To Chat with me click here
Showing posts with label Sensa. Show all posts
Showing posts with label Sensa. Show all posts

Monday, August 27, 2012

SENSA DOSARI TUPU

BAADHI YA WAISLAMU WAGOMEA, WAKAMATWA

SENSA ya watu na makazi iliyoanza jana nchini kote, imegubikwa na kasoro kadhaa katika maeneo mbalimbali, huku suala la uhaba wa vifaa kwa makarani likionekana kuwa kubwa.

Hata hivyo, mbali ya uhaba wa vifaa kwa makarani, pia tishio la baadhi ya viongozi wa Kiislamu kuwashawishi waumini wao kususia, nalo lilileta mkanganyiko kwa baadhi ya maeneo.

Katika maeneo kadhaa, vilionekana vipeperushi kwenye baadhi ya nyumba vyenye ujumbe wa kuwakataza Waislamu wasishiriki shughuli hiyo, jambo lililowalazimu polisi kusambaa mitaani na kuwatia mbaroni baadhi ya watu waliodaiwa kuvisambaza.

Pia, uelewa mdogo wa baadhi ya makarani nao ulilalamikiwa na wananchi wengi, kwani walitumia muda mrefu kuandikisha taarifa zao na huku wakidai kuwa maswali mengine yanayoulizwa kwenye dodoso hizo hayana maana yoyote.

Waislamu wasusia Dar
Jijini Dar es Salaam, makarani katika baadhi ya maeneo walikwama kupata takwimu za baadhi ya wakazi kutokana na kushikilia msimamo wa viongozi wao wa kiroho wa kususia sensa hiyo.