BAADHI YA WAISLAMU WAGOMEA, WAKAMATWA
SENSA
ya watu na makazi iliyoanza jana nchini kote, imegubikwa na kasoro kadhaa
katika maeneo mbalimbali, huku suala la uhaba wa vifaa kwa makarani likionekana
kuwa kubwa.
Hata
hivyo, mbali ya uhaba wa vifaa kwa makarani, pia tishio la baadhi ya viongozi
wa Kiislamu kuwashawishi waumini wao kususia, nalo lilileta mkanganyiko kwa baadhi
ya maeneo.
Katika
maeneo kadhaa, vilionekana vipeperushi kwenye baadhi ya nyumba vyenye ujumbe wa
kuwakataza Waislamu wasishiriki shughuli hiyo, jambo lililowalazimu polisi
kusambaa mitaani na kuwatia mbaroni baadhi ya watu waliodaiwa kuvisambaza.
Pia,
uelewa mdogo wa baadhi ya makarani nao ulilalamikiwa na wananchi wengi, kwani
walitumia muda mrefu kuandikisha taarifa zao na huku wakidai kuwa maswali
mengine yanayoulizwa kwenye dodoso hizo hayana maana yoyote.
Waislamu
wasusia Dar
Jijini
Dar es Salaam, makarani katika baadhi ya maeneo walikwama kupata takwimu za
baadhi ya wakazi kutokana na kushikilia msimamo wa viongozi wao wa kiroho wa
kususia sensa hiyo.


