To Chat with me click here

Friday, December 6, 2013

MANDELA’S DEATH LEAVING THE NATION WITHOUT ITS MORAL CENTER


1st Black President of the Republic of South Africa, Nelson Mandela

JOHANNESBURG — Nelson Mandela, South Africa’s first black president and an enduring icon of the struggle against racial oppression, died on Thursday 5, 2013 the government announced, leaving the nation without its moral center at a time of growing dissatisfaction with the country’s leaders. 

 “Our nation has lost its greatest son,” President Jacob Zuma said in a televised address late Thursday night, adding that Mr. Mandela had died at 8:50 p.m. local time. “His tireless struggle for freedom earned him the respect of the world. His humility, his compassion and his humanity earned him their love.”
Mr. Zuma called Mr. Mandela’s death “the moment of our deepest sorrow,” and said that South Africa’s thoughts were now with the former president’s family. “They have sacrificed much and endured much so that our people could be free,” he said. 

Mr. Mandela spent 27 years in prison after being convicted of treason by the white minority government, only to forge a peaceful end to white rule by negotiating with his captors after his release in 1990. He led the African National Congress, long a banned liberation movement, to a resounding electoral victory in 1994, the first fully democratic election in the country’s history. 

Mr. Mandela, who was 95, served just one term as South Africa’s president and had not been seen in public since 2010, when the nation hosted the soccer World Cup. But his decades in prison and his insistence on forgiveness over vengeance made him a potent symbol of the struggle to end this country’s brutally codified system of racial domination, and of the power of peaceful resolution in even the most intractable conflicts. 

Years after he retreated from public life, his name still resonated as an emblem of his effort to transcend decades of racial division and create what South Africans called a Rainbow Nation. 

“His commitment to transfer power and reconcile with those who jailed him set an example that all humanity should aspire to,” a grim President Obama said Thursday evening, describing Mr. Mandela as an “influential, courageous and profoundly good” man who inspired millions — including himself — to a spirit of reconciliation. 

Mr. Mandela and Mr. Obama both served as the first black leaders of their nations, and both men won the Nobel Peace Prize. But the American president has shied away from comparisons, often noting that his own sacrifices would never compare to the ones that Mr. Mandela endured.

Mr. Obama said that the world would “not likely see the likes of Nelson Mandela again,” and he noted that the former South African president had once said that he was “not a saint, unless you think of a saint as a sinner who keeps on trying.” 

Mr. Zuma did not announce the specific cause of Mr. Mandela’s death, but he had battling pneumonia and other lung ailments for the past six months, and had been in and out of the hospital. Though his death was announced close to midnight, when most in this nation of early risers are asleep, a small crowd quickly gathered outside the house where he once lived in Soweto, on Vilekazi Street. 

“Nelson Mandela, there is no one like you,” they sang, stamping their feet in unison to a praise song usually sung in joy. But in the midnight darkness, sadness tinged the melody. 

“He was our father, our mother, our everything,” said Numfundo Matli, 28, a housekeeper who joined the impromptu celebration of Mr. Mandela’s life. “What will we do without him?” 

His death comes during a period of deep unease and painful self-examination for South Africa.
In the past year and a half, the country has faced perhaps its most serious unrest since the end of apartheid, provoked by a wave of wildcat strikes by angry miners, a deadly response on the part of the police, a messy leadership struggle within the A.N.C. and the deepening fissures between South Africa’s rulers and its impoverished masses. 

Scandals over corruption involving senior members of the party have fed a broader perception that Mr. Mandela’s near saintly legacy from the years of struggle has been eroded by a more recent scramble for self-enrichment among a newer elite. 

After spending decades in penurious exile, many political figures returned to find themselves at the center of a grab for power and money. Mr. Zuma himself was charged with corruption before rising to the presidency in 2009, though the charges were dropped on largely technical grounds. He has faced renewed scrutiny in the past year over $27 million spent in renovations to his house in rural Zululand. 

Mr. Mandela served as president from 1994 to 1999, stepping aside to allow his deputy, Thabo Mbeki, to run and take the reins. Mr. Mandela spent his early retirement years focused on charitable causes for children and later speaking out about AIDS, which has killed millions of Africans, including his son Makgatho, who died in 2005. 

Mr. Mandela retreated from public life in 2004 at the age of 85, largely withdrawing to his homes in the upscale Johannesburg suburb of Houghton and his ancestral village in the Eastern Cape, Qunu.

Thursday, November 14, 2013

KAGASHEKI ANASWA KONTENA LA PEMBE ZA NDOVU

Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamisi Kagasheki
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki, amekamata kontena la futi 40 likiwa limesheheni pembe za ndovu kisiwani Unguja, Zanzibar jana alasiri.
Akizungumza na vyanzo vya habari hii kwa simu jana kutoka kisiwani humo, Waziri Kagasheki alisema kuwa kontena hilo lilikuwa likitokea Bandari ya Dar es Salaam na kwamba watu wawili wanashikiliwa kwa mahojiano zaidi wakilisaidia Jeshi la Polisi.
Waziri Kagasheki alisema kuwa hadi sasa haijulikani mzigo huo una thamani kiasi gani na kwamba unasadikiwa kumilikiwa na raia wa China.
Alisema kuwa operesheni hiyo ni endelevu ili kuwabaini wahusika wanaojihusisha na biashara hiyo haramu ya ujangili.
Tukio hilo linakuja zikiwa ni wiki mbili tangu waziri huyo kukamata pembe za ndovu 706 jijini Dar es Salaam zikimilikiwa na raia wa China.
Pembe hizo 706 ni sawa na tembo 353 waliouawa katika hifadhi za wanyamapori hapa nchini.
Wachina hao walikamatwa katika Mtaa wa Kifaru, Mikocheni wilayani Kinondoni chini ya operesheni iliyoongozwa na Waziri Kagasheki, ambaye aliambatana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Tarish Maimuna.
 
Waliokamatwa na shehena hiyo ya pembe za ndovu ni raia watatu wa China, ambao ni Xu Fujie, Chen Jinzha na Huang Qin wote kutoka mji wa Guandung, ambao wamefikishwa mahakamani wiki iliyopita.

KASHFA NZITO TUME YA UCHAGUZI

Naibu Katibu Mkuu Chadema - Mhe. Zitto Kabwe
TUME ya Uchaguzi nchini (NEC) inadaiwa kuingia katika mchakato wa mwisho wa kuzipa zabuni ya kuandaa vifaa vya Uchaguzi Mkuu mwaka 2015 kampuni za M/S Jazzmatrix Cooperation na M/S Invu IT Solution zinazodaiwa kuwa na rekodi mbaya ya utendaji.

Tanzania Daima limedokezwa kuwa mkakati huo unahusishwa na  njama za kutaka kukibeba Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi huo kwa kuchakachua matokeo ya kukibakiza madarakani.

 Kampuni hizo ambazo katika zabuni ya Tume ya Uchaguzi zimetajwa kushirikiana na Kampuni ya Kitanzania ya M/S SCI Tanzania Limited, mbali ya kutojulikana zinapotoka, pia ndizo zimekuwa na gharama kubwa kuliko kampuni nyingine zilizoomba kazi hiyo.

Kiwango ambacho kampuni hizo zilitaja na kukubaliwa na NEC kwa ajili ya kuandaa vifaa vya kielektroniki vya kusajili wapiga kura (Biometric Voters Registration) ni zaidi ya euro milioni 60, sawa na sh bilioni 126.3, wakati kampuni zinazofuata zikihitaji kuanzia euro milioni 40.

Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Zitto Kabwe, ni mmoja wa viongozi waliofichua mkakati huo, akidai unafanywa na serikali ya CCM ili kuhakikisha wanajiandaa kudhibiti kila eneo ili waweze kubaki madarakani.

Alisema lengo ni kuhakikisha mchakato wa vitambulisho vya kupigia kura vya kielektroniki vina kuwa na faida kwa CCM na kukiingizia fedha chama hicho za kutumia kwenye uchaguzi huo kupitia mfumo huo dhaifu wa vitambulisho hivyo.

Zitto alisema kutokana na hali hiyo, amemwandikia Mdhibiti na Mkaguzi  Mkuu wa Serikali (CAG) barua ya kutaka ukaguzi wa zabuni hiyo ufanyike kwa kushirikisha Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na vyombo vingine vya usalama kwa ajili ya kujiridhisha.

“Wenzetu CCM wanafanya mikakati ya kujiandaa na Uchaguzi Mkuu wa 2015 kwa kuhakikisha wanapata fedha za kutosha na hata mazingira mabaya ya vifaa vitakavyotumika katika upigaji kura na sasa wameshaingia hata katika Tume ya Uchaguzi kwa ajili ya kutengeneza mazingira,” alisema Zitto.

Aliongeza kuwa kiasi kilichotolewa ni kodi ya Watanzania na kwamba ni vema taifa likajiridhisha kuwa matatizo yaliyotokea Kenya na Ghana hayatajirudia Tanzania, hasa wakati wa upigaji kura.

 Gazeti hili limeona barua hiyo ya Zitto kwenda kwa CAG, ya Novemba 7, 2013, yenye kichwa cha habari; ‘Zabuni ya  Biometric Voters Registration (BRV KITS) No. IE/018/2012-13/HQ/G/19 yenye thamani ya sh bilioni 126.3.’

Zitto ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini anasema kuwa  NEC imekuwa katika mchakato wa zabuni tajwa hapo juu.

“Zabuni hiyo sasa imeanza kuleta malalamiko miongoni mwa wananchi kutokana na kinachosemekana kuwa kampuni iliyopewa zabuni hiyo haina uwezo kiteknolojia, pia bei zao ni kubwa.

“Katika mafunzo ya hivi karibuni ya SADCOPAC jijini Nairobi tuliazimia kuwa ni vema kwenye zabuni nyeti kama za namna hii, SAIs wawe na uwezo wa kufanya ukaguzi kabla ya zabuni kutolewa na kuanza kutekelezwa,” alisema.

Tuesday, November 12, 2013

JOHN MNYIKA AZUNGUMZA JUU TAARIFA YA SIRI YA CHADEMA KUHUSU ZITTO KABWE KUPOKEA PESA KUTOKA CCM ILI KUIHARIBU CHADEMA

Katibu Mwenezi wa Chadema; John Mnyika
Mgogoro ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), umeingia katika sura mpya baada ya viongozi wake wawili waandamizi, Naibu Katibu Mkuu, Zitto Kabwe na Mjumbe wa Kamati Kuu, Dk Kitila Mkumbo kuuandikia uongozi wa chama hicho wakitaka uikane taarifa inayowachafua mitandaoni.
Zitto na Dk Mkumbo wanatuhumiwa kupokea fedha na kushirikiana na viongozi wa Idara ya Usalama wa Taifa na wale wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa nia ya kuivuruga Chadema.
Taarifa hiyo yenye kichwa cha habari 'Ripoti ya siri juu ya Zitto Kabwe’, ambayo imesambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii katika siku za karibuni inadaiwa kuwa iliandaliwa na Kitengo cha Upelelezi cha Chadema baada ya uchunguzi wa mwenendo wa Zitto ndani na nje ya nchi kuanzia mwaka 2008.
Sehemu ya taarifa hiyo ya mtandaoni inadai kuwa Zitto alipelekewa kiasi cha Dola za Marekani 266,000 (Sh416 milioni) huko Ujerumani na maofisa wa Usalama wa Tanzania, Desemba 16, 2009.
 
Ripoti hiyo inadai kuwa fedha hizo zilipitishwa katika Benki ya Berliner ya Ujerumani kwenye akaunti ya raia wa nchi hiyo, Andrea Cordes, ambaye anadaiwa kumpelelekea Zitto.
 
Taarifa zaidi zinadai kuwa fedha hizo ziligawiwa kwa wafuasi mbalimbali wa chama hicho na miongoni mwao ni Dk Mkumbo.
Zitto amlima barua Dk Slaa
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, Zitto alisema amemwandikia barua Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willbrod Slaa kumwomba athibitishe ‘Taarifa ya Siri ya Chadema’ kama ni ya kweli au chama hicho kiikanushe ili aweze kuchukua hatua za kisheria dhidi ya waandishi wa kile alichokiita ‘hekaya.’

“Taarifa ya Chadema inasema kwamba chama hicho (chama changu), kilikuwa kimechunguza mwenendo wangu tangu mwaka 2008 hadi 2010 na kubaini kuwa mimi ninapokea fedha kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili kuivuruga Chadema,” alisema Zitto kwenye taarifa yake.
Zitto alisema taarifa hiyo ni ya kutunga na iliyojaa uongo wa kiwango cha kutisha, imemfedhehesha, imemsikitisha na kumkasirisha.
Alisema taarifa hiyo iliibuliwa katika kipindi ambacho alikuwa ziarani barani Ulaya katika nchi za Uswisi na Uingereza ambako alikuwa anafuatilia fedha zilizofichwa na Watanzania katika nchi hizo.

“Pengine lengo la ripoti hiyo lilikuwa ni kutaka kunipoteza kutoka katika nia na dhamira yangu ya dhati ya kutaka Watanzania wafaidike na utajiri wao. Muda ambao watunzi wa ripoti hiyo waliamua kutoa taarifa yao unazua maswali mengi kuliko majibu,” alieleza Zitto katika taarifa yake.
 
Dk Mkumbo alia na uenezi
Dk Mkumbo alieleza kusikitishwa na Idara ya Uenezi ya Chadema kwa kukaa kimya bila kutoa maelezo juu ya suala hilo.
“Hasa pale ambapo tumeambiwa waraka huu umetoka makao makuu. Hii si kawaida kwa idara yetu hii nyeti iliyosheheni watu mahiri. Mara zote huwa wepesi kabisa kwa vijana wetu katika idara hii kutoa ufafanuzi, tena kwa mambo mepesi kabisa yanayokigusa chama, vipi makamanda kwenye jambo hili imekuwaje?” aliandika Dk Mkumbo kwenye ukurasa wake wa mtandao wa Facebook jana na kuthibitisha kwa simu. Dk Kitila alisema pamoja na umaskini wake, hajawahi kuhongwa popote na wala hatarajii.
 
“Taarifa zinazosambazwa kuhusu mimi ni za uongo wa kijinga na uzushi wa kitoto kwa malengo ya siasa nyepesi. Ni wazi kwamba wanaosambaza habari chafu kunihusu hawanijui na ndiyo maana wanaweza kudiriki kuzusha kwamba mimi Kitila Mkumbo naweza kuhongwa Sh200,000.”
 
Alihoji pia Chadema ilikuwa na siri gani za hatari kiasi cha kumfanya Zitto, ambaye ni rafiki yake wa siku nyingi kuhongwa kiasi hicho kikubwa cha fedha.

Mnyika awajibu
Hata hivyo, Katibu Mwenezi wa Chadema, John Mnyika ameikana ripoti hiyo na kueleza kuwa haijaandikwa na makao makuu ya Chadema.
Mnyika alisema Zitto ameibua kitu ambacho anafahamu kuwa kimeshughulikiwa na uongozi wa chama hicho.
 
“Zitto anajua kuwa Andrea Cordes aliniandikia baruapepe na nakala kwake nikawajibu kuwa ripoti hiyo haijaandikwa na Makao Makuu ya chama na tukipokea malalamiko rasmi tutachunguza kwa sasa chama kinaichukulia ripoti hiyo kama ripoti nyingine zinazosambazwa mitandaoni,” alifafanua Mnyika.

Akizungumzia malalamiko ya Dk Mkumbo, Mnyika alisema alikuwa anapaswa kufuata taratibu za chama kama alikuwa na malalamiko.
Alisema baada ya taarifa hiyo ya siri kusambaa mtandaoni, Zitto alitoa kauli na kama Dk Mkumbo hakuridhika, alipaswa kuonana na watu wa Idara ya Uenezi ya Chadema.

“Idara ingetoa ufafanuzi zaidi. Mjadala huu usikuzwe bila sababu za msingi na kufunika masuala mengine muhimu ya kitaifa,” alisema Mnyika. 
Chanzo: Mwananchi

Tuesday, October 22, 2013

UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA UFANYIKE 2015


Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Warioba  

Jana  gazeti la Mwananchi lilichapisha habari katika ukurasa wa kwanza ikisema Tume ya Mabadiliko ya Katiba imeomba kuongezewa muda wa mwezi mmoja kutokana na ugumu wa kazi ya uchambuzi wa maoni yaliyotolewa na wananchi na asasi mbalimbali. Kama mambo yangekwenda kama ilivyotarajiwa hapo awali, Tume hiyo iliyoanza kazi Mei 1 mwaka jana, chini ya Jaji Joseph Warioba ingekamilisha kazi yake Novemba 1, mwaka huu.

Kwa mujibu wa Sura ya 83 ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Tume hiyo ilitakiwa kufanya kazi kwa miezi 18. Hata hivyo, Makamu Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Augustino Ramadhan alisema juzi kwamba wamepeleka serikalini ombi la kuongezewa muda wa kufanya kazi kutokana na kukabiliwa na kazi ya ziada ya kuchambua maoni hayo. Pamoja na Serikali kukiri kupokea ombi hilo, hadi tunakwenda mitamboni jana ilikuwa haijatoa jibu la kulikubali wala kulikataa.

Sisi hatuoni sababu yoyote inayoweza kuisukuma Serikali kulikataa ombi hilo, hasa kutokana na kujitokeza kwa mambo mengi ambayo hayakutarajiwa kabla na wakati wa mchakato wa Katiba Mpya. Mikutano ya Mabaraza ya Katiba iliyofanyika nchi nzima, kwa mfano ilizua tafrani kubwa ambapo wajumbe wa mabaraza hayo waligawanyika kwa misingi ya kisiasa na kiitikadi. Tume hiyo ililazimika kutumia muda mwingi kujielekeza katika kutoa tafsiri na kufafanua vifungu katika Rasimu ya Kwanza ya Katiba. Pia Tume ilitumia muda mrefu kuratibu mijadala ya Rasimu hiyo, kwani wajumbe wengi wa mabaraza hayo walikuwa wakijadili hoja zilizotokana na misimamo ya vyama vyao badala ya kujadili rasimu yenyewe.

Hivyo, Serikali haina budi kukubali ombi hilo la tume haraka iwezekanavyo, pamoja na ukweli kwamba kuiongezea tume mwezi mmoja kuchambua maoni ya wananchi na asasi mbalimbali ni kuongeza gharama za mchakato huo. Lakini, wahenga waliposema maji ukiyavulia nguo ni sharti uyaoge, walipatia kabisa usemi huo, kwani kama tumeamua kama taifa kupata Katiba Mpya itakayotuvusha miaka 50 mingine ijayo lazima tubebe gharama hizo za kutuletea demokrasia ya kweli.

Ni vyema tukatambua kwamba hatua ya tume ya kuomba kuongezewa mwezi mmoja siyo ya ajabu. Sheria inaipa tume hiyo fursa ya kuongezewa miezi miwili nje ya muda uliowekwa. Kinachotakiwa sasa ni Serikali kujipanga vizuri na kutekeleza mambo mbalimbali kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu wa 2015. Mambo hayo ni pamoja na kuandaa, kurekebisha na kupitisha sheria mbalimbali kwa lengo la kuondoa sheria kandamizi na kuweka sheria zitakazowezesha kuwapo mazingira linganifu ya ushindani wa kisiasa. Kwa mfano, inahitajika sheria mpya ya Tume Huru ya Uchaguzi.

Moja ya mambo muhimu ambayo Serikali inapata kigugumizi kuyatolea uamuzi ni suala la kufanya uchaguzi wa Serikali za Mitaa sambamba na Uchaguzi Mkuu wa 2015. Muda uliobaki kati ya sasa na 2014 (ambao ulipangwa kufanyika) hautoshi kufanya maandalizi na uchaguzi ulio huru na haki. Uchaguzi huo ni vyema usimamiwe na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi. Hivyo, Tamisemi iliyokuwa ikisimamia chaguzi za Serikali za Mitaa na kusababisha malalamiko mengi kutoka kwa wananchi itakuwa imeondolewa mzigo huo mzito. Kufanya uchaguzi huo wakati mmoja na Uchaguzi Mkuu kutapunguza gharama kwa kiasi kikubwa kama ilivyo katika nchi nyingi barani Afrika na kwingineko.

Monday, October 21, 2013

ZITTO ‘AMGEUZIA KIBAO’ CAG RUZUKU VYAMA VYA SIASA!

Mhe. Zitto Kabwe, Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya PAC
WAZIRI Kivuli wa Fedha na Uchumi, Zitto Kabwe ametaka Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), ichunguzwe kwa uzembe wa kushindwa kukagua hesabu za ruzuku za vyama vya siasa kwa muda wa miaka mitatu.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, Kabwe alisema CAG ameshindwa kukagua ruzuku ya Sh83 bilioni iliyotolewa kwa vyama vya siasa nchini tangu mwaka 2005 hadi 2010.

Alisema ingawa kuna tatizo katika Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, CAG hawezi kumtupia mzigo huo pekee yake kwani naye anahusika.

“Nikiwa Waziri Kivuli wa Fedha na Uchumi, ninamwomba CAG afanye audit (ukaguzi) kwa vyama vyote vya siasa kwa miaka mitatu iliyopita sasa na siyo baada ya miezi sita,” alisema Kabwe na kuongeza:

“Ruzuku ya vyama vya siasa ni eneo ambalo huwa haliangaliwi kabisa na fedha nyingi ya walipa kodi inakwenda katika vyama. Kuanzia mwaka 2005 mpaka 2010 jumla ya Sh 83 bilioni zimetolewa kama ruzuku kwa vyama vya siasa,” alisema Kabwe na kuongeza:

“Fedha zote hizi kwa miaka yote hii, hazikuwa zinakaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, (CAG).”

Kwa mujibu wa Kabwe, ubadhirifu unaoweza kujitokeza kwenye fedha za ruzuku zinazotolewa kwa vyama vya siasa, unatokana pamoja na mambo mengine na CAG kushindwa kukagua ruzuku hizo tangu vyama vianze kuipata mwaka 1996.

“Ndiyo maana kumekuwa na ubadhirifu mwingi wa fedha za ruzuku kwenye vyama takriban vyote hapa nchini,” alisema Zitto.

Alisema mwaka 2008, alipeleka pendekezo la mabadiliko ya Sheria ya Vyama vya Siasa katika Bunge la Novemba kutaka vyama vikaguliwe na CAG.

Alisema pendekezo lake lilisomeka: “Vyama vyote vitakaguliwa na CAG na itakuwa ni jukumu la vyama vya siasa kupeleka taarifa zao kwa CAG kwa mujibu wa sheria.”

“Hivyo tangu mwaka 2008 vyama vinatakiwa vikaguliwe na CAG kwa mahesabu yao lakini mpaka sasa hakuna chama ambacho kimeshakaguliwa,” alisema Zitto na kuongeza:

“CAG mwaka huu amelalama tu kwenye taarifa yake kuwa vyama havikupeleka taarifa zao kwa Msajili. Ametoa miezi sita ili wasahihishe makosa? miezi sita ili watafute nyaraka za kugushi ili kuyaweka mahesabu sawa?” alihoji.
Kabwe alisema kauli ya CAG kwamba hahusiki kuvikagua vyama vya siasa ni kukwepa majukumu kwani sheria ya sasa inamtaka afanye hivyo kwa kuteua wawakilishi.

“Hakuna sababu kwa CAG kutoa miezi sita kwa vyama, bali vyama sasa viheshimu Public Audit Act,(Sheria ya Ukaguzi wa Fedha za Umma), Public Finance Act (Sheria ya Fedha za Umma) and (na) Political Parties Act (Sheria ya Vyama vya Siasa)”

Kwa mujibu wa Kabwe, CAG anapaswa kudai mahesabu kutoka kwa vyama na wala si kusema kuwa hahusiki na watu binasi. “Vyama siyo ‘individuals’, vyama ni taasisi,” alisema.

“Kwa sheria mpya, wakaguzi wa vyama wanapaswa kuteuliwa na CAG na siyo vyama kwenda kuokota wakaguzi na kuweka hesabu zao kama ambavyo imezoeleka,” alisema.

Zitto alisema vyama vya siasa ndivyo vinavyounda Serikali, hivyo iwapo haviheshimu fedha za walipa kodi, Serikali wanazounda haziwezi kuheshimu fedha za walipa kodi.

“Ruzuku iliyotolewa kwa vyama mwaka 2010 ilikuwa ni mara tatu ya Bajeti ya Wizara ya Afrika Mashariki au ni zaidi ya Bajeti ya Wizara ya Viwanda na Biashara. CAG ni lazima afanye kazi yake,” alisema na kuongeza:

“Msajili wa Vyama naye achunguzwe, ofisi yake inafanya kazi kwa mujibu wa sheria, kwa nini hakuwa na taarifa za vyama vya siasa wakati yeye ndiye mwenye jukumu la kusimamia vyama.”
“Iwapo anashindwa kusimamia ruzuku kukaguliwa atawezaje kusimamia matumizi ya fedha kwenye uchaguzi wakati uchaguzi uligubikwa na matumizi ya fedha nyingi za kifisadi,” alidai Zitto.

Ripoti ya CAG iliyoishia Juni 30 mwaka 2010, imeeleza kuwa vyama sita vyenye wawakilishi bungeni vimeshindwa kuonyesha taarifa za matumizi ya ruzuku ya Sh17.14 bilioni.

Vyama hivyo ni CCM, CUF, Chadema, NCCR-Mageuzi, TLP na UDP. Katika hesabu za kawaida kuhusu fedha hizo, chama hicho tawala kimepata mgawo wa Sh12 bilioni kutokana na asilimia 70 ya mgawo.

CUF kinachopata asilimia 20 ya ruzuku kimepata mgawo wa Sh3.43 bilioni, Chadema chenye asilimia nane Sh1.37 bilioni na vyama vitatu vinavyoshikilia asilimia mbili Sh343 milioni.

Akijibu Madai hayo, Utouh alisema: “Sijakwepa majukumu. Fedha zinatoka serikalini, zinakwenda kwa Msajili wa Vyama.”

“Yeye (Msajili), ndiye mwenye kazi ya kuvigawia vyama fedha hiyo na sheria inataka baada ya matumizi, vyama vinapaswa kutengeneza hesabu zake na kuziwakilisha kwa Msajili. Siyo kazi yangu kuvitengenezea mahesabu vyama vya siasa.”

Kuhusu madai ya Zitto kwamba utaratibu huo wa Msajili kukagua vyama uko kwenye sheria ya zamani ambayo Zitto alidai kwamba alishatoa mapendekeza bungeni na kufanyiwa marekebisho, yanayomtaka CAG kuteua wakaguzi wa hesabu za vyama vya siasa, Utouh alisema:

“Mwulize yeye (Zitto) chama chake kilishanipelekea mahesabu ili niyakague kama anajua hivyo ndivyo inavyotakiwa? Tupo hapa kufanya kazi. Hatupo kukwepa majukumu. Mwulize kama hivyo ndivyo sheria inavyotaka Chadema ilishawahi kuniletea mahesabu yake?”

Chanzo: Gazeti la Mwananchi