilimia mbili Sh343 milioni.

Akijibu Madai hayo, Utouh alisema: “Sijakwepa majukumu. Fedha zinatoka serikalini, zinakwenda kwa Msajili wa Vyama.”

“Yeye (Msajili), ndiye mwenye kazi ya kuvigawia vyama fedha hiyo na sheria inataka baada ya matumizi, vyama vinapaswa kutengeneza hesabu zake na kuziwakilisha kwa Msajili. Siyo kazi yangu kuvitengenezea mahesabu vyama vya siasa.”

Kuhusu madai ya Zitto kwamba utaratibu huo wa Msajili kukagua vyama uko kwenye sheria ya zamani ambayo Zitto alidai kwamba alishatoa mapendekeza bungeni na kufanyiwa marekebisho, yanayomtaka CAG kuteua wakaguzi wa hesabu za vyama vya siasa, Utouh alisema:

“Mwulize yeye (Zitto) chama chake kilishanipelekea mahesabu ili niyakague kama anajua hivyo ndivyo inavyotakiwa? Tupo hapa kufanya kazi. Hatupo kukwepa majukumu. Mwulize kama hivyo ndivyo sheria inavyotaka Chadema ilishawahi kuniletea mahesabu yake?”

Chanzo: Gazeti la Mwananchi

Saturday, October 19, 2013

HIVI NDIVYO TEKNOLOJIA ILIVYO HIVI SASA!

Hii ni Kofia ya waendesha pikipiki ambayo inamwezesha mwendesha pikipiki kuona kwa nyumba bila kugeuza shingo wala kutumia vioo vya pembeni (side mirrors).

Flash Drive - hii ni ya kisasa kabisa, imetengezwa kwa GOLD na inauwezo mkubwa wa kutunza data zako. Uzuri wake zaidi ni kwamba ina lock-system, ambayo mtu hata akikuibia hataweza kuitumia labda awe anajua keyword yako.

Hiki ni chombo ambacho kinaweza kusaidia watu wengi ku-control matumizi yao ya vitu mbalimbali kama sukari, chumvi, n.k Kinauwezo wa kupima uzito au ujazo wa kitu kulingana na matumizi.

Friday, October 11, 2013

RWANDA DAY DRAWS CELEBRATIONS AND PROTESTS AGAINST PRESIDENT PAUL KAGAME



Rwandan-Canadians gathered in Toronto to connect with their community and learn about investment opportunities in their home country, as protesters loudly objected to the presence of President Paul Kagame.

Rwanda's President Paul Kagame

Hundreds of Rwandan-Canadians gathered in Toronto on Saturday to connect with their community and learn about investment opportunities in their home country.

But there was a small but noisy presence from a couple dozen protesters at the Rwanda Day event at Downsview Park, objecting to the presence of Rwanda’s controversial President Paul Kagame .

This was the first Rwanda Day held in Canada after previous versions in the U.S., London and Paris. Organizers said about 3,000 people attended, amid tight security and a large contingent of Toronto police.

“The main objective is to reconnect members of the community living abroad with their mother country,” said Shakilla Umutoni, Rwandan chargée d’affaires. That included updating them on developments in Rwanda and informing them of investment opportunities back home. 

About 15 Rwandan businesses and a few Canadian ones set up information booths at the event, she said, before the event turned into a party featuring a performance from Canadian rapper Shad, who was born in Kenya to Rwandan parents.

For Elvira Rwasamanzi, a 21-year-old biotech student from Ottawa, the focus on investing in Rwanda was one of the main draws of the day.
“It was really motivating,” said Rwasamanzi, who came to Canada from Rwanda as a young child. “It makes you want to give back because you’re proud.”

Kagame used part of his speech to encourage Rwandan-Canadians to invest in Rwanda, Umutoni said.
“He said if you travelled all the way from your country and got to Canada, take advantage of that . . . and do your best, not just for yourself but for your country.”

But it was the very presence of Kagame that brought protesters to the event, saying that Canada shouldn’t have let him enter given his record on human rights.

Rwandan opposition figures have been jailed and several countries suspended their aid to Rwanda last year citing its military support for M23 , a rebel group responsible for serious abuses in the Democratic Republic of Congo, according to the United Nations and human rights groups. Kagame has denied involvement.

Protesters also cited a 2010 UN report implicating the Rwandan government in killing tens of thousands of Hutus in the eastern part of what is now Congo, following the 1994 Rwandan genocide in which Hutus targeted Tutsis and up to a million people were killed. (Kagame and many of today’s government leaders are Tutsis.) Rwanda denounced the report. 

“Paul Kagame is a criminal financing a military movement in eastern Congo,” said Aime Kabuya of the Congolese Citizen Movement. “He shouldn’t have the freedom to travel that he does now. Why did Canada give him a visa?”

Perpétue Muramutse of the International Women’s Network for Democracy and Peace also raised concerns about Kagame’s pro-development message.

“The Rwandese are very poor,” she said. “They say there’s development in Rwanda but it’s development for just a small part of the people. When you go to the countryside, you see people with nothing to eat.”

Umutoni said she respected the right of protesters to express their views, but questioned why they were raising those concerns at Rwanda Day.
“This is purely a Rwandan event.”