To Chat with me click here

Monday, September 30, 2013

SHAMBULIO LA WESTGATE LADHIHIRISHA MAPUNGUFU MAKUBWA KATIKA USALAMA


Askari wa Kenya wakielekea katika maduka ya WestGate


Wakati vitisho vikirudiwa na dhihaka kutoka kwa al-Shabaab vilivyotokea siku chache zilizopita, Watu wa Kenya bado wanatafuta majibu ya ni kwa namna gani uzingiraji uliosababisha umwagaji wa damu ulivyotokea katika kituo cha biashara ya maduka ya matajiri huko Westgate Nairobi.

Kwa sasa, taarifa zilizo nyingi za uzingiraji zimeeleweka: Jumamosi iliyopita kundi la watu wenye silaha la al-Shabaab walivamia kituo kikubwa cha maduka, waliwaua kikatili wanunuzi na kurusha maguruneti kwenye mkusanyiko wa raia wasio na hatia. Hali hiyo iliyodumu kwa siku nne, watu hao wenye silaha waliawaua watu wapatao 67 na kushikilia idadi isiyojulikana ya mateka hadi vikosi vya usalama vya Kenya vilipopata udhibiti wa hali hiyo Jumanne. 

Lakini baada ya tukio hilo, maswali mengi yalibakia bila majibu: Nini kilichotokea kwa mateka waliobakia? Washambuliaji waliwezaje kuingia katika kituo cha maduka na kushikilia kwa muda mrefu? Nani kiongozi katika shambulio hilo na wapi aliko sasa?

Je, vikosi vya usalama na vya upelelezi vilipata tahadhari kabla kuhusu shambulio, na vingeweza kuliepusha? 

"Shambulio la kigaidi halikutokea pasipo mpango," alisema mchambuzi wa masuala ya usalama Raymond Kipkorir Cheruiyot, kanali mstaafu wa vikosi vya jeshi la Kenya na mmiliki shirika wa kampuni ya Multi Security Consultants Limited huko Nairobi.

"Magaidi walitekeleza shambulio wakati wakala wa usalama wakiwa kwenye kujiridhisha," aliiambia Sabahi. "Maduka ya biashara ya matajiri ya Westgate yalikuwa kwenye jengo lenye hadhi kubwa,ambalo lililpaswa kuwa chini ya uchunguzi imara wa usalama kwa saa 24 na kulindwa na polisi wenye silaha. Kwa njia hiyo, mpango wa shambulio hilo ungeweza kugundulika na kuepushwa."


Cheruiyot alikosoa mwitikio usioungana wa serikali ya Kenya wa kile kinachoelezwa kama shambulio lenye utata ambalo "timu yenye ufa ya magaidi" walipanga kwa uangalifu na kulitekeleza.

Mamlaka zinapaswa kuweka lengo lenye thamani kubwa kama hiyo chini ya uchunguzi wa kudumu, kupitia tena mipangilio na taratibu za usalama zilizopo, na kufuatilia wenyeji wanaowaonea huruma pamoja na au kuunga mikono ugaidi, alisema.

"Ndiyo, muda wamwitikio wa timu ya usalama ulikuwa mzuri, lakini utendaji wao ungeweza kuwa mzuri zaidi, kama walivyotenda kwenye tahadhari ya upelelezi ya nje kwamba maduka ya biashara ya matajiri ya Westgate yalikuwa rahisi kulengwa na magaidi," Cheruiyot alisema.

Sunday, September 29, 2013

ALIYETENGENEZA FILAMU YA 'THE INNOCENCE OF MUSLIM' INAYOMKASHIFU MTUME MUHAMMAD SAW, AACHIWA HURU


Mark Youssef Basseley alipokamatwa

Mark Youssef Basseley mtengeneza filamu ya ‘The Innocence of Muslims’ inayomkashifu Mtume Muhammad SAW na iliyosababisha maandamano makubwa duniani na kupelekea vifo vya watu kadhaa pamoja na balozi wa Marekani nchini Libya, ameachiliwa huru alhamisi amethibitisha mwanasheria wake.

Basseley alikuwa anatumikia kifungo cha mwaka mmoja kwa kukiuka masharti ya hukumu iliyotolewa 2010 ya kosa la udanganyifu. Alikuwa akitumikia adhabu hiyo katika kituo cha magereza huko Taxes.

Basseley aliwahi kutupwa jela miaka mitatu iliyopita kutokana na utapeli wa cheki za watu kwa kutumia majina mbalimbali feki. Alikaa jela mwaka mmoja kabla ya kutolewa kwa masharti kumalizia kifungo chake uraiani.Kujihusisha kwake kutengeneza filamu hiyo, kumevunja masharti aliyopewa hivyo akarudishwa jela kutumikia kifungo cha mwaka mmoja jela.

Kwa sasa atakuwa chini ya usimamizi kwa muda wa miaka minne kuangalia mwenendo wake katika jamii, kwa kutorudia makosa aliyotenda au kuiumiza jamii kwa namna yoyote ile. Hata hivyo haijaeleweka wapi ataishi na itakuwaje. Basseley amekuwa akiwindwa vikali na jamii ya kiislamu kwa ajili ya kuadabishwa kwa kile alichokitenda cha kuukashifu Uislamu na Mtume Muhammad SAW.

Basseley, ambaye ni tapeli mwenye kujipa majina mbalimbali mwenye umri wa miaka 56 aliwahi kuhukumiwa kwenda jela miezi 21 nchini Marekani kwa makosa mbalimbali ya utapeli, aliingia mafichoni pamoja na familia yake baada ya maandamano ya kuipinga filamu aliyoitengenza kuzidi kupamba moto.

Basseley alijiita jina la Sam Bacile wakati wa utengenezaji wa filamu ya "The Innocence of Muslims" ambayo trela lake lenye dakina 14 liliwekwa kwenye YouTube na video zake zikimuonyesha mtu aliyeigiza kama Mtume Muhammad, akifanya mapenzi, akibaka na akiamuru kuuliwa kwa watu.

Basseley au Nakoula Basseley Nakoula, hajaonekana hadharani tangu kuitoa filamu hiyo, polisi walimsaidia kumficha kwa kwenda nyumbani kwake kuichukua familia yake ya watu wanne, kisha kumhamisha kwenda mafichoni kusikojulikana. Polisi wa Los Angeles waliwasili majira ya alfajiri kabla jua halijachomoza na walimchukua mke wa Basseley na watoto wake watatu na kuwasindikiza kwenye maficho ya siri ambako Nakoula alikuwa amejificha.
 
Familia yake ilizificha sura zao wakati wakisindikwa na polisi toka kwenye nyumba yao iliyozungukwa na waandishi wa habari wengi waliokuwa wakikesha mbele ya nyumba hiyo.
"Tulichokifanya sisi ni kuwachukua na kuwapeleka sehemu ambayo Basseley amejificha", alisema msemaji wa polisi.
 
Baadae mahakama iliamuru akamatwe kwa kosa la kuvunja masharti ya hukumu aliyopewa ya kosa la utapeli. Katika mahojiano aliyowahi kufanya na CNN Basseley alisema,  “kamwe sikufikiria filamu yangu ingeweza kusababisha maumivu kwa watu au kufa kwa sababu ya filamu yangu.”
 
Anasema alitengeneza filamu hiyo ili kuweka wazi ukweli halisi kuhusu Mtume Muhammad SAW katika unyanyasaji wake kwa kivuli cha ishara ya Mwenyezi Mungu.
Mark Youssef Basseley picha ya kuchorwa akiwa mahakamani
Akiwa na msanii wake aliyeigiza filamu ya Innocence of Muslims

Sunday, September 22, 2013

NAIROBI WESTGATE SHOOT-OUT KILLS OVER 11 IN KENYA

A number of suspected Somali al-Shabab militants stormed the Westgate shopping centre in the Kenyan capital, Nairobi, on Saturday throwing grenades and firing automatic weapons.


Eleven people have died in a gun battle inside a Nairobi shopping centre, says a senior Kenyan security official.

Mutea Iringo blamed "armed criminals" and said police were in control of a "very serious situation". Officers are going shop to shop to secure the area. The Kenyan Red Cross says 30 died.

Eyewitnesses saw armed men in black entering the Westgate shopping centre on Saturday afternoon.

The Somali militant group al-Shabab has said it carried out the attack.

On its Twitter feed, the al-Qaeda-linked group said it confirmed it was behind what it called the "Westgate spectacle".

Al-Shabab has carried out a string of attacks in Kenya since 2011, when Kenyan troops moved into southern Somalia to fight the militants there.

Some eyewitnesses told AFP news agency they had heard the gunmen speaking Arabic or Somali.

Other witnesses said Muslims were told to leave and that non-Muslims would be targeted.

"They came and said: 'If you are Muslim, stand up. We've come to rescue you," said Elijah Lamau.

He said the Muslims left with their hands up, and then the gunmen shot two people.

The US state department says it has reports that American citizens were injured in what it called "a senseless act of violence".

 
For More pictures and videos on the incident kindly follow this link .....

Friday, September 20, 2013

DK. SLAA AVUNJA UONGOZI MZIMA WA CHAMA WILAYANI KYELA!



Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod Slaa, amevunja uongozi mzima wa chama hicho wilayani Kyela kwa madai kuwa viongozi hao hawakuwa waadilifu.

Badala yake, Dk. Slaa amekabidhi ofisi na mali za chama kwa Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Mbeya, Peter Mwamboneke, ambaye pia amepewa siku saba kuhakikisha anaandaa uchaguzi wa kujaza nafasi za viongozi hao.

Uamuzi huo ulitangazwa na Dk. Slaa kwenye mkutano wa hadhara mjini Kyela ulioandaliwa na chama hicho kwa ajili ya kutoa elimu ya umuhimu wa kushiriki kwenye mchakato wa upatikanaji wa Katiba iliyo bora kwa maisha ya Watanzania.

Alisema Chadema kwa sasa ni chama imara kilichokomaa na kuwa viongozi wanaopewa dhamana ya kuwaongoza wananchi kupitia chama hicho, kamwe hawawezi kufanya kazi kwa kushurutishwa kwa namna yoyote na chama kingine cha siasa nchini.

Aidha, alikemea vikali vitendo vya rushwa kwenye uchaguzi utakaoandaliwa, huku akionya kuwa yeyote atakayebainika ameingia madarakani kwa kutoa rushwa, ataenguliwa mara moja. Kuhusu mchakato wa upatikanaji wa Katiba mpya, Dk. Slaa alisema kinachoonekana hivi sasa ni kwamba Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimeanza kufanya mizengwe ya kuharibu mchakato huo ili Katiba hiyo isipite.

Alisema CCM inatambua kuwa rasimu ya Katiba ikipitishwa kama ilivyoandaliwa na Tume ya Jaji Warioba, utakuwa ni mwisho wa utawala wake na kuwa hivi sasa inatumia kila mbinu kujinusuru na ndiyo sababu ilipitisha kinyemela Muswada wa Sheria wa Mabadiliko ya Sheria ya Katiba bungeni.

Dk. Slaa alisema hivi sasa vyama vya upinzani vimeungana kupinga muswada huo kusainiwa na Rais na kuwaomba wananchi kuwaunga mkono kwenye mapambano hayo.

TANZANIA REJECTS OUTGOING GERMAN ENVOY MARGIT HELLWIG-BOETTE!




NAIROBI, KENYA: Tanzania has rejected the posting of Margit Hellwig-Boette, who has just finished her tour of duty in Kenya as Germany’s ambassador to Dar-es-Salam.

It’s not clear why the government of President JakayaKikwete rejected the envoy, who unlike her predecessors was less controversial, while serving in Nairobi.Margit has confirmed to the Standard that her posting has been rejected and saying she will be leaving to Berlin for redeployment.

“Yes, Tanzania has rejected my appointment. Under Diplomatic Code, a host country reserves the right to give consent for the posting of an envoy or reject.Tanzania has rejected but is not under any obligation to explain the reasons,” she said. The envoy added; “I am leaving Nairobi for Berlin tomorrow (Thursday) morning for redeployment.” Reports indicate that Kikwete’s administration was not keen on taking the diplomat, who has just served in a neighbouring country.

On Thursday night, former Prime Minister Raila Odinga hosted the Germany envoy for a dinner to celebrate the end of her four year tour of duty. During the event, the diplomat said that in Kenya’s 50-year history, the promulgation of the Constitution was the most significant event that promised to propel the country to prosperity.

“In my four-year stay here, I cannot think of anything else the leadership can bequeath the people of Kenya other than the full implementation of the Constitution,” she said.