To Chat with me click here

Friday, January 31, 2014

KIONGOZI WA KUNDI LA WATOTO “MBWA MWITU ATIWA MIKONONI MWA POLISI



Habari zilizotufikia katika mtandao wetu ni kuwa, aliyekuwa kiongozi na mwanzilishi wa kundi la vijana ambao wamekuwa wakijiita “MBWA MWITU” ambaye anafahamika kwa jina la bandia kama KASELA amekamatwa jana majira ya saa 7 mchana, maeneo ya Yombo Buza, ambako alikutwa akicheza POOL TABLE. 

Mashuhuda wa tukio hilo walisema kuwa, Kasela alikutwa akicheza pool table na baadhi ya raia wema, ndipo walipoamua kuwataarifu polisi juu ya uwepo wake eneo hilo. Polisi hawakuchukua muda wakawa wamefika eneo la tukio kabla mshukiwa hajastukia mpango huo. Baada ya kijana huyo kuwatambua askari polisi, alitimua mbio ambazo hazikufua dafu kwa askari hao ambao walikuwa na bunduki zao mkononi pamoja na baadhi ya raia wema waliojitolea kusaidia polisi. Polisi walifanikia kumnasa Kasela baada ya kujisalimisha kwao, alipoamrishwa kusimama.  

Yasemekana kijana huyu alizaliwa tarehe 28 December 1995 na anaishi na wazazi wake wote wawili (Baba na Mama) ambao nao walikwisha onja joto ya jiwe ya motto wao, baada ya kuwachapa makonde kwa kuwa walimsema katika kumrekebisha tabia. 

Mbali na kuwa yeye ndiye muasisi wa kundi hilo la vijana wadogo wa mbwa mwitu, kijana huyo amekwisha shiriki katika matukio mbalimbali ya wizi na umwagaji damu katika maeneo ya Yombo Vituka Lumo, Kiwalani na Buza. Matukio hayo ndiyo yaliyopelekea wananchi wa maeneo tajwa kujawa na hasira kiasi cha kuwasaka mbwa mwitu hao na kupelekea vifo vya wanakundi hilo wawili waliotambulika kwa majina ya Mpolendi na Traveller, huku wengine wakikimbilia mikoa ya jirani kama vile Tanga na Pwani.  

Kwa sasa hali ni swali katika maeneo hayo, na wananchi wamepokea kwa furaha sana taarifa za kukamatwa kwa kiongozi huyo wa kundi la mbwa mwitu. 

Mwisho kabisa kwa niaba yangu binafsi pamoja na wadau wengine wote wa blog yetu, napenda sana kulipongeza jeshi la polisi, kwa kuweza kufanikisha kumkamata kijana huyo ambaye amekuwa tishio na gumzo kwa wakazi wa maeneo taja. Ni matumaini yangu kuwa sharia itachukua mkondo wake. 

No comments:

Post a Comment